Skip to main content

Somalia inaangalia kuendelea na maendeleo kwa msaada kutoka mkutano wa London


Na Abdi Moalim, Mogadishu
Baada ya mikutano mingi wiki hii katika mkutano wa London kuhusu Somalia, Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud na mawaziri wake wamerudi nyumbani wakiwa na ahadi kutoka jumuiya za kimataifa ya takribani dola milioni 450 kusaidia miradi mingi.
Wakaazi wa Mogadishu waliandamana mitaa Jumanne (tarehe 7 Mei) kuonyesha kuunga mkono mkutano wa London kuhusu Somalia. [Abdi Said/Sabahi]
Katika hotuba yake ya ufunguzi kwenye mkutano huo, Mohamud alilinganisha Somalia na mti mchanga uliooteshwa huko Villa Somalia ambao unahitaji kumwagiliwa. kutunzwa na kulindwa dhidi ya wanyama.
"Kipindi cha kwanza cha ukuaji mara zote ni chenye hatari sana, ambapo msaada mkubwa na ulinzi unahitajika," alisema.
"Tunahitaji ulinzi dhidi ya wale wanaojaribu kutuangamiza kabisa," alisema. "Kwa pamoja, tunaweza kufanya Somalia kuwa imara tena -- mti mrefu uliosimama katika msitu wa Afrika ukiwa na mizizi mirefu uliokingwa kwa usalama katika kanda yake na kutoa kivuli kwa watu wake wakati wakijenga tena maisha yao."
Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon akipunga mkono kwa wakaazi wa Mogadishu waliojitokeza Jumanne (tarehe 7 Mei) kuonyesha kuunga kwao mkono mkutano wa kimataifa kuhusu Somalia huko London. [Abdi Said/Sabahi]
Jumuiya za kimataifa zilijibu mwitikio wa Mohamud kwa kuahidi mamia ya mamilioni ya dola. Pia ziliidhinisha mipango ya kina yaliyowasilishwa na mawaziri wa Somalia, na kuahidi utaalamu na ufadhili wa fedha ili kuzitekeleza.
Kwenye mkutano huo, serikali ya Uingereza iliahidi dola milioni 277, ambapo dola milioni 54 zitaelekezwa kwenye miradi kushughulikia changamoto ya usalama wa Somalia na serikali, na dola milioni 223 zitasaidia Somalia kukabiliana na njaa kwa siku zijazo.

Comments