Skip to main content

Mauaji ya Khashoggi hayawezi kuathiri uhusiano wa Marekani na Saud Arabia

Rais wa marekani Donald Trump ametetea uhusiano wa karibu uliopo kati ya marakeni na Saud Arabia bila kujali lawama juu ya mauaji ya mwanahabari Jamal Khashoogi yanayoiandama Saud Arabia.
Kwa mujibu wa BBC, Trump amesisitiza kuwa huenda mwanamfalme Mohamed Bin Salman alijua kuhusu mauaji lakini uhusiano uliopo ni baina yake na Saud Arabia na hawezi kuupoteza. Rais huyo wa nchi yenye nguvu zaidi duniani amewaambia waandishi wa habari kuwa asingependa kuharibu uchumi wa dunia kwa kuwa na mahausiano mabaya na Saud Arabia.
”Siwezi kuwambia nchi inayotumia pesa zake nyingi na imenisaidia kitu kimoja kikubwa sana, bei ya mafuta, sasa imetulia haipandi wala kushuka, hivyo siwezi kuharibu uchumi wa dunia kwa kuanza kuwa na uhusiano mbaya na Saud Arabia, siwezi kuharibu uchumi wa dunia na uchumi wa nchi yetu”. Trump ameongeza pia, kuvunja uhusiano na Saud Arabia ni sawa na kuachia pesa nyingi ziende kwa mataifa mengine kama Urusi na China.
”Ni marekani kwanza kwangu mimi, hatuwezi kuachia mabilioni ya pesa yaende kwa Urusi na China, na watu wengine wazipate, ni kuhusu mimi , ni rahisi tuu, marekani kwanza, na tukivunja huu uhuasiano mtaona bei za mafuta zitakavyopanda, sasa hivi nimeziweka chini, na wamenisaidia kufanya hivyo , na ningependa bei ishuke zaidi.” Kuhusu mwanamfalme bin Salman kuhusika na mauaji , trump amesema inawezekana Bin Salman alikua akijua kuhusu tukio hilo ama asiwe ana taarifa yoyote.
Uchunguzi wa shirika la kijasusi la nchi hiyo CIA ulioripotiwa na vyombo vya habari vya Marekani unaonesha kuwa uwezekano ni mkubwa kuwa bin Salman aliidhinisha mauaji ya Khashoggi. Lakini Trump anasema uchunguzi huo haujakamilika kwa asilimia 100.
Khashoggi aliuawa ndani ya ofisi za ubalozi wa Saudia mjini Istanbul Uturuki alipoenda kuchukua nyaraka kuhusu talaka yake na aliyekuwa mkewe nchini Saudia. Khashoggi alikuwa mkosoaji kinara wa sera za Saudia hasa zile za bin Salman na alikimbilia uhamishoni Marekani mwaka 2017 akihofia usalama wake.
Kwa upande wa Saud Arabia wamekuwa wakikanusha uhusika wa Bin Salman katika tukio hilo. Awali walikanusha kabisa kutokea kwa mauaji hayo lakini baada ya kubanwa walikiri na kulaumu oeresheni haramu iliyofanywa na maaisa usalama wa nchi hiyo.
Kauli ya Trump inawapa nafuu viongozi wa Saudia ambao wamekuwa wakipitia wakati mgumu kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa kutokana na mauaji hayo. Bado mwili wa mwanahabari huyo haujapatikana na inaaminika ulitoswa kwenye tindikali ili kupoteza ushahidi.
Hata hivyo, wakosoaji wa Trump wameshtushwa na kauli yake ya kuitetea Saudia. Tayari wajumbe wa Bunge la Wawakilishi la Marekani kutoka vyama vyote viwili vya Republican na Democrat wametishia kuwasilisha muswada wa kuiwekea vikwazo nch ya Saudia.
Katika maelezo yake, Trump aliisifia Saudia kuwa mshirika imara katika kuibana Iran katika programu yake ya matumizi ya teknolojia ya nyuklia.
Maelezo hayo ya Marekani yamepingwa vikali na Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran Javad Zarifambaye amesema ni ajabu kuona Trump anatumia jina la Iran katika utetezi wa tukio hilo, “Itakuwa Iran pia imesababisha moto wa nyika unaoendelea California. Maana sasa kwenye kila shida inayoikumba Marekani, Iran tunahusishwa.”

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...