Skip to main content

Kigogo cha soka nchini Yanga yatinga Nusufainali Kombe la Mapinduzi


Hiyo ni baada ya Yanga kutoka sare ya 1-1 na Singida United katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi usiku huu Uwanja wa Amaan.
Nusu Fainali ya kwanza itakuwa kati ya Yanga na URA Saa 10:30 jioni na saa 2:15 usiku Singida United na Azam zitachukua nafasi kwa mujibu wa ratiba kama hakutakuwa na mabadiliko.
Upo uwezekano mkubwa, mchezo kati ya Azam FC na Singida ukatangulia jioni na Yanga na URA wakahamishiwa usiku.
Katika mchezo usiku wa leo wa Kundi B, baada ya dakika 45 ngumu za kipindi cha kwanza, Singida United walitangulia kwa bao la mshambuliaji Daniel Lyanga dakika ya 72 aliyefunga kwa kichwa akimalizia mpira wa adhabu wa kiungo Kiggi Makassy kutoka nje kidogo ya boksi upande wa kushoto.
Yanga wakasawazisha katika mazingira yale yale, mpira wa adhabu wa kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajib kutoka upande wa kulia ulipounganishwa kwa kichwa na kiungo wa ulinzi, Said Juma ‘Makapu’ dakika ya kwanza ya muda wa nyongeza kati ya tatu baada ya kutimia dakika 90 za kawaida za mchezo.
Kwa ujumla ulikuwa mchezo mzuri ambao timu zote zilicheza kwa ustadi wa hali ya juu na kuwapa burudani watazamaji.
Kocha Mholanzi Hans van der Plujim anafikisha mechi tatu bila kuifunga timu yake ya zamani, Yanga tangu ahame baada ya sare mbili za 1-1, ya mjini Singida mwaka jana na leo Zanzibar kufuatia kufungwa 3-2 Dar es Salaam kwenye mchezo wa kirafiki.
Sifa ziwaendee makocha wasaidizi wa Yanga, Mzambia Noel Mwandila na mzalendo, Nsajigwa Shadrack Mwandemele kwa kuiongoza timu katika mechi nne bila kupoteza ikishinda nne na sare moja katika kipindi ambacho bosi wao, George Lwandamina yupo kwao, Zambia kwa matatizo ya kifamilia.     
Mchezo wa kwanza wa kukamilisha mechi za Kundi A, Simba walichapwa 1-0 na URA hapa hapa Amaan na kesho watapanda boti kurejea Dar es Salaam kuendelea na maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kikosi cha Singida United kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Michael Rusheshangoga, Shafiq Batambuze, Juma Kennedy, Malik Antiri, Yussuf Kagoma, Deus Kaseke, Mudathir Yahya/Kenny Ally dk75, Danny Lyanga, Kambale Salita Gentil/Lubinda Mundia dk75 na Kiggi Makassy. 
Yanga SC; Youthe Rostand, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Andrew Vincent ‘Dante’, Kevin Yondan, Maka Edward/Said Juma ‘Makapu’ dk72, Pius Buswita/Matheo Anthony dk67, Raphael Daudi, Yohanna Nkomola/Juma Mahadhi dk67, Ibrahim Ajib na Emmanuel Martin/Geoffrey Mwashiuya dk76. 

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.