Skip to main content

Kesi ya ulipuaji bomu iliyoteguliwa yaweka uhusiano baina ya Kenya na Iran mashakani


Na Julius Kithuure, Nairobi
Tangu mahakama ya Kenya ilipotoa hukumu kwa raia wawili wa Iran kwenda jela kifungo cha maisha kutokana na mashtaka yanayohusiana na ugaidi mapema mwezi huu, hali ya baadaye ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Nairobi na Tehran imekuwa wa mashaka, kukiwa na uwezekano wa kurudisha nyuma matumaini ya Iran ya kupanua shughuli na uwepo wake kisiasa nchini Kenya kwa miaka ijayo.
Sayed Mansour (katikati) na Ahmad Mohammed (kulia), wote wawili ambao ni raia wa Iran, wanafungwa pingu mara tu baada ya kuhukumiwa kifungo cha maisha jela hapo tarehe 6 Mei kutokana na mashtaka yanayohusiana na ugaidi, ikiwa ni pamoja na kumiliki iliyodaiwa kuwa milipuko kwa ajili ya kutumia katika mashambulio ya bomu. [Simon Maina/AFP]
Mgogoro huo wa kidiplomaisa ulitokana na shambulio la ugaidi lililoteguliwa nchini Kenya ambalo lililotolewa hukumu na mahakama ambalo lilikuwa limepangwa na Ahmed Mohammed, mwenye umri wa miaka 50, na Sayed Mansour, mwenye umri wa miaka 51, wote wawili raia wa Iran. 
Wanaume hao wawili walikamatwa mwezi Juni mwaka uliopita nje ya Laico Regency, hoteli yenye nyota tano inayomilikiwa na Mlibiya katikati ya Nairobi, siku nane baada uchunguzi mkubwa uliofanywa na Kitengo cha Polisi Kinachopambana na Ugaidi.
Tarehe 2 Mei, walitiwa hatiani kwa kumiliki kilogramu 15 za milipuko yenye nguvu ya RDX, ambayo polisi waligundua kufukiwa kwenye uwanja wa gofu. Mahakama ya Nairobi ilisema Mohammed na Mansour walishukiwa kuhusika na ulipuaji bomu uliopangwa na mtandao wa kigaidi huko Mombasa na Nairobi. Wanaume wote hao wawili walikana mashtaka hayo.
Lakini polisi wa Kenya walitetea uamuzi wao wa kuwakamata na kuwafungulia mashtaka Wairani hao wawili.

Comments