Skip to main content

Kuongezeka kwa uingiaji kwenye intaneti nchini Kenya kunatoa kazi, kuimarisha elimu


Na Rajab Ramah, Nairobi
Unganishwaji wa intaneti ulioboreshwa nchini Kenya unaongeza ukuaji wa uchumi, kupatikana kwa kazi na kuongeza upataji wa elimu, maofisa wahusika wa tasnia hiyo wamesema.
Mem Maina akionyesha matumizi ya simu mpya wakati wa maonyesho ya teknolojia ya Afrika ya DEMO kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta jijini Nairobi tarehe 25 Oktoba. Utafiti wa hivi karibuni ulionyesha kwamba simu za mkononi zinaweza kusaidia kuondoa pengo linalotenganisha la dijitali na kutoa ufikivu wa intaneti kwa Wakenya wengi zaidi. [Simon Maina/AFP]
Huduma za mtandao zinazopatikana kwenye kompyuta na simu za mkononi zimepunguza gharama za muamala katika sekta mbalimbali na kusaidia kufanya maisha ya raia kuwa rahisi, kwa mujibu wa mwenyekiti wa Chama cha Walaji cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Alex Gakuru.
"Wananchi wanaweza kupakua na kujaza nyaraka muhimu kama vile ripoti ya polisi kwa kubofya kipanya," aliiambia Sabahi. "Wanaweza kulipa bili kwa kutumia simu zao za mkononi na wanaweza kuomba kazi kupitia mtandao. Hii inamaanisha kwamba inapunguza kusafiri na matumizi."
Kwa mujibu wa ripoti ya Tume ya Mawasiliano ya Kenya ya 2011-2012 iliyotolewa Oktoba, matumizi ya intaneti kupitia kompyuta za kawaida yamekua kwa watumiaji milioni kwa silimia 19.2 hadi 7.7, wakati matumizi ya inteneti kwa njia ya simu za mkononi yamekua kwa watumiaji milioni kwa asilimia 1.7 hadi 29.7.
Ingawaje gharama kubwa za ufikiaji zimeendelea kuwepo, Gakuru alisema, kuogezeka kwa uingiaji kwenye intaneti umeboresha biashara, mawasiliano na mandhari ya elimu nchini Kenya.
Uunganishwaji mzuri umetafsiriwa kwenye gharama ndogo za matangazo kwa ajili ya biashara, kwani sasa wanaweza kufikia watu wengi kupitia mtandao. Kuwasiliana na wateja kupitia mtandao, ambao wanatoa mwitikio kwa wamiliki wa biashara, husaidia malengo ya kampuni na kukidhi vizuri matakwa ya wateja, Gakuru alisema.

Comments