Skip to main content

TRA:Yatakiwa kuongeza vyanzo vya mapato

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetakiwa kuongeza vyanzo vya mapato kuliko kutegemea vyanzo vilivyopo.
Picha
Agizo hilo limetolewa mwishoni mwa wiki na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk.Ashatu Kijaji alipokuwa akihutubia wahitimu na wageni waalikwa kwenye mahafali ya 11 ya Chuo cha Kodi (ITA) yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viunga vya Chuo hicho kilichopo Mwenge Dar es Salaam.
Dk.Ashatu alisema kuwa TRA hawana budi kuwa wabunifu katika kubuni miradi itakayoongeza mapato serikalini nakuepukana na lawama za ubadhirifu kwa baadhi ya watumishi wa Mamlaka hiyo.

Vilele Dk.Ashatu alitoa miezi sita kwa mamlaka hiyo kuhakikisha kodi ya pango la nyumba inalipwa lakini akionya kutenda haki katika ukadiriaji wa kodi hizo kulingana na uwiano wa nyumba husika.

“Niwape miezi sita kuhakikisha Kodi ya majengo inakusanywa lakini mtende haki kwa wananchi kwakukadiria kodi kulingana na ukubwa wanyumba, eneo nyumba ilipo na thamani ya nyumba kwakufanya hivyo mtakuwa mmejitoa katika lawama na mapato mtakusanya,”amesema.

Aidha Dk.Kijaji alipokuwa akijibu changamoto zilizoainishwa na Kamishina Mkuu wa TRA Charles Kichere ambapo kubwa ilikuwa  ufinyu wa bajeti ambayo TRA na Chuo cha Kodi wanapatiwa na Serikali, Dk. Ashatu aliwataka wabuni miradi endelevu ambayo itawapatia fedha nakuweza kuendesha majukumu yao ya kiutendaji.

“Kwa TRA niwaombe mbuni miradi endelevu itakayo wasaidia katika kukabiliana na kampeni na doria kwa wakwepa kodi kwakufanya hivyo mtakuwa mmefanikiwa lakini pasipo kufanya hivyo suala la kukusanya kodi kwakutegemea bajeti yenu ni gumu,”amesema.

Kwa upande wa Chuo cha Kodi Dk. Ashatu alipokuwa akijibu changamoto zilizo ainishwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Dk. Samwel Werema, kuhusu ufinyu wa bajeti wa Chuo hicho, Dk Ashatu alikitaka chuo kuandika maandiko na kufanya tafiti zitakazo waongezea fedha kwa ajili yakuendesha Chuo.
Mkuu wa Chuo Profesa Isaya Jairo aliiomba Serikali kuongeza bajeti ya uendeshaji wa chuo ili kuzalisha wataalamu bora zaidi hususani wale wanaobaki kufundisha ili wapatiwe mafunzo zaidi nje ya nchi ili warudipo watoe mchango mkubwa katika chuo na Taifa.
Hata hivyo wahitimu waliaswa kujiepusha na tamaa ya utajiri wa haraka ambao utawaingiza katika rushwa ambapo watakapo bainika watakosa ajira na kunyang’anywa cheti.

“Jiepusheni na rushwa, rushwa ni adui wa haki na maendeleo ,msitafute utajiri wa haraka Taifa linawategemea mkawe hodari na waaminifu huko makazini mkaoneshe utofauti na wahitimu wengine ili tujivunie kuwa tumezalisha wahitimu bora,”amesema.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...