Skip to main content

Serikali ya Somalia Kufanya Mfumo wa mishahara kuwa wa kisasa



Na Adnan Hussein, Mogadishu
Serikali ya Somalia itaanzisha mpango mpya hapo Aprili wa kuwalipa waajiriwa wake kupitia mfumo wa automatiki unaodhibitiwa na Benki Kuu ya Somalia.
Mfumo mpya katika mwezi wa Aprili utaanza kutumiwa kuwalipa waajiriwa wa serikali, ikiwa ni pamoja na wajumbe hawa wa Kikosi cha Polisi ya Somalia, moja kwa moja kupitia Benki Kuu ya Somalia. [Na AFP Photo/AU-UN IST Photo/Stuart Price]
Waziri wa Fedha na Mipango Mohamud Hassan Suleiman aliiambia Sabahi kuwa programu hiyo ni moja miongoni mwa mipango kadhaa yenye lengo la kuufanya mfumo wa fedha nchini kuwa wa kisasa, kutoa uwiano wa bajeti na kuzuia ufisadi wa kitawala na kifedha.
Waajiriwa wa serikali kwa sasa wanalipwa fedha taslimu na wahasibu waliopangiwa katika wizara zao husika baada ya fedha kulipwa na Benki Kuu. Wahasibu ndio wenye dhamana ya kukusanya fedah na kumlipa kila mwajiriwa baada ya kutia saini risiti ya karatasi kama njia ya uthibitisho.
Mchakato huu, ambao unahusisha kutoa na kusafirisha kiwango kikubwa cha fedha na kujaza fomu za karatasi, mara nyingi hupelekea kuchelewa kwa mishahara na kupotea kwa fedha, Suleiman alisema.
Waziri alisema kuwa mfumo huo mpya utazuia kuchelewa huko na kupelekea uwajibikaji mzuri zaidi na uwazi katika udhibiti wa fedha za umma.
Kukiwa na mfumo wa malipo ambao ni automatiki, kila mwajiriwa wa umma atapewa akaunti yake binafsi katika Benki Kuu ambako mishahara yao itakuwa inawekwa kwenye akaunti hizo na kupatikana kwa kutumia kadi ya beki mwanzoni mwa kila mwezi.

Comments