Skip to main content

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA KWA VYOMBO VYA HABARI


Police1 b1f97
Watu kumi na tatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi  Mkoani Dodoma kwa tuhuma za mauaji yanayohusisha imani za kishirikina.Watu hao wanashikiliwa kutokana na tukio la mauaji lililotokea siku ya Jumatano tarehe 09/01/2013 majira ya saa 04:00 mchana katika kitongoji cha Mtakuja kata ya  Chitemo katika Wilaya ya Mpwapwa.

Katika tukio hilo  walisababisha kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la NELSON S/O NYAGULU mwenye umri wa miaka 32, mkulima wa Chitemo  kwa kupigwa na risasi ya Bunduki aina ya Gobore tumboni na mtu aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KALANI.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba tarehe 08/01/2013 huko katika kijiji cha Chitemo kulikuwa na mnada, ambapo mvua ilinyesha sehemu moja ya kitongoji cha Mtakuja, sehemu ambayo alikuwa  anaishi mzee mmoja aliyejulikana kwa jina la LEONARD S/O NYAGALU, Miaka 70, Mgogo.
Kwa vile mvua hiyo haikunyesha sehemu kubwa katika kitongoji hicho inasemekana Mwenyekiti wa Kijiji JAVAN S/O MZAZI, Miaka 40, Mgogo, aliibua hoja kuwa kwa nini mvua inyeshe eneo moja tu analokaa Mzee huyo na kuacha kunyesha sehemu nyingine katika eneo hilo na kuwahamasisha wenzake kwenda kwa Mzee Nyagalu akawaeleze vizuri.
Majira ya 23.00 hrs usiku wakakusanyana na kuelekea kwa Mzee  Nyagalu, Walipofika Mzee huyo alisikia watu wakizungumza nyumbani kwake hivyo akavunja ukuta na akatoroka.
Inadaiwa kuwa kundi hilo lililokuwa limeongozana na Mwenyekiti wa Kijiji hicho waliingia ndani ya nyumba na kumkuta mke wa Mzee Leonard Nyagalu na kuanza kumpiga ili aonyeshe aliko mume wake, waliposhindwa kumpata wakabomoa nyumba na kuichoma moto.
Wakati wanafanya tukio hilo, walijitokeza watoto wa Mzee Leonard S/O Nyagalo, mmoja wao akiwa ni NELSON S/O NYAGALU, Miaka 32, Mgogo na ndipo nao wakaanza kupigwa.
Kwa mujibu wa watu walikuwa katika tukio hilo walisema ilisikika sauti ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KARANI akisema sasa mmetangaza vita na akafyatua gobore na risasi zikampata NELSON S/O NYAGALU tumboni zilizopelekea kupoteza maisha wakati anapata matibabu.
Baada ya kufyatua risasi toka katika gobole Bw. RASHID S/O KARANI aliwaaga wenzake kuwa anakwenda kujisalimisha Polisi lakini hadi sasa hajaonekana na jitihada za kumtafuta pamoja na silaha aliyotumia zinaendelea.
Majina ya wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na kushiriki katika tukio hilo  ni kama ifuatavyo:-
1.  Dickson S/O Chimosa, Miaka 52, Mgogo, Mkulima na Mkazi wa Chitemo.
2.  Javan S/O Mzazi, Miaka 44, Mgogo, Mwenyekiti wa Chitemo.
3.  Robert S/O Lusije, Miaka 51, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
4.  Donald S/O Mponi, Miaka 33, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
5.  Daniel S/O Mwamba, Miaka 24, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
6.  Maneno S/O Ngaile, Miaka 36, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
7.  Thomaso S/O Nyagalo, Miaka 28, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
8.  Gilbert S/O Lugaje, Miaka 39, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
9.  Aden S/O Simon, Miaka 33, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
10.      Malolo S/O Sanja, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
11.      Sospeter S/O Sanja, Miaka 35, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
12.      Jocktan S/O Chilomo, Miaka 40, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
13.      Keneth S/O Ngaile, Miaka 38, Mnyamwezi, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.

Aidha siku ya Jumamosi tarehe 05/01/2013 majira ya 08:00 asubuhi kulikuwa na tukio la mauji  lililotokea katika Kitongoji cha Magungu, Kijiji cha Mpendo, Kata ya Mpendo Tarafa ya Kwa Mtoro Wilaya ya Chemba Mkoa wa Dodoma.
Ambapo mtoto mmoja aliyetambulika kwa jina la TONY S/O SOKOINE mwenye umri wa miaka miwili na nusu (2.5), mkazi wa Kijiji cha Mpendo alifariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa kuchomwa na kisu shingoni kilichorushwa na mtoto mwenzake aliyefahamika kwa jina la SOMEI S/O REMENDA mwenye umri wa miaka mine (4) mkazi wa Kijiji cha Mpendo.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha Kifo hicho ni kwamba marehemu na mtuhumiwa walikuwa wanacheza nje nyumbani kwao kwa akina SOKOINE S/O RENENDA ambapo mtuhumiwa alirusha kisu kwa lengo la kumuua ndege aliyekuwa juu ya mti  uliokuwa karibu na nyumba yao, ndipo kisu huchi kiligonga kwenye mti huo na wakati kinadondoka kilimjeruhi marehemu kwa kumchoma shingoni  na kusababisha kifo chake.

DAVID A. MISIME - ACP
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA DODOMA    

CONTACT:
POLISI MKOA WA DODOMA
DAWATI LA HABARI, ELIMU NA MAHUSIANO,
Phone:  0715 006523, Luppy Kung’alo – Mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)
Phone:  0712  360203, Silyvester Onesmo – Police  Konstebo  (PC)

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...