Skip to main content

DR. Kigwangala asikiliza changamoto mbalimbali zinazo wakabili wachongaji wa vinyago

Image result for DR.HAMISI KIGWANGALLA
Waziri wa maliasili na utalii hapa nchini DR.Hamis Kigwangala(picha na mtandao)

  Dar es salaam
Waziri wa maliasili na utalii hapa nchini DR.Hamis Kigwangala leo amezungumza na  wafanyabiashara na wachongaji wa vinyago katika eneo la Mwenge jijini Dar es salaam, katika ziara yake hii leo,  ya kutembelea maeneo mbalimbali yenye mchango mkubwa kwenye utalii na kuliingizia taifa kipato.

Baada ya kuwasili katika  eneo hilo na kutembelea baadhi ya mabanda mbalimbali ya sanaa hiyo,  Dk.Kigwangala amesikiliza changamoto mbalimbali zinazo wakabili wachongaji wa vinyago.

Dk.Kigwangala amewataka wafanyabiashara hao kumaliza changamoto zao, ili serikali iweze kurahisisha mipango juu ya wachongaji na wafanyabiasahara wa eneo hilo.

Dk.Kigwangala aliendelea na ziara yake ambapo pia hii leo amewatembelea wasanii wa sanaa ya uchoraji manispaa ya kinondoni katika eneo la Morogoro store maarufu tingatinga,  na kusema kuwa seriakali kupitia utalii inataka kila mwananchi kuweza kufaidika na sekta utalii hapa nchini.

Kwa upande wao viongozi wa Morogoro store maarufu tingatinga wamepongeza hatua ya waziri wa maliasili na utalii kuithamini kazi yao kwa kuwatembelea na kuwajuza mipango ya serikali.

Awali Waziri Dk.Kigwangala ametembelea kituo utalii cha kumbukumbu ya hayati mwalimu nyerere kilichopo magomeni kota jijini hapa nakujionea changamoto mbalimbali zinazokikabili kituo hicho, ambacho kilikuwa nyumba ya mwalimu nyerere miaka ya nyuma na kuahidi kuzitatua changamoto hizo.

Kazi ya sanaa ni kama kazi nyingine hapa nchini watanzania tuwajali na kuwathamini wasanii wa uchongaji na uchoraji ili waweze kutimiza malengo yao, na kuondokana na dhana ya wataii ni watu kutoka nje ya nchi.

Comments