Skip to main content

SAMATTA: NITAIFANYIA MAKUBWA TAIFA STARS


MSHAMBULIAJI Mbwana Samatta anayecheza soka ya kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, amesema amepanga kuifanyia mambo makubwa timu ya taifa, Taifa Stars.

Samatta alisema hayo mjini Dar es Salaam juzi, muda mfupi kabla ya Taifa Stars kwenda Ethiopia kwa ziara ya mechi moja ya kirafiki.

Mshambuliaji huyo, ambaye amekuwa akishutumiwa kwa kucheza chini ya kiwango anapoichezea Taifa Stars, alisema si kweli kwamba hana uzalendo kwa timu yake ya taifa.

"Habari hizi zinanikera sana. Hivi mimi ningejulikana vipi na TP Mazembe kama sio Taifa Stars na Simba? Wangeniona wapi? Mimi nitaendelea kuichezea timu yangu ya Taifa kwa mapenzi yote ili niwazibe midomo wabaya wangu,"alisema mchezaji huyo.

Alisema yupo tayari kuichezea Taifa Stars wakati wowote atakapoitwa na Kocha Kim Poulsen kwa sababu moja ya sifa za mwanasoka wa kimataifa ni kufanya vizuri katika timu yake ya taifa.

Samatta alisema moja ya ndoto zake ni kuifungia Taifa Stars mabao mengi katika michuano ya kimataifa na pia kuiwezesha kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014 zitakazofanyika nchini Brazil.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu za African Lyon na Simba alisema, kwa sasa yupo fiti baada ya kupona na kusisitiza kuwa, ataanza kuonyesha makali yake leo katika pambano kati ya Taifa Stars na Ethiopia litakalofanyika mjini Addis Ababa.

"Kwa kweli najisikia faraja kubwa leo hii kusafiri na wachezaji wenzangu wa nchi yangu,nina imani mwaka huu nitafanya mengi makubwa, ikiwa ni pamoja na kufunga mabao kwa kushirikiana na wenzangu. Na hilo nitalifanya hata kwa klabu yangu ya TP Mazembe,"alisema nyota huyo.

Samatta alikiri kuwa, kwa sasa anakabiliwa na kibarua kizito cha kupata namba ya kudumu kwenye klabu yake ya TP Mazembe kutokana na kuwepo kwa wachezaji wengi nyota kutoka katika nchi mbalimbali.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.