Skip to main content

Uchambuzi Wa Habari: Wabunge CCM Kumgomea Kikwete, Thubutu!



Ndugu zangu,

GAZETI la Mwananchi Jumapili lilibeba kwenye kurasa ya mbele habari yenye kichwa; “ Wabunge CCM wagoma kukutana na Kikwete.” Kwamba wajipanga kukwamisha muswaada wa mabadiliko ya Katiba.

Yumkini habari ile ilikuwa ni ‘burudani’ tu ya wasomaji kwa siku ya Jumapili. Maana, tunaojaribu kufuatilia siasa za nchi hii tunafahamu, kuwa jambo hilo haliwezekani. Nitafafanua.

Na ‘ The Citizen’ leo Jumanne kwenye kurasa ya mbele limebeba habari hii; “Katiba; Chadema, CCM in tug-of-war”.

Mwandishi Lucas Liganga anatutoa kwenye reli kwa kuripoti kuwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanadai kuwa mvutano kati ya Chadema na CCM unaweza kututoa kwenye reli mchakato wa kupata Katiba Mpya.

Swali ni hili; Ni nani aliyetoka kwenye reli?
Nahofia, kuwa wanaotajwa kuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa ndio waliotoka kwenye reli.

Nionavyo; mchakato wa mabadiliko ya Katiba bado uko kwenye reli kwa vile aliyeuweka kwenye reli bado anataka uwepo kwenye reli, ni JK.

Ndugu zangu,
Kwenye nchi za Kifalme, baada ya Mungu Mfalme ndiye anayefuatia. Insha-allah ina maana ya ’ neno la Mungu’ ama utashi wa Mungu. Na kwenye nchi ya Kifalme, basi, baada ya ’ Utashi wa Mungu’ unafuata ’ Utashi wa Mfalme’.

Na katika ’ Jamhuri’ kwa maana nchi zinazoongozwa na ’ Rais’ utaratibu ni huo huo; kwamba baada ya ’ utashi wa Mungu’ kinachofuata ni ’ utashi wa Rais’.

Ndio, katika mifumo hii ya utawala; mfalme na Rais wana nguvu nyingi zinazoweza kukaribiana na za Mungu. Ndio maana tunataka mabadiliko ya Katiba ambayo, mbali ya mambo mengine, yatapunguza nguvu za Rais. Katika dunia ya sasa, Rais hapaswi kuwa juu ya kila kitu.

Kinachoshangaza kwa wabunge wa CCM
Kama kuna wanaodhani hoja ya mabadiliko ya Katiba ni ya Chadema wanakosea. Mchakato wa kutaka mabadiliko ya Katiba n i hoja ya wananchi hata kabla ya kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Akina James Mapalala bado wako hai, wafuatwe waeleze historia ya harakati za kuleta mabadiliko ya Katiba katika nchi hii.

Wabunge wa CCM wafanye nini?
Tofauti na mazoea ya huko nyuma. Katika hili la Katiba na namna iliyo bora ya kuendesha mchakato huu ni suala ambalo haliepukiki kuwahusisha wananchi na watu wa vyama vya upinzani.
Mwenyekiti wao Kikwete ameshaliona hili. Kwa kulisimamia hili la Katiba kwa jinsi alivyoyapokea mapendekezo ya wadau wengine nje ya CCM , Kikwete anajitengezea mazingira ya kukubalika zaidi na Watanzania, na pia kuheshimiwa zaidi kama kiongozi wa nchi. Maana, atakuwa amekisikia kilio cha wengi.

Kwa wabunge wa CCM kumwekea ‘ mawe barabarani’ Mwenyekiti wao kimsingi wataharakisha kazi ya kuchimbwa kwa makaburi yao ya kisiasa na ya chama chao pia ifikapo mwaka 2015.

Katika mazingira ya sasa. Wabunge CCM, kwa kuamini kuwa Mwenyekiti wao wa chama ‘ kamwaga mboga’, nao wanaweza kuamua ‘kumwaga ugali’ kwa kupitia Bunge. Lakini, Mwenyekiti wao ana uwezo wa kwa haraka, kupika vyote viwili; mboga na ugali, akala na akashiba. Wabunge wake hawatakuwa na uwezo huo. Lakini, JK , katika saa 24 zijazo, kwa kadri upepo wa kisiasa utakavyovuma, anaweza pia kufanya kisichotarajiwa; anaweza, ama kulivunja Bunge au kulivunja Baraza la Mawaziri.

Ndio maana, jana tumemsikia Jenister Mhagama wa CCM akiwaambia wabunge wa CCM simu zao ziwe wazi na wasiwe mbali pindi watakapohitajika. Mwenyekiti wao ametua Dodoma jana.

Kwa wabunge wa CCM, hawawezi kwenda kinyume na ‘ utashi’ wa Mwenyekiti tena unaotokana na hekima yake ya kuwasikiliza anaowaongoza.

Kinatachoanyika sasa ni ‘ face-saving’- kwa wabunge wa CCM kutengeneza sentesi za ‘ kuziba nyuso’ na huku wakimpongeza Mwenyekiti wao kwa busara na hekima zake. Na anastahiki.

Na Mhagama huyo huyo jana ameongea na gazeti la Chama chake, Uhuru. Ni kwenye gazeti la Uhuru leo tunapoupata ukweli.

Na ukweli ni huu; “ Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama , amekanusha habari zilizoandikwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa, wabunge hao walipanga mkakati wa kukwamisha muswaada wa Katiba uliotarajiwa kuwasilishwa bungeni jana na kukutana na Rais Kikwete. ( Uhuru, Februari 7, 2012)

Na tusubiri tuone, kama Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama, naye amelidanganya gazeti la Chama chake.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.