Skip to main content

HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA MHE. GEORGE H. MKUCHIKA (MB), KWENYE UFUNGUZI WA KONGAMANO KUHUSU “KUKUZA NA KUIMARISHA UONGOZI NA VIONGOZI TANZANIA”, KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE, DAR ES SALAAM, 02 NOVEMBA, 2018



            MHESHIMIWA MIZENGO PINDA, WAZIRI MKUU MSTAAFU WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,MHESHIMIWA ANNE MAKINDA, SPIKA MSTAAFU WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,DKT. LAUREAN NDUMBARO, KATIBU MKUU, OFISI YA RAIS -MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA,PROF. JOSEPH SEMBOJA, AFISA MTENDAJI MKUU, TAASISI YA UONGOZI,VIONGOZI WASTAAFUVIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA, SERIKALI, MASHIRIKA YA UMMA, BINAFSI NA ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI,WAGENI WAALIKWA,WAANDISHI WA HABARI,MABIBI NA MABWANA.

Napenda nitumie fursa hii kuwashukuru waandaaji wa Kongamano hili, Taasisi ya UONGOZI, kwa kunipa heshima kubwa ya kuwa Mgeni Rasmi. Nawashukuru na kuwapongeza kwa maandalizi mazuri ya Kongamano hili lenye umuhimu mkubwa, hasa wakati huu ambapo Serikali inakamilisha matengenezo ya Program ya Maboresho ya Utumishi wa Umma Awamu ya Tatu ambayo inatambua na kusisitiza umuhimu wa kukuza na kuimarisha Uongozi na viongozi ndani ya Sekta na Umma. Hivyo, mawazo yatakayotokana na mjadala wa leo yatatumika kuimarisha Program hii ya maboresho Serikalini.

Ndugu Washiriki;

Kongamano hili kuhusu “Kukuza na Kuimarisha Uongozi na Viongozi Tanzania” ni muhimu kwetu sote; Serikali, Bunge na Mahakama; Mashirika ya Umma na Binafsi na; Vyama vya Siasa na Asasi zisizo za Kiserikali. Litatoa fursa ya kubadilishana taarifa, mawazo na uzoefu kuhusu dhana ya uongozi na mikakati ya kukuza na kuimarisha uongozi na viongozi nchini Tanzania na kwingineko.  Litatoa fursa ya kutathmini hali ilivyokuwa huko nyuma, tangu miaka ya uhuru, hadi hivi sasa; na yapi mazuri yakuendeleza huko tuendako.  

Uongozi bora ni msingi wa maendeleo endelevu katika jamii au taifa lolote duniani. Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliliona hili na kuliweka wazi alipotamka masharti manne ya maendeleo kwa Taifa ambayo ni: watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Hili la uongozi bora ambalo ndio mada yetu ya leo alilifanyia kazi kwa nguvu zake zote.

Ndugu Washiriki;

Kuandaa, kujenga na kuimarisha uongozi na viongozi wa sasa na wa baadaye ni mchakato mpana unaohusisha mifumo rasmi na isiyo rasmi. Kwa Tanzania, ni mchakato ulioanza kabla ya uhuru wa Tanganyika, ambapo Chama cha TANU katika miaka ya mwisho ya 1950 kiliamua kuanzisha Chuo cha Kivukoni kwa lengo la kuandaa viongozi wa ngazi za juu katika Taifa jipya la Tanganyika. Aidha, Taasisi ya Mzumbe (Institute of Development Management) ililenga kujenga viongozi wa Serikali za Mitaa hadi mwanzoni mwa miaka ya 1970 ambapo Serikali za Mitaa ziliondolewa. Baada ya hapo IDM ilijikita kujenga viongozi katika utumishi wa Umma.

Kabla ya miaka ya mwanzoni ya 1980, dhana ya uongozi ilijengwa ndani ya misingi ya itikadi ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Mihimili yote mitatu ya Dola ilielekeza nguvu zake katika kujenga uongozi na viongozi watakaoifikisha jamii katika ndoto ya Ujamaa na Kujitegemea. Mifumo na taasisi zilianzishwa kukidhi matakwa haya. Kwa mfano, Chuo cha Kivukoni kilibadilika na kuwa Chuo cha Itikadi ya Chama Tawala cha TANU na baadaye CCM ya Ujamaa na Kujitegemea; mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (National Service) yalianzishwa kwa lengo la kujenga umoja na usawa kati ya jamii ya vijana Wa-Tanzania;  Sekretarieti ya Maadili (Ethics Secretariat) ilianzishwa kwa lengo la kujenga uadilifu na maadili mema katika Utumishi wa Umma na; Taasisi ya Kuzuia Rushwa (Anti-Corruption Squard) ilianzishwa ili kutiisha uaminifu kwa wananchi wote. Aidha, mifumo ya ajira, malipo na maendeleo ya Watumishi wa Umma, ilijengwa ndani ya itikadi ya Chama Tawala ya Ujamaa na Kujitegemea.

