Skip to main content

WATOTO LAKI 236 ELFU WALIOZALIWA KUANZIA MWAKA 2015 KATI YAO 9,400 WAMEFARIKI


Katibu Mkuu Wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto  DR Mpoki(kushoto) Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Dkt. Detlef Wachter wakionyesha vifaa kwa ajili ya kutolea huduma za matibabu kwa watoto njiti

 

Zaidi ya watoto njiti  laki 236 elfu  waliozaliwa katika kipindi kilichoanzia mwaka 2015 kati yao watoto 9,400 wamefariki kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo  kutokua na ujuzi wa namna ya kuwahudumia pamoja ukosefu wa vifaa vya kuwahudua hapa nchini.

Hayo yameelezwa leo  Jijini Dar es salaam  katika  hafla fupi ya Maadhimisho ya Siku Ya Mtoto Njiti Duniani  ambapo Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii jinsia Wazee na Watoto imekabidhiwa Vifaa mbalimbali vitakavyotumika kutoa huduma ya kuwahudumia watoto hao msaada uliotolewa na taasisi ya  Mradi wa kusaidia Afya Tanzania kutoka nchini  Ujerumani GIZ.

Akizungumza  katika Maadhimisho hayo jana  Katibu Mkuu Wa Wizara hiyo DR Mpoki  Ulusibisya  amsema  watotot wanao zaliwa bila ya kutimiza siku zao ndio wanao changia ongezeko la vifo vya watoto wachanga ambapo shirika hilo limeona Mkoa wa Mtwara na Lindi imekuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa hivyo na kusema kuwa vifaa hivyo vitasambazwa katika Mikoa hiyo.

Aidha DR MPOKI amsema GIZ imeweza kutoa mafunzo  Afya ya muda wa miaka miwili kwa watumishi wa  Afya  kwenye vituo vya kutolea huduma huku akielezea namna ambayo vifaa hivyo vitavyo weza msadia mtoto njiti

Kwa upande wake Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Mtwara DR  WEDSON SICHALWE amesema hali ya vifo kwa watoto wachanga  imekuwa ni mbaya ambapo asilimia  25 kila mwaka  katika mkoa wa Mtwara wanazaliwa watoto wenye uzito mdogo.

Comments