Skip to main content

KIMBEMBE JANA SIMBA, AZAM, COASTAL UNION ZAUA



MABINGWA watetezi Simba leo wameuanza vyema mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuichapa African Lyon mabao 3-1 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika pambano hilo, Simba ingeweza kutoka uwanjani na ushindi mkubwa wa mabao iwapo mshambuliaji wake, Mrisho Ngasa angekuwa makini kila alipolifikia lango la African Lyon.

Ngasa pia alipoteza penalti katika kipindi cha pili baada ya shuti lake kumlenga kipa Abdul Seif. Hadi mapumziko, Simba ilikuwa mbele kwa mabao 3-0.

Mabao ya Simba katika kipindi hicho cha kwanza yalifungwa na Mrisho Ngasa, aliyefunga mawili na Ramadhani Chombo 'Redondo'.

Redondo, aliyerejea Simba akitokea Azam, alifunga bao la kwanza dakika ya tatu baada ya kuunganisha wavuni mpira wa krosi uliopigwa na Ngasa kutoka pembeni ya uwanja na kuamsha shangwe kutoka kwa mashabiki wa Simba.

Bao la pili lilifungwa na Ngasa baada ya gonga safi kati yake na Mwinyi Kazimoto kabla ya kufumua shuti lililompita kipa Seif wa African Lyon.

Lyon ingeweza kupunguza tofauti ya mabao dakika ya 31 wakati ilipopata adhabu ya penalti baada ya beki Paul Ngelema wa Simba kumwangusha Fred Lewis ndani ya eneo la hatari. Hata hivyo, shuti la kwanza la Shamte Ally liliokolewa na kipa Juma Kaseja wa Simba, lakini mwamuzi Israel Mujuni aliamuru penalti hiyo irudiwe. Na iliporudiwa, shuti la Shamte lilitoka pembeni ya lango.

Ngasa aliifungia Simba bao la tatu baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Chanongo, aliyepandishwa kutoka kikosi cha pili, ambaye alionyesha kila dalili za kuweza kuziba vyema pengo la Emmanuel Okwi, aliyeuzwa kwa klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia.

Lyon ilibadili sura ya mchezo katika kipindi cha pili, ambapo ilicheza gonga safi na kutoa usumbufu mkubwa kwa mabeki na viungo wa Simba, ambao walikuwa wakiutafuta mpira kwa toshi.

Mashambulizi hayo ya Lyon yalizaa matunda dakika ya 59 baada ya kupata bao la kujifariki kupitia kwa Bright Ike baada ya kupokea pasi kutoka kwa Fred.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa leo, Mtibwa Sugar ilichapwa bao 1-0 na ndugu zao wa Polisi kwenye uwanja wa Manungu. Bao pekee na la ushindi la Polisi lilifungwa na Muzamil Saidi.

Katika mechi zingine, Coastal Union iliwacharaza ndugu zao wa Mgambo JKT mabao 3-1, Ruvu Shooting waliwalaza ndugu zao wa JKT Ruvu bao 1-0, Azam iliinyuka Kagera Sugar mabao 3-1 wakati JKT Oljoro iliibamiza Toto Africans mabao 3-1.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo wakati Yanga itakapomenyana na Prisons kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...