Skip to main content

MEYA WA JIJI DAR AFUNGUKA TAARIFA

 

Ndugu waandishi wa habari: Nimeshikwa na mshtuko, simanzi baada ya kusambaa kwa  taarifa ambazo naweza kusema kuwa ni za uzushi kwamba  ninampango wa kujiondoa ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema. naomba taarifa hizo zipuuzwe manahazina ukweli wowote na kwamba zinampango wa kunichafua mimi pamoja na Chama Changu.
Image result for meya wa jiji la dar
Ndugu wandishi wa habari : Napenda ieleweke kuwa  sijawahi kudhani wala kufikiria kuhama Chadema na kwenda kwenye chama chochote kile cha siasa. Chadema ni chama ambacho nimetoka nacho mbali tangu mwaka 2004 hadi leo, nimejenga chama kwa gaharama zangu mwenyewe.
waandishi wa habari: Leo nimekuwa Meya wa jiji la Dar es Salaam kupitia Chama Changu cha Chadema,natambua kuwa  chama kimeniheshimu sana kwa kunipa nafasi hii hivyo sina sababu ya kuondoka kwani  ninania ya kuwatumikia Wananchi ambao wameniamini na wamenichagua kwa mapenzi yao wakiamini kuwa nitawaletea Maendeleo nikiwa ndani ya Chama Cha Chadema.
.Nafahamu  tuhuma hizi zinatokana na aina ya utendaji wangu katika Jiji la Dar es Salaam kwani nimekuwa nikifanya kazi badala ya kupambana na serikali pale ambapo watu wanaamini kuwa mambo hayajaenda sawa.

Ndugu waandishi wa habari:  Kukaa kwangu kimya huku ,kutokufanya siasa za kiharakati ndani ya jiji la Dar es Salaam  haimanishi kwamba nipo upande wowote ama kukihujumu chama changu. Ila huu ni mfumo ambao nimeuchagua na kujijengea kwa ajili ya kuwatumikia wananchi nasio kufanya harakati za kisiasa kwakuwa nina  nia  ya kufanya maendeleo ndani ya jiji la Dar  es Salaam.
Ndugu waandishi wahabari: Naomba ifahamike kuwa hakuna Mkurya ambaye aliwahi kuwa msaliti,katika nafasi yoyote ambayo aliwahi kuwa nayo. Kutokana historia hiyo, naomba niaminike na wanachama na wananchi wote kuwa haitakuja kutokea Mkurya mimi nikakisaliti chama changu.
Nakama  itakuja kutokea nikafanya hivyo ninaweza kuhatarisha maisha yangu, Familia yangu, na hivyo kujikuta nikaingia kwenye matatizo makubwa ambayo kimsingi sio mazuri. Mama yangu ni mjane, kama itafanya hivyo Chadema wote Mkoa wa Mara hawawezi kuwaacha ndugu zangu salama .

Comments