Skip to main content

KIMBEMBE JANA SIMBA, AZAM, COASTAL UNION ZAUA



MABINGWA watetezi Simba leo wameuanza vyema mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuichapa African Lyon mabao 3-1 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika pambano hilo, Simba ingeweza kutoka uwanjani na ushindi mkubwa wa mabao iwapo mshambuliaji wake, Mrisho Ngasa angekuwa makini kila alipolifikia lango la African Lyon.

Ngasa pia alipoteza penalti katika kipindi cha pili baada ya shuti lake kumlenga kipa Abdul Seif. Hadi mapumziko, Simba ilikuwa mbele kwa mabao 3-0.

Mabao ya Simba katika kipindi hicho cha kwanza yalifungwa na Mrisho Ngasa, aliyefunga mawili na Ramadhani Chombo 'Redondo'.

Redondo, aliyerejea Simba akitokea Azam, alifunga bao la kwanza dakika ya tatu baada ya kuunganisha wavuni mpira wa krosi uliopigwa na Ngasa kutoka pembeni ya uwanja na kuamsha shangwe kutoka kwa mashabiki wa Simba.

Bao la pili lilifungwa na Ngasa baada ya gonga safi kati yake na Mwinyi Kazimoto kabla ya kufumua shuti lililompita kipa Seif wa African Lyon.

Lyon ingeweza kupunguza tofauti ya mabao dakika ya 31 wakati ilipopata adhabu ya penalti baada ya beki Paul Ngelema wa Simba kumwangusha Fred Lewis ndani ya eneo la hatari. Hata hivyo, shuti la kwanza la Shamte Ally liliokolewa na kipa Juma Kaseja wa Simba, lakini mwamuzi Israel Mujuni aliamuru penalti hiyo irudiwe. Na iliporudiwa, shuti la Shamte lilitoka pembeni ya lango.

Ngasa aliifungia Simba bao la tatu baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Haruna Chanongo, aliyepandishwa kutoka kikosi cha pili, ambaye alionyesha kila dalili za kuweza kuziba vyema pengo la Emmanuel Okwi, aliyeuzwa kwa klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia.

Lyon ilibadili sura ya mchezo katika kipindi cha pili, ambapo ilicheza gonga safi na kutoa usumbufu mkubwa kwa mabeki na viungo wa Simba, ambao walikuwa wakiutafuta mpira kwa toshi.

Mashambulizi hayo ya Lyon yalizaa matunda dakika ya 59 baada ya kupata bao la kujifariki kupitia kwa Bright Ike baada ya kupokea pasi kutoka kwa Fred.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa leo, Mtibwa Sugar ilichapwa bao 1-0 na ndugu zao wa Polisi kwenye uwanja wa Manungu. Bao pekee na la ushindi la Polisi lilifungwa na Muzamil Saidi.

Katika mechi zingine, Coastal Union iliwacharaza ndugu zao wa Mgambo JKT mabao 3-1, Ruvu Shooting waliwalaza ndugu zao wa JKT Ruvu bao 1-0, Azam iliinyuka Kagera Sugar mabao 3-1 wakati JKT Oljoro iliibamiza Toto Africans mabao 3-1.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo wakati Yanga itakapomenyana na Prisons kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.