Skip to main content

Kigogo Wa Bakwata Kufikishwa Mahakamani Leo (Gazeti Mwananchi)



Frederick Katulanda, Mwanza
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) Mkoa wa Mwanza, leo inatarajia kumpandisha kizimbani kigogo wa Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) mkoani Mwanza, kwa kosa la kuhujumu uchumi.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mwanza, Christopher Mariba, zimedai kuwa kufikishwa mahakamani kwa Kigogo huyo, kunatokana kutumia msamaha wa kodi wa Serikali kununua saruji kwa niaba ya wafanyabiashara kwa jina la Bakwata, hivyo kukwepa kodi zaidi ya Sh15 milioni kila mwezi mmoja.

Imeelezwa kufikishwa mahakamani kwa kigogo huyo kunatokana na hujuma hizo kuanza kufichuliwa na Gazeti la Mwananchi Jumapili, baada ya kutolewa mara ya kwanza Januari 25, 2009 Takukuru walifanya uchunguzi wao na kubaini kuwa kulikuwa na ukweli.

“Uchunguzi wetu umekamilika, kama Mungu akijalia kesho (leo) tutamfikisha mahakamani, sasa naomba mfike wenyewe mahakamani maana siwezi kuongea sana juu ya masuala haya,” alisema Mariba.

Pia, katika habari iliyoandikwa na Mwananchi Jumapili zilieleza katibu huyo akiwa na dhamana ya kuongoza Bakwata, alishirikiana na wafanyabiashara wa Mwanza kutumia jina la Bakwata kununua tani za saruji 2,298 kwa Sh31,589,34.

Kipindi cha wiki mbili wanadaiwa walinunua saruji kwa bei ya Sh16,500 kila mfuko, kisha kuiuza kwa bei ya Sh19,000 yenye kodi sawa na Sh43,651,913, hivyo kujinufaisha binafsi na kuikosesha Serikali mapato.

Ilielezwa kuwa kiasi hicho cha fedha kiliwekwa katika akaunti namba 015101004917 iliyopo tawi la NBC Mwanza kabla ya kuingizwa kwenye akaunti hiyo ilikuwa na salio la Sh474,045.45, lakini baada ya kuingia fedha hizo zilitolewa kwa vipindi tofauti zikionyesha kwenda kwa Cement Distributor kulipia ununuzi wa saruji.

Kulingana na kumbukumbu ya nyaraka mbalimbali kutoka ofisi ya Bakwata mkoani Mwanza ambazo gazeti hili imebahatika kuziona, Januari 3, mwaka huu akaunti hiyo ikiwa salio la Sh474,045.45, ilionyesha kupokea Sh8,680,000 na kiasi hicho kutolewa siku hiyo kwenda kwa Cement Distributor.

Kiasi kingine cha Sh11,085,163,00 kiliingia katika akaunti hiyo Januari 9, mwaka huu lakini pia kilitolewa siku hiyo pia kikielekea kununua saruji.

Fedha nyingine Sh11,824,176 ilingia katika akaunti hiyo na kutolewa siku hiyo, hivyo kuifanya akaunti hiyo katika wiki mbili kupokea Sh31,590,200 na kiasi hicho kutolewa na kuifanya akaunti hiyo kubakiwa na salio la Sh474,045.45.

Kesi hii itakuwa ya kwanza ya aina yake kwa viongozi wa dini kufikishwa mahakamani wakikabiliwa na tuhuma za kusababisha Serikali kukosa mapato www.mwananchi.co.tz.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.