Skip to main content

Yanga yaiombea mema Simba


Imani Makongoro

KATIKA hali ambayo ni nadra kusikika, mabingwa wa soka nchini Yanga wamesema wanawaombea wapinzani wao Simba washinde katika mechi ya marudiano dhidi ya timu ya Kiyovu ya Rwanda, kwa vile wanaamini ushindi kwao ni sifa kwa Watanzania wote na siyo Simba peke yao.
Simba inatarajia kurudiana na Kiyovu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kati ya Machi 2 au 3, huku Wekundu hao wa Msimbazi wakijivunia sare ya ugenini ya bao 1-1 Jumamosi iliyopita katika michuano ya Kombe la Shirikisho.
Yanga wanaamini kuwa Simba wana nafasi ya kufanya vizuri kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika jijini Dar es Salaam, wakati wao wakienda Misri kwa kurudiana na Zamalek baada ya sare ya 1-1 wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.
Wakati Yanga ikitoa kauli hiyo, Jumamosi iliyopita ilishuhudia mashabiki wa Simba wakiwashangilia wapinzani wao Zamalek kwenye Uwanja wa Taifa jijini.
Akizungumza jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Celestin Mwesigwa alisema klabu yao haioni sababu ya kutoiombea Simba mazuri pale linapokuja suala la kitaifa.
"Maombi yetu ni timu zote za Tanzania zipite, hatuwezi kuiombea Simba itolewe kutokana na upinzani uliopo baina yetu na wao. Wao (Simba) na sisi tuko ndani ya Tanzania. Ni lazima tuombeane ili tuleta sifa Tanzania," alisema.
Akiongelea kitendo cha mashabiki wa timu yake kununua jezi za Kiyovu kama walivyofanya wale wa Simba katika mechi yao dhidi ya Zamalek, Mwesigwa alisema wao kama viongozi wa Yanga hawawezi kuwazuia mashabiki kununua na kuvaa jezi hizo katika mechi ya marudiano ya Simba na Kiyovu.
"Kila  shabiki ana uhuru wa kiushangilia timu anayoipenda hivyo mwenye maamuzi ya kuvaa jezi ya Zambarau na Kijivu katika mechi ya Kiyovu na Simba ni shabiki mwenyewe sisi hatuwezi kumzuia," alisema.
Kauli kama hiyo pia iliwahi kutolewa na Mwenyekiti wa Simba Aden Rage kufuatia mashabiki wa timu yake kununua jezi za Zamalek kwa lengo la kuwaunga mkono kwenye mechi dhidi ya Yanga.
Alikaririwa akisema; "Simba haina uwezo wa kuwazuia mashabiki wake kushangilia timu nyingine wanayoipenda. Kwa maana hiyo, kama wataishangilia Zamalek, hilo siyo agizo letu ila uamuzi wao binafsi."
Kuhusu maandalizi kwa ajili ya mechi ya marudiano, Mwesigwa wanajipanga vizuri ili kuhakikisha wanashinda mechi hiyo ya marudiano ugenini.
"Tulijiandaa katika mechi zote mbili lakini bahati mbaya mechi ya kwanza tukiwa nyumbani timu yetu ilitoka sare ya 1-1. Tunajiandaa kurekebisha makosa yaliyotokea na mwalim ameshaanza kazi hiyo," alisema.Source Mwananchi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.