Skip to main content

ALIVYOFUNGUKA DIAMOND :NAMPENDA PENNY KULIKO WEMA



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond' amekiri kuwa anampenda zaidi mpenzi wake mpya, Penny Mungilwa kuliko ilivyokuwa kwa mpenzi wake wa zamani, Wema Sepetu.

Diamond alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, mapenzi yake kwa Penny yamemfanya ajione kama vile ameoza kwa binti huyo.

"Ni sawa na kusema treni imegonga mwamba maana kila ninapokuwa naye, nasikia raha ya ajabu, sijui ameniroga. Ananipenda mno,nami nampenda, kwake nimefika,"alisema Diamond.

Msanii huyo nyota wa bongo fleva alisema japokuwa udanganyifu katika mapenzi ni jambo la kawaida, lakini Penny hajawahi kuonyesha dalili hiyo kwake.

Alisema kwa kawaida, mwanamke anapofanya udanganyifu wa mapenzi, inakuwa aibu kwa mwanaume, lakini udanganyifu huo ukifanywa na mwanaume, inakuwa sifa kwake.

"Ni kweli Wema alinipenda, alinionyesha mapenzi ya dhati, lakini alifanya udanganyifu hadharani, alinivunjia heshima, alinivunja moyo, sikupenda kitendo alichokifanya,"alisema Diamond.

Diamond alikanusha madai kuwa, aliwahi kuhusiana kimapenzi na mcheza filamu nyota, Irene Uwoya lakini alikiri kuhusiana kimapenzi na Jokate Mwegelo na Jacqueline Wolper.

Alipoulizwa ni kwa nini amekuwa akipenda kuhusiana kimapenzi na wacheza filamu kuliko wasanii wa fani zingine, Diamond alisema ni kwa sababu amekuwa akikutana nao mara kwa mara sehemu mbalimbali.

"Huwezi kujitosa kimapenzi kwa mtu usiyemfahamu. Hawa ndio ambao nakutana nao mara kwa mara,"alisema.

Je, ni kwa nini wasichana wengi wamekuwa wakimpenda Diamond?

"Unajua mimi nampenda sana mama yangu. Huenda Mungu ananiona na ameamua kunirejeshea upendo huo kupitia kwa watoto wa kike kwa kuwajaza mapenzi kwangu,"alisema.

Diamond alisema yeye ni mstaarabu na amekuwa akijituma katika kazi zake ndiyo sababu hata anapogombana na mpenzi wake, atabaki kumpenda.

Hata hivyo, Diamond alikiri kuwa anajuta kukosana na mpenzi wake wa zamani, Jokate kwa vile ni mwanamke mstaarabu na asiyekuwa na doa.

"Kusema kweli, Jokate hakuwahi kunikosea. Ni mtoto asiye na kosa lolote. Nilimfuata mwenyewe, nikampenda, lakini nilimkosea,"alisema Diamond.

Aliitaja sababu kubwa iliyomfanya agombane na Jokate kuwa ni uamuzi wake wa kurudiana kimapenzi na Wema.

"Nilikuwa nimegombana na Wema, tukarudiana, Jokate hakuufurahia uamuzi huo, sijui nilirogwa, sijui ilikuwa ni utoto, maana ujana ukizidi sana ni matatizo! Hajawahi kunikosea. Ni mstaarabu na ana maisha mazuri,"alisema.

Diamond alisema hajawahi kumuomba msamaha Jokate kwa kosa hilo kwa sababu hadi sasa anajisikia aibu kufanya hivyo.

Wakati huo huo, Diamond amesema amekubali kucheza filamu na Wema kutokana na muandaaji wake kumlipa kiasi kikubwa cha pesa.

"Sidhani kama kuna mcheza filamu wa Tanzania aliyewahi kulipwa fedha nyingi kiasi hiki na tayari nimeshalipwa. Hata katika muziki, sijawahi kulipwa pesa nyingi kiasi hiki,"alisema.

Diamond alisema awali, alimueleza muandaaji wa filamu hiyo wasiwasi aliokuwa nao kuhusu kucheza filamu hiyo na Wema, lakini baadaye akagundua kwamba hiyo ni kazi.

"Kuna watu waliokuwa na uhusiano wa kimapenzi, wakatengana lakini baadaye wakaja kufanya shughuli nyingi pamoja,"alisema msanii huyo.

Katika hatua nyingine, Diamond amesema akaunti yake benki haijawahi kupungua sh. milioni 100.

Alisema akaunti yake inapopungua pesa, huwa anachanganyikiwa na kuongeza kuwa, alianza kuwa na kiasi hicho cha pesa benki tangu 2011.

"Ukipiga hesabu, huu sasa ni mwaka 2013. Hapa nazungumzia zaidi ya bilioni moja benki,"alisema.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.