Skip to main content

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA KWA VYOMBO VYA HABARI


Police1 b1f97
Watu kumi na tatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi  Mkoani Dodoma kwa tuhuma za mauaji yanayohusisha imani za kishirikina.Watu hao wanashikiliwa kutokana na tukio la mauaji lililotokea siku ya Jumatano tarehe 09/01/2013 majira ya saa 04:00 mchana katika kitongoji cha Mtakuja kata ya  Chitemo katika Wilaya ya Mpwapwa.

Katika tukio hilo  walisababisha kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la NELSON S/O NYAGULU mwenye umri wa miaka 32, mkulima wa Chitemo  kwa kupigwa na risasi ya Bunduki aina ya Gobore tumboni na mtu aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KALANI.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba tarehe 08/01/2013 huko katika kijiji cha Chitemo kulikuwa na mnada, ambapo mvua ilinyesha sehemu moja ya kitongoji cha Mtakuja, sehemu ambayo alikuwa  anaishi mzee mmoja aliyejulikana kwa jina la LEONARD S/O NYAGALU, Miaka 70, Mgogo.
Kwa vile mvua hiyo haikunyesha sehemu kubwa katika kitongoji hicho inasemekana Mwenyekiti wa Kijiji JAVAN S/O MZAZI, Miaka 40, Mgogo, aliibua hoja kuwa kwa nini mvua inyeshe eneo moja tu analokaa Mzee huyo na kuacha kunyesha sehemu nyingine katika eneo hilo na kuwahamasisha wenzake kwenda kwa Mzee Nyagalu akawaeleze vizuri.
Majira ya 23.00 hrs usiku wakakusanyana na kuelekea kwa Mzee  Nyagalu, Walipofika Mzee huyo alisikia watu wakizungumza nyumbani kwake hivyo akavunja ukuta na akatoroka.
Inadaiwa kuwa kundi hilo lililokuwa limeongozana na Mwenyekiti wa Kijiji hicho waliingia ndani ya nyumba na kumkuta mke wa Mzee Leonard Nyagalu na kuanza kumpiga ili aonyeshe aliko mume wake, waliposhindwa kumpata wakabomoa nyumba na kuichoma moto.
Wakati wanafanya tukio hilo, walijitokeza watoto wa Mzee Leonard S/O Nyagalo, mmoja wao akiwa ni NELSON S/O NYAGALU, Miaka 32, Mgogo na ndipo nao wakaanza kupigwa.
Kwa mujibu wa watu walikuwa katika tukio hilo walisema ilisikika sauti ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KARANI akisema sasa mmetangaza vita na akafyatua gobore na risasi zikampata NELSON S/O NYAGALU tumboni zilizopelekea kupoteza maisha wakati anapata matibabu.
Baada ya kufyatua risasi toka katika gobole Bw. RASHID S/O KARANI aliwaaga wenzake kuwa anakwenda kujisalimisha Polisi lakini hadi sasa hajaonekana na jitihada za kumtafuta pamoja na silaha aliyotumia zinaendelea.
Majina ya wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na kushiriki katika tukio hilo  ni kama ifuatavyo:-
1.  Dickson S/O Chimosa, Miaka 52, Mgogo, Mkulima na Mkazi wa Chitemo.
2.  Javan S/O Mzazi, Miaka 44, Mgogo, Mwenyekiti wa Chitemo.
3.  Robert S/O Lusije, Miaka 51, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
4.  Donald S/O Mponi, Miaka 33, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
5.  Daniel S/O Mwamba, Miaka 24, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
6.  Maneno S/O Ngaile, Miaka 36, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
7.  Thomaso S/O Nyagalo, Miaka 28, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
8.  Gilbert S/O Lugaje, Miaka 39, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
9.  Aden S/O Simon, Miaka 33, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
10.      Malolo S/O Sanja, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
11.      Sospeter S/O Sanja, Miaka 35, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
12.      Jocktan S/O Chilomo, Miaka 40, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
13.      Keneth S/O Ngaile, Miaka 38, Mnyamwezi, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.

Aidha siku ya Jumamosi tarehe 05/01/2013 majira ya 08:00 asubuhi kulikuwa na tukio la mauji  lililotokea katika Kitongoji cha Magungu, Kijiji cha Mpendo, Kata ya Mpendo Tarafa ya Kwa Mtoro Wilaya ya Chemba Mkoa wa Dodoma.
Ambapo mtoto mmoja aliyetambulika kwa jina la TONY S/O SOKOINE mwenye umri wa miaka miwili na nusu (2.5), mkazi wa Kijiji cha Mpendo alifariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa kuchomwa na kisu shingoni kilichorushwa na mtoto mwenzake aliyefahamika kwa jina la SOMEI S/O REMENDA mwenye umri wa miaka mine (4) mkazi wa Kijiji cha Mpendo.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha Kifo hicho ni kwamba marehemu na mtuhumiwa walikuwa wanacheza nje nyumbani kwao kwa akina SOKOINE S/O RENENDA ambapo mtuhumiwa alirusha kisu kwa lengo la kumuua ndege aliyekuwa juu ya mti  uliokuwa karibu na nyumba yao, ndipo kisu huchi kiligonga kwenye mti huo na wakati kinadondoka kilimjeruhi marehemu kwa kumchoma shingoni  na kusababisha kifo chake.

DAVID A. MISIME - ACP
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA DODOMA    

CONTACT:
POLISI MKOA WA DODOMA
DAWATI LA HABARI, ELIMU NA MAHUSIANO,
Phone:  0715 006523, Luppy Kung’alo – Mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)
Phone:  0712  360203, Silyvester Onesmo – Police  Konstebo  (PC)

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...