Skip to main content

MONJA 'ANELKA' AMALIZIA SOKA YAKE KISIWANI


Monja 'Anelka'

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
MSHAMBULIAJI wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Monja Privas Liseki amejiunga na Miembeni ya Daraja la Kwanza Zanzibar kwa mkataba wa miaka miwili.
Monja yupo kwenye kikosi cha Miembeni FC kinachoshiriki Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, ambayo leo usiku itamenyana na Azam FC, ikitoka kuifunga 4-1 Mtibwa Sugar katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi B.
“Nipo hapa Miembeni, nadhani nitastaafu nikiwa na timu hii. Huku nimekuja kumalizia soka yangu nafikiri,”alisema Monja alipozungumza na BIN ZUBEIRY leo.   
Monja alizaliwa Agosti 8, mwaka 1975, Kinondoni Muslim mjini Dar es Salaam na alipata elimu yake pekee, ya Msingi katika shule ya Muhimbili, Upanga mjini Dar es Salaam. “Mimi nilikuwa napenda sana soka, nilipomaliza shule ya Msingi tu, nikaachana na shule kabisa nikaanza mitikasi ya soka hadi nikasajiliwa Sigara mwaka 1991 nikiwa bado mdogo sana nina miaka 16 tu,”alisema Monja.
Alicheza Sigara hadi mwaka 1996 iliposhushwa daraja, akahamia Simba SC ambako alidumu hadi mwaka 1998 alipotolewa kwa mkopo Yanga ili aichezee kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Hata hivyo, Monja anasema baada ya kwisha kwa Ligi ya Mabingwa, Yanga walitaka kumsajili moja kwa moja, ila yeye akakataa na kwenda kujiunga na Mtibwa Sugar ambayo aliichezea hadi mwaka jana alipotua Miembeni.
“Nikiwa Mtibwa nilikuwa nikitoka mara moja moja kwenda kubadilisha upepo kwa kucheza Uarabuni na kurudi Mtibwa, kwa mfano mwaka juzi nilitolewa kwa mkopo niende kuisaidia Ocean View ya Zanzibar, niliichezea hadi ikachukua ubingwa wa Zanzibar,”alisema.  
Mbali na kujivunia kuwa mchezaji mkongwe zaidi katika soka ya Tanzania, lakini pia Monja anajivunia kucheza timu ya taifa, kucheza klabu kubwa Simba na Yanga na pia kucheza soka ya kulipwa Uarabuni.
Katika hayo amecheza michuano mikubwa kama Ligi ya Mabingwa Afrika, Kombe la Washindi, Kombe la CAF, Kombe la Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia katika hatua za awali za kuwania tiketi ya kushiriki fainali za michuano hiyo.
“Mimi ndiye mchezaji wa kwanza wa Tanzania kufunga bao katika Ligi ya Mabingwa Afrika, kama utakumbuka Yanga ndio klabu ya kwanza ya Tanzania kucheza michuano hii. Sasa mimi nikiwa na Yanga mwaka 1998, wakati huo naitwa Andy Cole kwa jina la utani, niliifungia Yanga bao katika mechi na Manning Rangers ya Afriika Kusini huu Uwanja ambao siku hizi mnauita Uhuru, wakati huo unaitwa Taifa. Hiyo mechi tulitoka 1-1. Nikarudia kufunga tena kwenye mechi na hao jamaa jamaa kwao, siku wakitufunga 4-1,”alisema.
Monja alisema kwa sasa anataka aitwe Nicolas Anelka wa Tanzania kwa sababu huyo ndiye mchezaji mkongwe ambaye anaendelea kucheza soka ya ushindani.
WASIFU WAKE:
JINA: Monja Privas Liseki
KUZALIWA: Agosti 8, 1975
ALIKOZALIWA: Kinondoni
KLABU YA SASA: Miembeni FC
KUJIUNGA: 2012
KLABU ZA AWALI:
Mwaka          Klabu
1991- 1995   Sigara FC
1996- 1998   Simba SC
1998- 1999   Yanga SC
1999-2012    Mtibwa Sugar

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...