Skip to main content

Kigogo cha soka nchini Yanga yatinga Nusufainali Kombe la Mapinduzi


Hiyo ni baada ya Yanga kutoka sare ya 1-1 na Singida United katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi usiku huu Uwanja wa Amaan.
Nusu Fainali ya kwanza itakuwa kati ya Yanga na URA Saa 10:30 jioni na saa 2:15 usiku Singida United na Azam zitachukua nafasi kwa mujibu wa ratiba kama hakutakuwa na mabadiliko.
Upo uwezekano mkubwa, mchezo kati ya Azam FC na Singida ukatangulia jioni na Yanga na URA wakahamishiwa usiku.
Katika mchezo usiku wa leo wa Kundi B, baada ya dakika 45 ngumu za kipindi cha kwanza, Singida United walitangulia kwa bao la mshambuliaji Daniel Lyanga dakika ya 72 aliyefunga kwa kichwa akimalizia mpira wa adhabu wa kiungo Kiggi Makassy kutoka nje kidogo ya boksi upande wa kushoto.
Yanga wakasawazisha katika mazingira yale yale, mpira wa adhabu wa kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajib kutoka upande wa kulia ulipounganishwa kwa kichwa na kiungo wa ulinzi, Said Juma ‘Makapu’ dakika ya kwanza ya muda wa nyongeza kati ya tatu baada ya kutimia dakika 90 za kawaida za mchezo.
Kwa ujumla ulikuwa mchezo mzuri ambao timu zote zilicheza kwa ustadi wa hali ya juu na kuwapa burudani watazamaji.
Kocha Mholanzi Hans van der Plujim anafikisha mechi tatu bila kuifunga timu yake ya zamani, Yanga tangu ahame baada ya sare mbili za 1-1, ya mjini Singida mwaka jana na leo Zanzibar kufuatia kufungwa 3-2 Dar es Salaam kwenye mchezo wa kirafiki.
Sifa ziwaendee makocha wasaidizi wa Yanga, Mzambia Noel Mwandila na mzalendo, Nsajigwa Shadrack Mwandemele kwa kuiongoza timu katika mechi nne bila kupoteza ikishinda nne na sare moja katika kipindi ambacho bosi wao, George Lwandamina yupo kwao, Zambia kwa matatizo ya kifamilia.     
Mchezo wa kwanza wa kukamilisha mechi za Kundi A, Simba walichapwa 1-0 na URA hapa hapa Amaan na kesho watapanda boti kurejea Dar es Salaam kuendelea na maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kikosi cha Singida United kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Michael Rusheshangoga, Shafiq Batambuze, Juma Kennedy, Malik Antiri, Yussuf Kagoma, Deus Kaseke, Mudathir Yahya/Kenny Ally dk75, Danny Lyanga, Kambale Salita Gentil/Lubinda Mundia dk75 na Kiggi Makassy. 
Yanga SC; Youthe Rostand, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Andrew Vincent ‘Dante’, Kevin Yondan, Maka Edward/Said Juma ‘Makapu’ dk72, Pius Buswita/Matheo Anthony dk67, Raphael Daudi, Yohanna Nkomola/Juma Mahadhi dk67, Ibrahim Ajib na Emmanuel Martin/Geoffrey Mwashiuya dk76. 

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...