Skip to main content

SUNZU MAJARIBIONI READING


LONDON, England BEKI wa kati wa kimataifa wa Zambia, Stopilla Sunzu yuko nchini England ambako anafanyiwa majaribio ya kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya Reading.

Sunzu (23) kwa sasa anaichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na anatarajiwa kuichezea Zambia katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zinazotarajiwa kuanza Jumamosi nchini Afrika Kusini.

Beki huyo wa kimataifa wa Zambia, anatarajiwa kutumia wiki moja kufanyiwa majaribio na Reading kabla ya kurejea kwenye kikosi cha Zambia.

Mabingwa watetezi Zambia wamepangwa kuanza michuano hiyo kwa kumenyana na Ethiopia. Taarifa iliyotolewa na tovuti ya Reading juzi ilisema kuwa, Sunzu alipewa ruhusa na Chama cha Soka cha Zambia pamoja na TP Mazembe ya kuondoka kwa muda kwenye kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo ili kufanya mazoezi na Reading na kupimwa uwezo na makocha wa timu hiyo.

"Stoppila atajiunga tena kwenye kikosi cha Zambia baadaye wiki hii, kabla ya kucheza mechi yao ya kwanza ya fainali za Mataifa ya Afrika Jumatatu ijayo," ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, licha ya kuichezea TP Mazembe ya DRC, Sunzu anafahamika vyema na Kocha Mkuu wa Reading, Brian McDermott kutokana na kuwepo kwenye kikosi cha vijana cha timu hiyo alipokuwa mdogo.

Reading ilisema kupitia taarifa hiyo kuwa, Sunzu atafanyiwa majaribio kwa siku nne ili makocha waweze kuona uwezo wake kabla ya kuamua kumsajili kwenye dirisha dogo.

Sunzu ni miongoni mwa wachezaji walioteuliwa kuwania tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika mwaka jana.

Beki huyo ndiye aliyeifungia Zambia penalti ya mwisho katika mechi ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka jana na kuibuka na ushindi wa penalti 8-7 dhidi ya Ivory Coast.

Mbali na Sunzu, tayari Reading imeshamsajili beki Stephen Kelly kutoka Fulham, kiungo Hope Akpan kutoka Crawley na Daniel Carrico kutoka Sporting Lisbon ya Ureno wakati wa dirisha dogo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.