Skip to main content

Kigogo cha soka nchini Yanga yatinga Nusufainali Kombe la Mapinduzi


Hiyo ni baada ya Yanga kutoka sare ya 1-1 na Singida United katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi usiku huu Uwanja wa Amaan.
Nusu Fainali ya kwanza itakuwa kati ya Yanga na URA Saa 10:30 jioni na saa 2:15 usiku Singida United na Azam zitachukua nafasi kwa mujibu wa ratiba kama hakutakuwa na mabadiliko.
Upo uwezekano mkubwa, mchezo kati ya Azam FC na Singida ukatangulia jioni na Yanga na URA wakahamishiwa usiku.
Katika mchezo usiku wa leo wa Kundi B, baada ya dakika 45 ngumu za kipindi cha kwanza, Singida United walitangulia kwa bao la mshambuliaji Daniel Lyanga dakika ya 72 aliyefunga kwa kichwa akimalizia mpira wa adhabu wa kiungo Kiggi Makassy kutoka nje kidogo ya boksi upande wa kushoto.
Yanga wakasawazisha katika mazingira yale yale, mpira wa adhabu wa kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajib kutoka upande wa kulia ulipounganishwa kwa kichwa na kiungo wa ulinzi, Said Juma ‘Makapu’ dakika ya kwanza ya muda wa nyongeza kati ya tatu baada ya kutimia dakika 90 za kawaida za mchezo.
Kwa ujumla ulikuwa mchezo mzuri ambao timu zote zilicheza kwa ustadi wa hali ya juu na kuwapa burudani watazamaji.
Kocha Mholanzi Hans van der Plujim anafikisha mechi tatu bila kuifunga timu yake ya zamani, Yanga tangu ahame baada ya sare mbili za 1-1, ya mjini Singida mwaka jana na leo Zanzibar kufuatia kufungwa 3-2 Dar es Salaam kwenye mchezo wa kirafiki.
Sifa ziwaendee makocha wasaidizi wa Yanga, Mzambia Noel Mwandila na mzalendo, Nsajigwa Shadrack Mwandemele kwa kuiongoza timu katika mechi nne bila kupoteza ikishinda nne na sare moja katika kipindi ambacho bosi wao, George Lwandamina yupo kwao, Zambia kwa matatizo ya kifamilia.     
Mchezo wa kwanza wa kukamilisha mechi za Kundi A, Simba walichapwa 1-0 na URA hapa hapa Amaan na kesho watapanda boti kurejea Dar es Salaam kuendelea na maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kikosi cha Singida United kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Michael Rusheshangoga, Shafiq Batambuze, Juma Kennedy, Malik Antiri, Yussuf Kagoma, Deus Kaseke, Mudathir Yahya/Kenny Ally dk75, Danny Lyanga, Kambale Salita Gentil/Lubinda Mundia dk75 na Kiggi Makassy. 
Yanga SC; Youthe Rostand, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Andrew Vincent ‘Dante’, Kevin Yondan, Maka Edward/Said Juma ‘Makapu’ dk72, Pius Buswita/Matheo Anthony dk67, Raphael Daudi, Yohanna Nkomola/Juma Mahadhi dk67, Ibrahim Ajib na Emmanuel Martin/Geoffrey Mwashiuya dk76. 

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AFANYA MAHOJIANO NA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Moh amed Shein,alipokuwa akifanya mahojiano na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kupitia ZBC TV na kutoa wito kwa Watanzania hasa wa Zanzibar kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishaji vitambulisho hivyo,ambapo zoezi hilo  linatarajia kuwanza Oktoba 15 mwaka. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu mjini Zanzibar leo,(kulia) Mtangazji wa ZBC TV Nasra Nassor. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...