Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna Makinda akiingia ndani
ya ukumbi wa bunge leo mjini kuongoza kikao cha tisa cha mkutano wa
sita wabunge ambapo bunge linahitimisha shughuli zake mjini Dodoma.
Mbunge
wa Same Mashariki Anna Kilango akijadili jambo na Mwanasheria mkuu wa
serikali Jaji Frederick Werema ndani ya ukumbi wa Bunge leo wakati wa
kipindi cha maswali na majibu mjini dodoma
Mbunge
wa Singida mjini Mohammed Dewji akimsikiliza kwa makini Waziri wa
Nchi,Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu Stephen Wasira ndani ya ukumbi
wa bunge leo mjini Dodoma.
Wajumbe
na Viongozi wa chama cha wamiliki wa shule Vyuo na shule binafsi
(TAMONGSCO) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoka ndani ya
ukumbi wa bunge leo mjini Dodoma. Viongozi hao wapo bungeni Dodoma
kukutana na kamati ya kudumu ya bunge ya huduma za jamii kwa lengo la
kuhimiza ushirikiano kati yao na wabunge pamoja na serikali ili
kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazoikabili sekta binafsi
ya elimu nchini Tanzania.
Mbunge
wa Bumbuli January Makamba akiwasilisha Hoja binafsi kuhusu sheria ya
udhibiti wa shughuli za upangaji nyumba za makazi aliyoitoa chini ya
kanuni ya 54 (1) ya kanuni za bunge toleo la 2007 ya kuliomba bunge
kuazimia kwa kauli moja ,kuitaka serikali katika mkutano ujao wa saba
kuleta Muswaada wa Sheria ya kudhibiti Upangaji wa Nyumba na Makazi
kufuatia malalamiko mengi kutoka kwa wananchi wanaoishi mijini kutokana
na adha wanazopata katika kutafuta nyumba za kupanga au kuishi kwenye
nyumba hizo.
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akiwasalimia
viongozi na wachezaji wa timu ya Villa Squard ya Kinondoni jijini Dar
es salaam waliofika bungeni hapo kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa
na bunge.
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akifurahia
jambo na wanafunzi wa shule ya sekondari Hijra ya mjini Dodoma nje ya
ukumbi wa Bunge Dodoma.
Comments