Skip to main content

watetezi wa haki za binadamu waibukakuishauri Idara ya Uhamiaji


BARAZA la Habari Tanzania (MCT), Mtandao wa Wawatetezi wa Haki za  Binadamu Tanzania (THRDC), na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) umeishauri Idara ya Uhamiaji Tanzania kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kwa matakwa ya sheria.

Wito huo ulitolewa jana na watetezi wa haki za binadamu jijini Dar es Salaam kufuatia kitendo cha kukamatwa maofisa wa Kamati ya Ulinzi wa Waandishi wa Habari (CPJ) Angela Quintal raia wa Afrika ya Kusini na Muthoki Mumo raia wa Kenya.

Awali akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Katibu Mtendaji wa MCT Pili Mtambalike, alisema Maofisa hao wa CPJ walikamatwa na watu watatu ambao mmoja wao alijitambulisha kuwa ni Ofisa  wa Idara ya Uhamiaji mnamo tarehe 7 mwezi huu majira ya saa 4.30 usiku katika Hotel ya Southern Sun ya jijini Dar es Salaam.

Baada ya kukamatwa Maofisa hao walipekuliwa, walihojiwa na kupokonywa vitendea kazi vyao, ikiwemo komyuta mpakato, simu pamoja na hati zao za kusafiria na baadae maofisa hao kurudishiwa vifaa vyao na kuamriwa waendelee na shughuli zao.

“Kulingana na hofu iliyotanda kwakukamatwa kwao wadau wa Habari walifanya jitihada kwakushirikiana na balozi za wadau hao wa Habari kurudishiwa hati zao za kusafiria lakini balozi husika ziliwashauri kurudi makwao,”alisema

Kwa upande wake Ofisa Programu Utetezi LHRC Raymond Kanegene alisema Waandishi hao walikuja Tanzania kwa minajili ya kuangalia hali ya Usalama wa Waandishi wa Habari Tanzania lakini taarifa zilizotoka kwa msemaji wa Idara ya Uhamiaji Ally Mtanda zilisema waandishi hao walikiuka mashariti ya visa kwakuwa walipewa hati ya matembezi.

“Cha kusikitisha maofisa hao wakati wakukamatwa kwao hawakuambiwa sababu za kukamatwa kwao, badae Idara ya Uhamiaji iliwachia huru pasina shariti lolote na hivyo kuleta shaka kwao, kwamba huenda hakukuwa na sababu za msingi za kukamatwa hivyo basi tunawaomba ndugu zetu wa uhamiaji kuwa makini,”alisema
Hata hivyo Kanegene alisema ingetumika njia nyingine ya kushughulikia suala la wanakamati ya CPJ kuliko njia iliyotumika na kutahadharisha kuwa haileti haiba njema kwa mahusiano ya kimataifa kanakwamba Tanzania siyo sehemu salama.

Naye Mratibu Taifa wa THRDC Onesmo Ngurumwa alisema watetezi wa haki za binadamu hawakulizishwa na hatua zilizo chukuliwa dhidi ya wadau wa Habari kutoka nchi hizo za jirani.

“Kwa umoja wetu tunasikitishwa na namna Idara ya Uhamiaji ilivyo watendea Maofisa hao wa CPJ kwakuwa walikuja nchini kihalali na hata kuachiwa kwao hakukua na mashariti yoyote waliyopewa zaidi ya kuambiwa waendelee na shughuli zao, hii ni dhahiri kuwa hawakuwa na kosa lolote ,”alisema

Kutokana na sintofahamu iliyojitokeza waandishi wa Habari nchini wametakiwa kufanya kazi zao kwa weledi na kufuata sheria za nchi lakini Idara ya Uhamiaji ifanye kazi zake kwa weledi na kuzingatia mikataba ya kimataifa ambayo Tanzania imeridhia ili kudumisha Amani, upendo na mshikamano.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...