Skip to main content

CUF yampongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwakutatua changamoto ya ununuzi wa Korosho


Chama cha Wananchi CUF kimempongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwakutatua changamoto ya ununuzi wa Korosho iliyokuwa ikiwakabili wakulima wa zao hilo katika Mikoa ya Kusini mwa Tanzania.

Tokeo la picha la Chama cha Wananchi CUF
Pongezi hizo zimeolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano Abdul Kambaya, alipozungumza na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya CUF Jijini Dar es salaam.

“Chama cha Wananchi CUF kinampongeza Rais Dk.John Pombe Magufuli kwa hatua aliyoichukuwa ya kununua korosho zote za wakulima, jambo hilo ni jema kwa maslahi ya wakulima na Uchumi wa Taifa,”amesema Kambaya
Vilele Kambaya alisema Sera ya Uchumi ya Ilani ya chama chao imeandikwa bayana jinsi itakavyo watetea wanyonge hususani wakulima nakueleza kuwa maamuzi yaliyofanywa na Rais yana mashiko.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF Mneke Jafari , alisema sanjari na jitihada zilizochukuliwa na Rais jitihada zaidi zinahitajika kumkomboa mkulima kwakua ndiye anaye changia pato kubwa la Taifa (GDP) kwa 70%.

“Ipo haja ya yakupitia upya sera na mfumo wa Wizara ya Kilimo na Chakula ili kuepuka matatizo yanayojitokeza katika ununuzi wa mazao na bidhaa za kilimo za aina zote,  ikiwemo uwajibishwaji wa Bodi zisizo kizi vigezo kisheria,”amesema.

Wakati huohuo Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano Abduli Kambaya alizungumzia kuhama kwa Mbunge wa Temeke (CUF) Abdalah Mtolea na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi alisema CUF ipo imara.

“Hili ni vuguvugu la siasa na Mtolea siyo wa kwanza kuhama lakini cha kushangaza hoja zakuhama kwake ni dhaifu zote ukizipitia hazina mashiko mathalani kuhofia kufukuzwa wiki ijayo wakati hakuwa na ushahidi wa kimaandishi kuwa angelifukuzwa,”amesema.

Vilevile Kambaya alisema miongoni mwa hoja ambazo hazina mashiko nikuisifia CHADEMA kuwa ndiyo waliokuwa wakimpa ushirikiano kuliko CUF na badala yake CUF imegubikwa na migogoro nakutangaza Bungeni kuwa yupo tayali kushirikiana na Chama chochote na baada ya saa chache alijiunga na CCM.

Hata hivyo Kambaya alichambua wanasiasa wanaohama kutoka upinzani kuelekea CCM akisema kundi la kwanza ni la Viongozi ambao bado wanahisi wataendelea kuwa Viongozi.

Na kundi la pili alisema ni kundi ambalo haliridhiki kiuchumi na kile wanachokipata wakiamini CCM watapatiwa nyadhifa za juu kama  Ukuu wa Wilaya, Ukurugenzi wa Halmashauri, Ukuu wa Mkoa na Ubalozi.

Kushiriki au kutokushiriki katika uchaguzi utakaofanyika baada ya Mbunge Mtolea kuhama chama kutaamuliwa na Halmashauri ya Baraza Kuu la CUF ndiyo lenye Mamlaka ya kuamua washiriki au laa.

Comments