Skip to main content

watetezi wa haki za binadamu waibukakuishauri Idara ya Uhamiaji


BARAZA la Habari Tanzania (MCT), Mtandao wa Wawatetezi wa Haki za  Binadamu Tanzania (THRDC), na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) umeishauri Idara ya Uhamiaji Tanzania kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kwa matakwa ya sheria.

Wito huo ulitolewa jana na watetezi wa haki za binadamu jijini Dar es Salaam kufuatia kitendo cha kukamatwa maofisa wa Kamati ya Ulinzi wa Waandishi wa Habari (CPJ) Angela Quintal raia wa Afrika ya Kusini na Muthoki Mumo raia wa Kenya.

Awali akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Katibu Mtendaji wa MCT Pili Mtambalike, alisema Maofisa hao wa CPJ walikamatwa na watu watatu ambao mmoja wao alijitambulisha kuwa ni Ofisa  wa Idara ya Uhamiaji mnamo tarehe 7 mwezi huu majira ya saa 4.30 usiku katika Hotel ya Southern Sun ya jijini Dar es Salaam.

Baada ya kukamatwa Maofisa hao walipekuliwa, walihojiwa na kupokonywa vitendea kazi vyao, ikiwemo komyuta mpakato, simu pamoja na hati zao za kusafiria na baadae maofisa hao kurudishiwa vifaa vyao na kuamriwa waendelee na shughuli zao.

“Kulingana na hofu iliyotanda kwakukamatwa kwao wadau wa Habari walifanya jitihada kwakushirikiana na balozi za wadau hao wa Habari kurudishiwa hati zao za kusafiria lakini balozi husika ziliwashauri kurudi makwao,”alisema

Kwa upande wake Ofisa Programu Utetezi LHRC Raymond Kanegene alisema Waandishi hao walikuja Tanzania kwa minajili ya kuangalia hali ya Usalama wa Waandishi wa Habari Tanzania lakini taarifa zilizotoka kwa msemaji wa Idara ya Uhamiaji Ally Mtanda zilisema waandishi hao walikiuka mashariti ya visa kwakuwa walipewa hati ya matembezi.

“Cha kusikitisha maofisa hao wakati wakukamatwa kwao hawakuambiwa sababu za kukamatwa kwao, badae Idara ya Uhamiaji iliwachia huru pasina shariti lolote na hivyo kuleta shaka kwao, kwamba huenda hakukuwa na sababu za msingi za kukamatwa hivyo basi tunawaomba ndugu zetu wa uhamiaji kuwa makini,”alisema
Hata hivyo Kanegene alisema ingetumika njia nyingine ya kushughulikia suala la wanakamati ya CPJ kuliko njia iliyotumika na kutahadharisha kuwa haileti haiba njema kwa mahusiano ya kimataifa kanakwamba Tanzania siyo sehemu salama.

Naye Mratibu Taifa wa THRDC Onesmo Ngurumwa alisema watetezi wa haki za binadamu hawakulizishwa na hatua zilizo chukuliwa dhidi ya wadau wa Habari kutoka nchi hizo za jirani.

“Kwa umoja wetu tunasikitishwa na namna Idara ya Uhamiaji ilivyo watendea Maofisa hao wa CPJ kwakuwa walikuja nchini kihalali na hata kuachiwa kwao hakukua na mashariti yoyote waliyopewa zaidi ya kuambiwa waendelee na shughuli zao, hii ni dhahiri kuwa hawakuwa na kosa lolote ,”alisema

Kutokana na sintofahamu iliyojitokeza waandishi wa Habari nchini wametakiwa kufanya kazi zao kwa weledi na kufuata sheria za nchi lakini Idara ya Uhamiaji ifanye kazi zake kwa weledi na kuzingatia mikataba ya kimataifa ambayo Tanzania imeridhia ili kudumisha Amani, upendo na mshikamano.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.