Skip to main content

Rais Magufuli akiwa na Rais Museven Wazungumzia Uanzishwaji mahakama maalum kushughulikia ufisadi na udhibiti wa safari holela


Rais Magufuli akiwa na Rais Museven(picha na mtandao)
UANZISHWAJI wa mahakama maalum kushughulikia ufisadi na udhibiti wa safari holela kwenda nje ya nchi ni miongoni mwa maeneo yaliyotajwa na Rais John Magufuli kuwa ndiyo yanayoipa Tanzania mafanikio makubwa katika vita isiyokoma dhidi ya rushwa na ufisadi. 

Mambo mengine, ambayo hujengwa na dhamira ya dhati ya serikali katika kuondokana na tatizo hilo linalochukuliwa kwa uzito mkubwa kama ilivyo kwa mapambano dhidi ya ugonjwa wa kansa, ni pamoja na kuwaondoa watumishi hewa, kuwabaini na kuwaondoa watu wenye vyeti bandia ndani ya kada ya utumishi wa umma na pia kukomesha ‘dili’ za rushwa.
 

Rais Magufuli alitoa ufafanuzi huo nchini Uganda jana wakati alipoulizwa na waandishi wa habari mbele ya mwenyeji wake, Rais Yoweri Museveni, kuhusu siri ya mafanikio ya serikali yake katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi.
 

Baada ya ufafanuzi huo ulioambatana na maelezo ya kina, Rais Museveni alionyesha kuvutiwa na yale yanayofanyika Tanzania na kuahidi kuiga mazuri hayo ili kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya rushwa nchini kwake.
 

Rais Magufuli alitoa ‘darasa’ hilo kwa Waganda alipokuwa na mwenyeji wake katika Ikulu ndogo ya Masaka nchini Uganda ambako, Rais Magufuli alikuwa akiendelea na ziara yake ya kikazi ya siku tatu nchini humo.
 

Awali, mwandishi mmojawapo katika hafla hiyo alimuuliza Magufuli namna serikali yake ilivyofanikiwa katika vita dhidi ya rushwa na namna ambavyo anaweza kumshawishi mwenyeji wake, Rais Museveni, kuiga hatua alizochukua.
 

Katika ufafanuzi wake, Magufuli alisema rushwa bado ipo Tanzania licha ya kwamba hatua zimeanza kuchukuliwa na kuongeza kuwa serikali inayopiga vita rushwa ni lazima ionyeshe njia kwanza.
 

Akielezea zaidi, Rais Magufuli alisema alianzisha mahakama maalum kushughulikia mafisadi, pamoja na kufuta mianya ya rushwa ikiwamo mishahara hewa, kufuta safari holela za nje ya nchi ambazo zilikuwa nyingi kaisi kwamba baadhi ya vigogo walikuwa wakiishia uwanjani na wake zao kuwapelekea mabegi kabla hawajapanda ndege kusafiri tena, lakini sasa hilo halipo baada ya safari zote za lazima kuhitaji vibali maalumu kutoka kwake na kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
 

Alisema hatua zote hizo, zikiwamo pia za udhibiti wa mianya ya rushwa katika maeneo mbalimbali, zimewezesha fedha kuokolewa na mwishowe kuelekezwa katika shughuli za maendeleo kwa ajili ya kuwanufaisha wananchi.
 

Akitoa mfano, Rais Magufuli alisema hata yeye amekuwa akikataa kusafiri nje ya nchi pasipokuwa na ulazima wa kufanya hivyo, pamoja pia na makamu wake wa rais na pia waziri mkuu na badala yake kuwatuma mawaziri, lengo likiwa ni kupunguza gharama kubwa za safari zinazotokana na ukubwa wa msafara wake, makamu na waziri mkuu.
 

“Kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa (UN) hivi karibuni, nilitakiwa mimi nihudhurie lakini nilimtuma Waziri wa Mambo ya Nje … na nilimsisitizia itakuwa safari ya watu watatu tu. 


Alikwenda na alituwakilisha vizuri sana,” alisema na kuongeza: 
Aidha, alisema watumishi hewa 20,000 walilipwa mshahara wa Sh. bilioni 238.7 kwa mwaka na kwamba fedha hizo zimeokolewa baada ya kuondolewa kwao.
 

Kuhusu vyeti feki, Rais Magufuli alisema zaidi ya watumishi 12,000 walilipwa bilioni 142 kwa mwaka, licha ya kutokuwa na sifa za elimu na kitaaluma na baadhi yao waliwekwa kwenye nyadhifa na nafasi mbalimbali za uongozi.
 

Kwa upande wake, Rais Museveni, alisema ameona matokeo mazuri ya serikali ya Tanzania baada ya kuanza kuchukua hatua za kupiga vita rushwa na kwamba tatizo kubwa Uganda ni kuwapo kwa urasimu ambao unasababisha rushwa.
chanzo:muungwana

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...