Skip to main content

ALIVYOFUNGUKA DIAMOND :NAMPENDA PENNY KULIKO WEMA



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' amekiri kuwa anampenda zaidi mpenzi wake mpya, Penny Mungilwa kuliko ilivyokuwa kwa mpenzi wake wa zamani, Wema Sepetu.

Diamond alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, mapenzi yake kwa Penny yamemfanya ajione kama vile ameoza kwa binti huyo.

"Ni sawa na kusema treni imegonga mwamba maana kila ninapokuwa naye, nasikia raha ya ajabu, sijui ameniroga. Ananipenda mno,nami nampenda, kwake nimefika,"alisema Diamond.

Msanii huyo nyota wa bongo fleva alisema japokuwa udanganyifu katika mapenzi ni jambo la kawaida, lakini Penny hajawahi kuonyesha dalili hiyo kwake.

Alisema kwa kawaida, mwanamke anapofanya udanganyifu wa mapenzi, inakuwa aibu kwa mwanaume, lakini udanganyifu huo ukifanywa na mwanaume, inakuwa sifa kwake.

"Ni kweli Wema alinipenda, alinionyesha mapenzi ya dhati, lakini alifanya udanganyifu hadharani, alinivunjia heshima, alinivunja moyo, sikupenda kitendo alichokifanya,"alisema Diamond.

Diamond alikanusha madai kuwa, aliwahi kuhusiana kimapenzi na mcheza filamu nyota, Irene Uwoya lakini alikiri kuhusiana kimapenzi na Jokate Mwegelo na Jacqueline Wolper.

Alipoulizwa ni kwa nini amekuwa akipenda kuhusiana kimapenzi na wacheza filamu kuliko wasanii wa fani zingine, Diamond alisema ni kwa sababu amekuwa akikutana nao mara kwa mara sehemu mbalimbali.

"Huwezi kujitosa kimapenzi kwa mtu usiyemfahamu. Hawa ndio ambao nakutana nao mara kwa mara,"alisema.

Je, ni kwa nini wasichana wengi wamekuwa wakimpenda Diamond?

"Unajua mimi nampenda sana mama yangu. Huenda Mungu ananiona na ameamua kunirejeshea upendo huo kupitia kwa watoto wa kike kwa kuwajaza mapenzi kwangu,"alisema.

Diamond alisema yeye ni mstaarabu na amekuwa akijituma katika kazi zake ndiyo sababu hata anapogombana na mpenzi wake, atabaki kumpenda.

Hata hivyo, Diamond alikiri kuwa anajuta kukosana na mpenzi wake wa zamani, Jokate kwa vile ni mwanamke mstaarabu na asiyekuwa na doa.

"Kusema kweli, Jokate hakuwahi kunikosea. Ni mtoto asiye na kosa lolote. Nilimfuata mwenyewe, nikampenda, lakini nilimkosea,"alisema Diamond.

Aliitaja sababu kubwa iliyomfanya agombane na Jokate kuwa ni uamuzi wake wa kurudiana kimapenzi na Wema.

"Nilikuwa nimegombana na Wema, tukarudiana, Jokate hakuufurahia uamuzi huo, sijui nilirogwa, sijui ilikuwa ni utoto, maana ujana ukizidi sana ni matatizo! Hajawahi kunikosea. Ni mstaarabu na ana maisha mazuri,"alisema.

Diamond alisema hajawahi kumuomba msamaha Jokate kwa kosa hilo kwa sababu hadi sasa anajisikia aibu kufanya hivyo.

Wakati huo huo, Diamond amesema amekubali kucheza filamu na Wema kutokana na muandaaji wake kumlipa kiasi kikubwa cha pesa.

"Sidhani kama kuna mcheza filamu wa Tanzania aliyewahi kulipwa fedha nyingi kiasi hiki na tayari nimeshalipwa. Hata katika muziki, sijawahi kulipwa pesa nyingi kiasi hiki,"alisema.

Diamond alisema awali, alimueleza muandaaji wa filamu hiyo wasiwasi aliokuwa nao kuhusu kucheza filamu hiyo na Wema, lakini baadaye akagundua kwamba hiyo ni kazi.

"Kuna watu waliokuwa na uhusiano wa kimapenzi, wakatengana lakini baadaye wakaja kufanya shughuli nyingi pamoja,"alisema msanii huyo.

Katika hatua nyingine, Diamond amesema akaunti yake benki haijawahi kupungua sh. milioni 100.

Alisema akaunti yake inapopungua pesa, huwa anachanganyikiwa na kuongeza kuwa, alianza kuwa na kiasi hicho cha pesa benki tangu 2011.

"Ukipiga hesabu, huu sasa ni mwaka 2013. Hapa nazungumzia zaidi ya bilioni moja benki,"alisema.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...