Skip to main content

SALMA kikwete, ATEMBELEA AMREF NA POUR FOUNDATION

 

IMG_4658
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mwanzilishi na Rais wa Foundation Pour  l¨ Enfrance Mama Anne Aymone Giscard d’ Estaing na Mke wa Rais Mstaafu wa Ufaransa Bwana Valery Giscard d’ Estaing, wakati Mama Salma alipotembelea makao makuu ya taasisi hiyo jijini Paris Ufaransa tarehe 22:1:2013: Mama Salma yupo nchini Ufaransa akifuatana na Rais Kikwete kwenye ziara ya kiserikali nchini humo:
IMG_4690
Rais wa AMREF France Bwana Nicolas Merindol akimkaribisha Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete kwenye makao makuu ya shirika hilo jijini Paris nchini Ufaransa tarehe 22, 1, 2013 na baadaye viongozi hao walifanya mazungumzo juu ya ushirikiano zaidi wa taasisi hizo katika masuala ya afya na elimu:
 Na: Anna Nkinda – Paris
Ushirikiano wa pamoja baina ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na wadau wa maendeleo nchini umeiwezesha taasisi hiyo kuwasaidia na kuwainua wanawake kiuchumi ambao wameweza  kujishughulisha na kazi za ujasiriamali na
hivyo kujikwamua na hali ngumu ya maisha.
Pia Taasisi hiyo imeweza kutoa ufadhili wa masomo kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi jambo ambalo limewafanya watoto hao wapate elimu  sawa watoto wengine wenye wazazi  na kuimarisha afya za mama wajawazito na watoto
Hayo yamesemwa leo na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati alipotembelea Taasisi inayoshughulika na masuala ya watoto (France Parrainages)  kiliyopo mjini Paris ambacho kinafanya kazi na Kituo cha Ufaransa cha  kuwaangalia watoto kwa kushirikiana na Taasisi ya Partage Tanzania inayohudumia watoto yatima katika mkoa wa Kagera.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa  WAMA alisema kuwa Taasisi hiyo imeweza  kujenga shule ya Sekondari ya WAMA – NAKAYAMA iliyopo Rufiji Mkoani Pwani ambayo ina wanafunzi  247 ambao ni watoto yatima  na matarajio ya baadaye ni kuwa na wanafunzi 780.
“Katika mkoa wa Lindi tumejenga mabweni ya wanafunzi wa sekondari wa kike,  tunagharamia  masomo ya Sekondari kwa  wanafunzi 250 na wanafunzi 16 wa elimu ya juu kutoka mikoa yote nchini”, alisema Mama Kikwete.
Aliendelea kusema kuwa Taasisi hiyo  imeweza kuwasaidia wanawake kiuchumi  na kuwafanya waweze kuongeza kipato cha familia zao, kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vikundi vidogo vidogo ambavyo vinaweza kutengeneza bidhaa za kusindika za vyakula na kuziuza.
Kwa upande wake Charline Flauge’re ambaye ni msimamizi wa Programu za Kituo cha Ufaransa cha  kuwaangalia watoto upande wa Afrika alisema kuwa Taasisi ya Partage Tanzania ambayo inahudumiwa na kituo hicho inafanya kazi nchini katika mkoa wa Kagera ambayo ni moja ya nchi tatu muhimu  kutokana na idadi ya watoto wanaowahudumia kufikia 10000.
Alisema kuwa watoto hao yatima wanaishi vijijini na familia zao zinajishughulisha na kazi za ukulima mdogo wa kahawa na migomba wao wanatoa ufadhili ambao unawasaidia waweze kuishi na familia zao na kupata upendo wa ndugu bila ya kuishi katika vituo vya kulelea watoto yatima
Flauge’re alisema, “Tunashukuru kwa kuwahudumia watoto hawa ambao wameweza kukua wenyewe ndani ya familia zao za mama,  kaka au dada, ufadhili huu umeweza kumsaidia mzazi aliyebaki hai, bibi na babu zao kuwaangalia na hivyo  kukua katika afya njema  na mazingira yao waliyozaliwa
Alimalizia kwa kusema kuwa ufadhili huo hautoi fedha na vitu  peke yake bali pia unajenga mahusiano baina ya watoto na wafadhili wao ambao wanaishi nchini Ufaransa kwani watoto  wanawaandikia wafadhili barua na kuwasiliana nao na wakati mwingine wanakuja kuwasalimiana nchini Tanzania na hivyo kujifunza mila na desturi za pande zote mbili.
Taasisi  ya WAMA ilianzishwa  mwaka 2006 ikiwa na malengo ya kutoa ufadhili wa masomo kwa watoto wa kike ambao hawakupata nafasi ya kusoma, kuimarisha afya ya mama wajawazito na watoto, kuwainua wanawake kiuchumi na kuwasaidia watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi.Source Mjengwa.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...