kutoka bungeni dodoma
Na Zawadi Msalla
Vyombo vya Habari nchini vimeaswa kutumia uhuru wake vizuri bila kusababisha madhara ndani ya nchi kama ilivyotokea katika baadhi ya nchi za Afrika.
Akichangia hotuba ya wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mhe.Jaddy Simayi Jaddy mbunge wa Mkwajuni alisema baadhi ya vyombo vya habari vilivyopo hapa nchini vinaweza kuchangia machafuko ndani ya nchi kwani mwelekeo wa mambo yanayoandikwa yana dalili ya uchochezi.
Comments