Skip to main content

Somalia inaangalia kuendelea na maendeleo kwa msaada kutoka mkutano wa London


Na Abdi Moalim, Mogadishu
Baada ya mikutano mingi wiki hii katika mkutano wa London kuhusu Somalia, Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud na mawaziri wake wamerudi nyumbani wakiwa na ahadi kutoka jumuiya za kimataifa ya takribani dola milioni 450 kusaidia miradi mingi.
Wakaazi wa Mogadishu waliandamana mitaa Jumanne (tarehe 7 Mei) kuonyesha kuunga mkono mkutano wa London kuhusu Somalia. [Abdi Said/Sabahi]
Katika hotuba yake ya ufunguzi kwenye mkutano huo, Mohamud alilinganisha Somalia na mti mchanga uliooteshwa huko Villa Somalia ambao unahitaji kumwagiliwa. kutunzwa na kulindwa dhidi ya wanyama.
"Kipindi cha kwanza cha ukuaji mara zote ni chenye hatari sana, ambapo msaada mkubwa na ulinzi unahitajika," alisema.
"Tunahitaji ulinzi dhidi ya wale wanaojaribu kutuangamiza kabisa," alisema. "Kwa pamoja, tunaweza kufanya Somalia kuwa imara tena -- mti mrefu uliosimama katika msitu wa Afrika ukiwa na mizizi mirefu uliokingwa kwa usalama katika kanda yake na kutoa kivuli kwa watu wake wakati wakijenga tena maisha yao."
Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon akipunga mkono kwa wakaazi wa Mogadishu waliojitokeza Jumanne (tarehe 7 Mei) kuonyesha kuunga kwao mkono mkutano wa kimataifa kuhusu Somalia huko London. [Abdi Said/Sabahi]
Jumuiya za kimataifa zilijibu mwitikio wa Mohamud kwa kuahidi mamia ya mamilioni ya dola. Pia ziliidhinisha mipango ya kina yaliyowasilishwa na mawaziri wa Somalia, na kuahidi utaalamu na ufadhili wa fedha ili kuzitekeleza.
Kwenye mkutano huo, serikali ya Uingereza iliahidi dola milioni 277, ambapo dola milioni 54 zitaelekezwa kwenye miradi kushughulikia changamoto ya usalama wa Somalia na serikali, na dola milioni 223 zitasaidia Somalia kukabiliana na njaa kwa siku zijazo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...