Skip to main content

MONJA 'ANELKA' AMALIZIA SOKA YAKE KISIWANI


Monja 'Anelka'

Na Mahmoud Zubeiry, Zanzibar
MSHAMBULIAJI wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Monja Privas Liseki amejiunga na Miembeni ya Daraja la Kwanza Zanzibar kwa mkataba wa miaka miwili.
Monja yupo kwenye kikosi cha Miembeni FC kinachoshiriki Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, ambayo leo usiku itamenyana na Azam FC, ikitoka kuifunga 4-1 Mtibwa Sugar katika mchezo wake wa kwanza wa Kundi B.
“Nipo hapa Miembeni, nadhani nitastaafu nikiwa na timu hii. Huku nimekuja kumalizia soka yangu nafikiri,”alisema Monja alipozungumza na BIN ZUBEIRY leo.   
Monja alizaliwa Agosti 8, mwaka 1975, Kinondoni Muslim mjini Dar es Salaam na alipata elimu yake pekee, ya Msingi katika shule ya Muhimbili, Upanga mjini Dar es Salaam. “Mimi nilikuwa napenda sana soka, nilipomaliza shule ya Msingi tu, nikaachana na shule kabisa nikaanza mitikasi ya soka hadi nikasajiliwa Sigara mwaka 1991 nikiwa bado mdogo sana nina miaka 16 tu,”alisema Monja.
Alicheza Sigara hadi mwaka 1996 iliposhushwa daraja, akahamia Simba SC ambako alidumu hadi mwaka 1998 alipotolewa kwa mkopo Yanga ili aichezee kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Hata hivyo, Monja anasema baada ya kwisha kwa Ligi ya Mabingwa, Yanga walitaka kumsajili moja kwa moja, ila yeye akakataa na kwenda kujiunga na Mtibwa Sugar ambayo aliichezea hadi mwaka jana alipotua Miembeni.
“Nikiwa Mtibwa nilikuwa nikitoka mara moja moja kwenda kubadilisha upepo kwa kucheza Uarabuni na kurudi Mtibwa, kwa mfano mwaka juzi nilitolewa kwa mkopo niende kuisaidia Ocean View ya Zanzibar, niliichezea hadi ikachukua ubingwa wa Zanzibar,”alisema.  
Mbali na kujivunia kuwa mchezaji mkongwe zaidi katika soka ya Tanzania, lakini pia Monja anajivunia kucheza timu ya taifa, kucheza klabu kubwa Simba na Yanga na pia kucheza soka ya kulipwa Uarabuni.
Katika hayo amecheza michuano mikubwa kama Ligi ya Mabingwa Afrika, Kombe la Washindi, Kombe la CAF, Kombe la Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia katika hatua za awali za kuwania tiketi ya kushiriki fainali za michuano hiyo.
“Mimi ndiye mchezaji wa kwanza wa Tanzania kufunga bao katika Ligi ya Mabingwa Afrika, kama utakumbuka Yanga ndio klabu ya kwanza ya Tanzania kucheza michuano hii. Sasa mimi nikiwa na Yanga mwaka 1998, wakati huo naitwa Andy Cole kwa jina la utani, niliifungia Yanga bao katika mechi na Manning Rangers ya Afriika Kusini huu Uwanja ambao siku hizi mnauita Uhuru, wakati huo unaitwa Taifa. Hiyo mechi tulitoka 1-1. Nikarudia kufunga tena kwenye mechi na hao jamaa jamaa kwao, siku wakitufunga 4-1,”alisema.
Monja alisema kwa sasa anataka aitwe Nicolas Anelka wa Tanzania kwa sababu huyo ndiye mchezaji mkongwe ambaye anaendelea kucheza soka ya ushindani.
WASIFU WAKE:
JINA: Monja Privas Liseki
KUZALIWA: Agosti 8, 1975
ALIKOZALIWA: Kinondoni
KLABU YA SASA: Miembeni FC
KUJIUNGA: 2012
KLABU ZA AWALI:
Mwaka          Klabu
1991- 1995   Sigara FC
1996- 1998   Simba SC
1998- 1999   Yanga SC
1999-2012    Mtibwa Sugar

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...