Mchakato wa kujenga uongozi na viongozi ulihusisha pia sekta binafsi na asasi zisizokuwa za umma, kama vile za kidini, tasnia ya burudani kama vile muziki na maonyesho, familia na jamii yote kwa ujumla. Kila mmoja kwa nafasi yake alishiriki katika kujenga uongozi na viongozi wenye mrengo wa kijamaa na kujitegemea.


Ndugu Washiriki;

Mabadiliko ya kiuchumi, kijamii na kisiasa yaliyofanyika katikati ya miaka ya 1980 yalileta athari kubwa kwenye mifumo ya kujenga uongozi na viongozi wa Taifa letu. Tafsiri ya Itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea ilibadilika, kutokana na kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa, na uchumi wa soko huria. Kwa bahati mbaya, swala la uongozi na namna gani viongozi waandaliwe kuongoza mabadiliko haya ya kiuchumi, kisiasa na kijamii haikupewa kipaumbele kama ilivyokuwa hapo awali. Aidha, mifumo na taasisi zilizokuwa zikiandaa viongozi zilibadilisha malengo na muelekeo wake. Kwa mfano, Taasisi ya IDM Mzumbe ilibadilishwa na kuwa Chuo Kikuu.  Chuo cha Kivukoni kiliporomoka na baadae kikabadilishwa na kuwa Chuo Kikuu, na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (national service) yalisitishwa.

Taasisi za sanaa kama vile za burudani, muziki na maonyesho zilibadilisha muelekeo; ziliacha ajenda ya kuandaa uongozi na viongozi wenye kubeba ajenda ya kitaifa. (Inawezekana pia hawakujua ajenda ya kitaifa ni ipi). Familia na jamii kwa ujumla zilijielekeza kuiga maisha na utamaduni wa nchi za magharibi. Hadi mwanzoni mwa miaka ya 2010 hakukuwepo na mfumo na taasisi iliyokuwa na ajenda bayana ya kuandaa uongozi na viongozi wa Tanzania tunayoitaka. Hali hii ilisababisha ombwe katika uandaaji wa uongozi na viongozi na hivyo kuhatarisha kufikia matarajio ya Taifa.

Ndugu Washiriki;

Serikali ililiona hili tatizo, na kuanzia mwaka 2010 ilianza kuchukua hatua madhubuti za kuendeleza uongozi na viongozi nchini. Taasisi ya UONGOZI ilianzishwa mwaka 2010 ikiwa na lengo la kuwajengea viongozi wa Kiafrika uwezo wa kufikia maendeleo endelevu kwa wananchi wake; Chuo cha Taifa cha Ulinzi (National Defence College) kilianzishwa mwaka 2012 kwa ajili ya kuwaandaa maafisa wa ngazi za juu Serikalini kushika majukumu ya kiuongozi ya kimkakati;  mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) yamerejeshwa kwa lengo la kujenga umoja, mshikamano na usawa miongoni mwa vijana wetu; taasisi za kujenga maadili ya uongozi na viongozi zimeimarishwa; n. k.

Ndugu Washiriki;

Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imedhamiria kwa dhati kuandaa na kuendeleza uongozi na viongozi nchini. Mifano michache inathibitisha dhamira hiyo. Hivi karibuni Mheshimiwa Rais ametangaza kuanzishwa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kinacholenga kujenga uongozi na viongozi   katika nchi zilizokuwa za mstari wa mbele katika ukombozi wa Bara la Afrika. Zaidi ya hayo, Serikali imeendelea kuimarisha nidhamu katika utendaji wa kazi, kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma, kujenga jamii yenye uadilifu na inayochukia rushwa. Aidha, Serikali imetengeneza Programu ya Maboresho Awamu ya Tatu ambayo sehemu kubwa inalenga kujenga mfumo wa kuandaa viongozi Serikalini. Jitihada hizi ni muhimu sana katika kuendeleza uongozi na viongozi wenye sifa chanya na zinahitaji kuungwa mkono na sisi sote. 

Ndugu Washiriki;

Kwa kumalizia, napenda niwapongeze tena wote kwa kuhudhuria kwa wingi kwenye kongamano hili muhimu lenye lengo la kujadili namna gani tunaweza tukajenga na kuendeleza uongozi na viongozi nchini. Uwepo wenu hapa unadhihirisha dhamira yenu katika kuisaidia Serikali kufikia lengo hili muhimu.

Aidha, ni matarajio yangu kuwa baada ya kongamano mtaweza kuibua mambo muhimu yatakayoiwezesha Serikali kuandaa na kujenga uongozi na viongozi wenye sifa za kuongoza jamii ya Watanzania ya hivi sasa na hata ile ya wakati ujao. Swali la msingi kwa washiriki wa kongamano ni: Je, ni mfumo upi na mkakati gani utaliwezesha Taifa kuandaa na kujenga uongozi na viongozi wa Taifa letu; kwa kuzingatia mazingira na mahitaji yetu, ya kanda na ya kimataifa?

Ndugu Washiriki;

Baada ya kusema haya, naomba sasa kutamka kuwa Kongamano hili limefunguliwa rasmi, na nawatakia ushiriki mwema.

ASANTENI KWA KUNISIKILIZA

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.