Skip to main content

Angaza siasa Mugabe akubali kung'atuka kwa masharti mawili





Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amekubali kujiuzulu kwa masharti mawili. 

Masharti hayo ni kuwekewa kinga ya kutoshitakiwa yeye na mkewe Grace Mugabe, pamoja na kubaki na mali zake zote.Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na timu ya majadilliano  kimeliambia  shirika la utangazaji la CNN kwamba Mugabe ameshaandaa barua ya kujiuzulu.



Chanzo hicho kimeeleza kwamba majenerali  wa jeshi la nchi hiyo wameridhia matakwa hayo. CNN limeambiwa kwamba chini ya makubaliano hayo, Mugabe na Grace hawatashtakiwa.
Pia, viongozi wawili waandamizi wa serikali ya Mugabe wameliambia shirika la habari la Reuters Jumapili kwamba Mugabe alikuwa amekubali kujiuzulu lakini hawakuwa wanajua yaliyomo katika mkataba wa kuondoka kwake.
“Ili ionekane amejiuzulu rasmi, utaratibu ni kwamba barua lazima iandikwe kwenda kwa Spika wa Bunge”, Chanzo kingine kimeongeza.
Mugabe ambaye anakabiliwa na shinikizo la kuachia wadhifa wake jana aliwashangaza watu kwa kushindwa kutangaza kujiuzulukinyume na matarajio ya wengi alipokuwa akilihutubia Taifa kwa njia ya Televisheni.

Aidha chama chake cha Zanu -PF kilikuwa kimempa kimempa muda hadi kufikia mchana wa leo awe ameng’atua na kama asipofanya hivyo atashtakiwa bungeni.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, maelfu ya wananchi wa Zimbabwe wakiongozwa na jeshi waliaandamana kwa ajili yakumshinikiza ajiuzulu.

Comments