Skip to main content

Sikia maneno haya kutoka kwa Lema:Kafulila Usiende CCM peke yako, Nenda na Mkeo

 




Kwenye ukurasa wake wa twiter Godbless Lema ameandika ujumbe 
akisema Kafulila ni rafiki yake wa karibu, lakini kwa namna alivyoamua 
hana shaka atamshauri mke wake ambaye ni mbunge kupitia chama 
cha CHADEMA, kufanya kama yale aliyoyafanya.

"David Kafulila ni rafiki yangu, nafikiri kwa namna hii alivyoamua ataweza 
bila shaka kumshauri Mbunge wa Chadema, Jesca Kishoa (mke wake) 
kufikiri kama yeye, hii inaweza kusaidia maoni yake juu ya uamuzi 
aliouchukua leo na kuthibitisha ukweli huu kama hupo", ameandika 
Godbless Lema.

Jana David Kafulila ametangaza kukihama chama cha CHADEMA 
akidai vyama vya upinzani havina nia ya kupambana dhidi ya ufisadi, 
lakini mke wake Jesca Kishoa ambaye ni mbunge wa viti maalum 
kupitia CHADEMA bado hajazungumza chochote.



Comments