Skip to main content

ADB Banki yaipatia serikali kiasi cha shilingi Bilioni 486.516 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo


Benki ya Maendeleo Afrika (ADB) imeipatia Serikali ya Tanzania kiasi cha shilingi Bilioni 486.516 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Akizungumza mbele ya waandidishi wa Habari mwishoni mwa wiki wakati wa uwekaji saini wa hati ya makubaliano ya fedha hizo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Doto James, amesema mkopo huo ni wa mashariti nafuu ambao utarejeshwa ndani ya miaka 40.


Picha inayohusiana
“Mkopo huo uliombatana na msaada wa shilingi bilioni 45 zitakazo tumika katika bajeti ya maendeleo ya mwaka wa fedha 2018/19 ni matokeo ya utawala bora na uwajibikaji wakusimamia rasilimali fedha unaotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano,”amesema.

Vilevile James aliitaja miradi itakayo nufaika na fedha hizo kuwa ni mradi wa ujenzi wa Njia ya kusafirisha umeme wa msongo mkubwa (400Kv) kuanzia Nyakanazi hadi Kigoma, mradi wakudhibiti sumukuvu, na mradi wa  mpango wa kuendeleza utawala bora na maendeleo ya sekta binafsi nchini.
Kwa upande wake Mwakilishi Mkaazi wa Benki ya Maendeleo Afrika Alex Mubiru, alisema kuwa ADB imekuewa na mahusiano na Serikali ya Tanzania kwa mda mrefu, ni miongoni mwa nchi za kwanza kujiunga na Benki hiyo lakini alielezea pia uwezo wa Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
“Benki ya ADB imekuwa na mahusiano mazuri na Tanzania kuanzia mwaka 1962 ilipoamua kuwa mwanachama katika benki hiyo na imekuwa ikichangia michango yake kila mwaka,”amesema
Kutokana na uhusiano huo ADB imevutiwa na Tanzania na kuamua kuipa Tanzania msaada wa shilingi bilioni 45 bila marejesho yoyote na kuahidi kuwa itaendelea kuisadia Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mifugo Mali asili na Uvuvi  katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ahamad Haji alisema mkopo na msaada huo umekuja wakati muafaka nautasaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa pande zote mbili.
“Ni faraja kwetu kwakuwa mkopo na msaada huu utanufaisha pande zote mbili bara na visiwani ambapo umeme unatunufaisha wote japo ni huko Nyakanazi,  lakini udhibiti wa sumu kuvu unatuhusu moja kwa moja, fedha hizo zitajenga maghala ya kuhifadhia nafaka na kuboresha vituo vya utafiti na kilimo Unguja na Pemba,”amesema.
Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la umeme Tanzania Dk. Titus Mwinuka alisema kuwa kazi waliyo nayo mbele yao ni kuhakikisha mradi huo mkubwa wakufua umeme unakamilika kwa wakati.
“Kwa upande wetu wataalamu wamejipanga kuhakikisha mradi huu una kamilika nakuunganisha Mkoa wa Kigoma kwenye Gridi ya Taifa ambapo tokea nchi ipate Uhuru haijawahi kuunganishwa na gridi ya Taifa na badala yake yalikuwa yakitumika mafuta ya dizeli kuendesha mitambo ya uzalishajii umeme,”amesema.
Mradi huo wa ujenzi wa njia ya kusafirisha Umeme wa msongo mkubwa kutoka Nyakanazi hadi Kigoma wenye urefu wa kilometa  280 ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa serikali ya awamu ya tano ya kuwa na uchumi wa viwanda kwakujenga miundombinu wezeshi ikiwemo umeme wa uhakika kwa gharama nafuu.
Utekelezaji wa mradi huo utahusisha upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha Nyakanazi,ujenzi wa kituo kipya cha kupoza umeme cha Kidahwe na ununuzi wa vifaa vya uunganishaji wateja wapya wapatao 10,000 katika mkoa wa kigoma.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.