Skip to main content

Al-Shabaab waondoka Bardhere wakati vikosi vya washirika vyakaribia


Na Adnan Hussein, Mogadishu
Wanamgambo wa al-Shabaab wanaondoka mfululizo huko Bardhere katika mkoa wa Gedo wakati mamia ya askari wa Somalia, wakisaidiwa na majshi ya Ethiopia, wakisonga mbele kuelekea mjini kudai udhibiti na kurejesha sheria na utaratibu.
Jeshi la Taifa la Somalia, kama linavyoonekana hapa likiwa Elasha Biyaha mwezi Novemba 2012, linatayarisha shambulio kubwa dhidi ya wanamgambo wa al-Shabaab katika mkoa wa Gedo. [Na Stuart Price/AU-UN IST/AFP]
Mkazi wa eneo hilo Farhan Mohamed Jama alisema aliiona misafara na magari ya kijeshi ya al-Shabaab yakiondoka kutoka Bardhere kwa muda wa usiku kadhaa, yakienda magharibi kuelekea Burdubo na Dinsor katika mkoa wa Bay.
"Kuna mazingira ya kutokuwepo na sheria mjini na al-Shabaab wametangaza hali ya tahadhari wakijitayarisha na mashambulizi dhidi ya kambi na ngome zake," Jama aliiambia Sabahi. "Katika baadhi ya mitaa na katikati, kuna mamia ya wanamgambo wa waasi ambao wameanza kupiga risasi nzito hewani usiku wa manane wiki hii iliyopita katika jaribio la kuwashitua wakazi na kuonyesha nguvu zao katika eneo hili."
Siku ya Alhamisi jioni (tarehe 3 Januari), al-Shabaab waliwakamata viongozi 13 wa dini na kuwashutumu kuwa wanakula njama za kuvikaribisha vikosi vinavyokaribia, Jama alisema.
Hawa Ahmed Kheyre, muuzaji wa maandazi mwenye umri wa miaka 30 katika soko la Bardhere, alisema kuwa al-Shabaab wamewaondosha baadhi ya wapiganaji wao kutoka mjini ili kujitayarisha kwa vita vya msituni na ulipuaji mabomu.
"Tunaishi katika nyakati za zahama kwa matokeo ya vitisho kutoka kwa watu wenye siasa kali ambao wamezagaa vijijini kote na milimani ya mkoa wa Gedo," alisema. "Tunasumbuliwa na mivutano, mauaji na mashitaka kutoka mikononi mwa wafuasi wa kikundi hiki ambao wamejipenyeza miongoni mwa watu wa eneo hili."
Diyad Abdi Kalil, afisa wa jeshi la Somalia huko Gedo, alisema kwa kweli vikosi vya Somalia vinapanga kuishambulia Bardhere na Burdubo, ambazo bado ziko katika udhibiti wa al-Shabaab, lakini hakusema lini.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...