Skip to main content

Uchambuzi Wa Habari: Wabunge CCM Kumgomea Kikwete, Thubutu!



Ndugu zangu,

GAZETI la Mwananchi Jumapili lilibeba kwenye kurasa ya mbele habari yenye kichwa; “ Wabunge CCM wagoma kukutana na Kikwete.” Kwamba wajipanga kukwamisha muswaada wa mabadiliko ya Katiba.

Yumkini habari ile ilikuwa ni ‘burudani’ tu ya wasomaji kwa siku ya Jumapili. Maana, tunaojaribu kufuatilia siasa za nchi hii tunafahamu, kuwa jambo hilo haliwezekani. Nitafafanua.

Na ‘ The Citizen’ leo Jumanne kwenye kurasa ya mbele limebeba habari hii; “Katiba; Chadema, CCM in tug-of-war”.

Mwandishi Lucas Liganga anatutoa kwenye reli kwa kuripoti kuwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanadai kuwa mvutano kati ya Chadema na CCM unaweza kututoa kwenye reli mchakato wa kupata Katiba Mpya.

Swali ni hili; Ni nani aliyetoka kwenye reli?
Nahofia, kuwa wanaotajwa kuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa ndio waliotoka kwenye reli.

Nionavyo; mchakato wa mabadiliko ya Katiba bado uko kwenye reli kwa vile aliyeuweka kwenye reli bado anataka uwepo kwenye reli, ni JK.

Ndugu zangu,
Kwenye nchi za Kifalme, baada ya Mungu Mfalme ndiye anayefuatia. Insha-allah ina maana ya ’ neno la Mungu’ ama utashi wa Mungu. Na kwenye nchi ya Kifalme, basi, baada ya ’ Utashi wa Mungu’ unafuata ’ Utashi wa Mfalme’.

Na katika ’ Jamhuri’ kwa maana nchi zinazoongozwa na ’ Rais’ utaratibu ni huo huo; kwamba baada ya ’ utashi wa Mungu’ kinachofuata ni ’ utashi wa Rais’.

Ndio, katika mifumo hii ya utawala; mfalme na Rais wana nguvu nyingi zinazoweza kukaribiana na za Mungu. Ndio maana tunataka mabadiliko ya Katiba ambayo, mbali ya mambo mengine, yatapunguza nguvu za Rais. Katika dunia ya sasa, Rais hapaswi kuwa juu ya kila kitu.

Kinachoshangaza kwa wabunge wa CCM
Kama kuna wanaodhani hoja ya mabadiliko ya Katiba ni ya Chadema wanakosea. Mchakato wa kutaka mabadiliko ya Katiba n i hoja ya wananchi hata kabla ya kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Akina James Mapalala bado wako hai, wafuatwe waeleze historia ya harakati za kuleta mabadiliko ya Katiba katika nchi hii.

Wabunge wa CCM wafanye nini?
Tofauti na mazoea ya huko nyuma. Katika hili la Katiba na namna iliyo bora ya kuendesha mchakato huu ni suala ambalo haliepukiki kuwahusisha wananchi na watu wa vyama vya upinzani.
Mwenyekiti wao Kikwete ameshaliona hili. Kwa kulisimamia hili la Katiba kwa jinsi alivyoyapokea mapendekezo ya wadau wengine nje ya CCM , Kikwete anajitengezea mazingira ya kukubalika zaidi na Watanzania, na pia kuheshimiwa zaidi kama kiongozi wa nchi. Maana, atakuwa amekisikia kilio cha wengi.

Kwa wabunge wa CCM kumwekea ‘ mawe barabarani’ Mwenyekiti wao kimsingi wataharakisha kazi ya kuchimbwa kwa makaburi yao ya kisiasa na ya chama chao pia ifikapo mwaka 2015.

Katika mazingira ya sasa. Wabunge CCM, kwa kuamini kuwa Mwenyekiti wao wa chama ‘ kamwaga mboga’, nao wanaweza kuamua ‘kumwaga ugali’ kwa kupitia Bunge. Lakini, Mwenyekiti wao ana uwezo wa kwa haraka, kupika vyote viwili; mboga na ugali, akala na akashiba. Wabunge wake hawatakuwa na uwezo huo. Lakini, JK , katika saa 24 zijazo, kwa kadri upepo wa kisiasa utakavyovuma, anaweza pia kufanya kisichotarajiwa; anaweza, ama kulivunja Bunge au kulivunja Baraza la Mawaziri.

Ndio maana, jana tumemsikia Jenister Mhagama wa CCM akiwaambia wabunge wa CCM simu zao ziwe wazi na wasiwe mbali pindi watakapohitajika. Mwenyekiti wao ametua Dodoma jana.

Kwa wabunge wa CCM, hawawezi kwenda kinyume na ‘ utashi’ wa Mwenyekiti tena unaotokana na hekima yake ya kuwasikiliza anaowaongoza.

Kinatachoanyika sasa ni ‘ face-saving’- kwa wabunge wa CCM kutengeneza sentesi za ‘ kuziba nyuso’ na huku wakimpongeza Mwenyekiti wao kwa busara na hekima zake. Na anastahiki.

Na Mhagama huyo huyo jana ameongea na gazeti la Chama chake, Uhuru. Ni kwenye gazeti la Uhuru leo tunapoupata ukweli.

Na ukweli ni huu; “ Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama , amekanusha habari zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa, wabunge hao walipanga mkakati wa kukwamisha muswaada wa Katiba uliotarajiwa kuwasilishwa bungeni jana na kukutana na Rais Kikwete. ( Uhuru, Februari 7, 2012)

Na tusubiri tuone, kama Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama, naye amelidanganya gazeti la Chama chake.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Poland’s GROM special services mastermind found dead

Brigadier General Slawomir Petelicki, responsible for the formation of the GROM special services unit in the 1990s, was found dead at his apartment, Saturday, with bullet wounds to the head. Sławomir Petelicki, 1946-2012. Photo: Archive/PAP/Radek Pietruszka Police spokesman Maciej Karczynski informed that Petelicki’s body was found by his wife in the garage of his Warsaw apartment on Saturday. He was 65. Primary investigations point to suicide as the cause of death. It is expected that prosecutors will decide on an investigation into Petelicki’s death on Monday. After examining the scene of the incident, “the body of General [Petelicki] has been taken to a forensic laboratory, although a post-mortem will probably take place on Monday,” prosecutor Katarzyna Calow-Jaszewska from the Warsaw District Prosecution told the PAP news agency. “He was a tough man, a brilliant soldier and commander,” Colonel Krzysztof Przepiorka, head of the ...