Skip to main content

SUMU AMBAYO HUPASWI KUMUAMBIA MPENZI WAKO



Unapokuwa faragha na mpenzi wako, kuna baadhi ya mambo unatakiwa kuyaepuka kwani yanaweza kutibua hali ya hewa na mwishowe kutopata ile furaha mliyodhamiria. Achilia mbali hayo ya kufanya, pia kuna maneno ambayo unatakiwa kujichunga sana kutoyatamka pale unapokuwa kwenye uwanja wa kujidai na mpenzi wako.

Haya nayo madhara yake ni makubwa kwani yanaweza hata kuufanya uhusiano wenu ukafikia tamati. Maneno hayo 8 ni haya yafuatayo;

1.Sitaki hivi na vile

Unapokuwa faragha na mpenzi wako hutakiwi kugomea vitu ambavyo mpenzi wako anataka kukufanyia tena kwa ukali. Kwa mfano, kuna baadhi ya wanawake wanaposhikwa maeneo flani ya miili yao husema; ‘bwana mi staki, mwenzio unanichanganya’.

 Sentensi hiyo inapotolewa kimahaba haina madhara na inaweza kunogesha mambo kwani inaeleweka mwanamke anaposema hivyo anamaanisha nataka sitaki, lakini unapomwambia mpenzi wako sitaki hiki tena kwa lugha ya ukali ukimaanisha unachokisema, unaweza kuharibu mambo.

2. Hivyo siyo vizuri 

Unamwambia mpenzi wako kwa macho makavu kuwa anavyokufanyia siyo vizuri? Hapana, hiyo siyo poa. Hata kama uko ‘streiti’ lakini tafuta njia nyingine ya kumfikishia ujumbe huo bila kumharibia ‘mudi’ yake kwani wanaume si watu wanaopenda kukosolewa katika kila jambo.

3.Siyo mkali uwanjani

Unaweza kujikuta umeangukia kwa mwanaume ambaye hayajui ‘majamboz’, yaani wewe ndiye unayechukua muda mwingi kumuelekeza afanyeje ili muipate furaha. 

Hilo siyo suala la kukufanya uanze kumlaumu na kufikia hatua ya kumchana laivu kuwa yeye siyo mkali. Mvumilie, endelea kuwa naye huku ukiamini siku moja atakuwa mzoefu. Fahamu kuwa, kisaikolojia ukimwambia siyo mzuri faragha ndiyo unazidisha tatizo na anaweza kuona ni bora asiwe na wewe kabisa ili kukwepa kuumbuka.


4. Wewe siyo mtundu kama x-dear wangu

Kwanza unatakiwa kujua kuwa, uwapo faragha hutakiwi kuuzungumzia uhusiano wako uliopita, kwa kuufananisha au kuutofautisha. Hivyo hutakiwi pia kumwambia mpenzi wako kuwa yeye siyo mtundu kama mpenzi wako wa zamani. Ukimwambia hivyo utamfanya ahisi ipo siku unaweza kumuacha na kumrudia wa zamani, mazingira ambayo siyo mazuri.


5. Ingekuwa yule wangu wa zamani angenifanyia hivi

Kwa mfano mpenzi wako hataki kukufanyia kitu flani ambacho uliwahi kufanyiwa na mpenzi wako wa zamani, hutakiwi kuwa muwazi katika hilo. Cha kufanya akishaonesha hataki kukufanyia hicho kitu, mpotezee kisha endeleeni na mambo mengine, wala usimkumbushie kuwa ingekuwa mpenzi wako wa zamani angekufanyia. 

6. Mbona hufanyi sahihi 

Kweli anaweza kufanya mambo katika njia ambayo unaona siyo sahihi kwako lakini huna sababu ya kuwa mkali, mwelekeze namna unavyotaka afanye tena kwa upole kwa kutumia lugha ya kimahaba.

 7. Hii inaboa, unaniboa


Hata kama ndiyo ukweli wenyewe lakini unapokuwa faragha na mpenzi wako epuka kumwambia anakuboa au anafanya mambo yanayokuboa. Ukimtamkia hivyo, wewe utakuwa umemboa zaidi na furaha lazima itoweke. 

8. Jina la mwanaume mwingine 
Dah!Kama unataka siku hiyo hiyo uachwe, jaribu kutaja jina la mwanaume mwingine wakati uko faragha na mpenzi wako. Ni mbaya sana kwani unaonesha unamuwaza sana yeye kuliko mpenzi wako.

 Katika hili nalo unatakiwa kuwa makini. Hayo ndiyo baadhi ya maneno ambayo unatakiwa kutumia gharama yoyote kuyaepuka unapokuwa faragha na mpenzi wako. 

Tambua penzi linashikiliwa na vitu vidogovidogo sana ambayo unaweza kuvidharau lakini madhara yake yakawa makubwa. Kwa maana hiyo, hakikisha kila neno unalotaka kulitoa mdomoni mwako kwenda kwa mpenzi wako unalipima kwanza, usipofanya hivyo unaweza kuja kujuta siku moja. chanzo:bongo hot zone

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...