Skip to main content

Wakandarasi katika halmashauri Ilala wametakiwa kutumia vifaa vya kisasa katika kusafisha maeneo yao


Image result for KUMBI LA MOTO
Naibu Meya wa manispaa ya Ilala Omari Kumbilamoto(picha na mtandao)

Katika  kuifanya  halmashauri ya Ilala jijini  Dar es Salaam kuwa  safi na ya kuvutia wakandarasi  katika halmashauri hiyo wametakiwa kutumia vifaa vya kisasa katika kusafisha maeneo wanayoyasimamia.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Diwani wa kata ya Vingunguti na naibu Meya wa manispaa ya Ilala Omari Kumbilamoto wakati  akizungumza na mwandishi wa habari hizi  mara baada ya kurejea kwake hapa nchini akitokea nchini Dubai ambapo alikuwa nchini humo kwa takriban wiki mbili kwa lengo la kujifunza namna ambavyo manispaa za miji mingine  zinavyoweza kutekeleza majukumu yake .

Aidha Kumbilamboto akizungumzia  kuhusu  kata ya vingunguti amesema kata hiyo imeweza kutatua changamoto wanazokabiliana nazo kwa asilimia tisini huku akilipongeza jeshi la polisi kwa kutoa mafunzo kwa walinzi shirikishi katika kata hiyo ambayo yamefanikisha usalama kwa watu wapitao usiku wakielekea machinjioni.

Diwani huyo wa kata ya vingunguti na naibu meya wa manispaa ya Ilala amewataka  wakazi wa kata hiyo kuongeza umoja na mshikamano baina yao na kutokuingiza itikadi za vyama vyao katika masuala ya maendeleo.

Comments