Trump asema hatasikiliza mkanda wa mauaji, amtetea bin Salman
Rais wa Marekani
Donald Trump amesema amejuzwa kuhusu mkanda wa sauti wa mauaji ya
mwanahabari Jamal Khashoggi lakini amesema binafsi hatousikiliza.
"Ni mkanda wa maumivu, ni mkanda mbaya," Trump ameiambia runinga ya Fox News.
Shirika
la ujasusi la Marekani CIA linaaminika kufikia kikomo kuwa mwanamfalme
Mohammed bin Salman aliamrisha kutekelezwa kwa maujai hayo, japo bado
Ikulu ya White House haijathibitisha uchunguzi huo.
Saudi Arabia imeziita taarifa hizo kuwa ni za uongo na kudai
kuwa bin Salman hakuwa na taarifa yoyote juu ya kutekelezwa kwa mkasa
huo.
Khashoggi, alikuwa ni kinara wa kuukosoa utawala wa kifalme
wa Saudia. Aliuawa ndani ya ubalozi mdogo wa Saudia jijini Istanbul
Oktoba 2 alipoenda kuchukua karatasi zake za talaka.
Saudia inasema aliuawa katika operesheni haramu iliyotekelezwa na maafisa wake wa usalama.
Hata
wanaomuunga mkono Trump ndani ya Bunge la Wawakilishi wanamtaka achukue
hatua kali juu ya mauaji hayo. Lakini kutokana na unyeti wa Saudia kama
mshirika thabiti wa Marekani katika Mashariki ya Kati kunamfanya Trump
kuwa mgumu katika kufanya maamuzi. Mwanamfalme wa Saudia aliamini 'Khashoggi alikuwa hatari'
Trump amesema hana haja ya kusikiliza sababu ameshaelezwa juu ya maudhui ya mkanda huo.
"Ninafahamu
kila kitu kilichomo ndani ya mkanda bila hata ya kuusikiliza,"
aliiambia Fox katika mahojiano yaliyorushwa jana Jumapili Novemba 18.
"Iikuwa ni vurumai, uovu mkubwa na mbaya sana."
Katika mahojiano hayo, Tump amesema Mohammed bin
Salman amemwambia kuwa alikuwa hajui lolote juu ya mpango na kutekelezwa
kwa mauaji hayo.
Trump amedai kuwa yawezekana isijulikane kabisa
nani alikuwa nyuma ya mauaji hayo, hata hivyo amesema tayari kuna
vikwazo vimeshawekwa juu ya wale wanaoshukiwa kutekelza uovu huo.
"Lakini
wakati huo huo tunaye mshirika na mimi nataka nishikamane na mshirika
ambaye kwa namna nyingi tu amekuwa mwema," amesema Trump.
Hata hivyo, mahojiano ya Trump na Fox yalifanyika kabla ya kuvuja kwa ripoti ya CIA.
Japo CIA hawakutoa ushahidi wa moja kwa moja juu ya
uhusika wa bin Salman to the murder, maofisa wa shirika hilo wanaamini
tukio kama hilo lisingeweza kufanyika bila ruhusa yake.
Jumamosi,
wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema haijafikia hitimisho juu ya
mauaji hayo, ikisema kuna maswali mengi ambayo hayajapata majibu.
Jana Jumapili Trump amesema serikali yake lazima ifanye maamuzi.
"Tutakuwa na ripoti kamili ndani ya siku mbili, yawezekana Jumatatu au Jumanne," amesema Trump. Kwa msaada wa BBC Swahili.
By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo. -WANANCHI WATAKA IPUNGUZE UKALI WA MAISHA MACHO na masikio ya mamilioni ya Watanzania na wadau wa nje, leo yanaelekezwa Dodoma ambako Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/12 itasomwa.Wananchi wengi wamekuwa na shauku ya kujua mwelekeo wa bajeti hiyo hasa katika kipindi hiki ambacho wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha iliyotokana na kupanda kwa bei vyakula na bidhaa za mafuta. Kwa takriban wiki nzima iliyopita, baadhi ya wananchi wamekuwa wakituma ujumbe mfupi wa maandishi kwa simu katika vyombo vya habari, wakiisihi serikali kuhakikisha kuwa bajeti ya mwaka huu inawaondoa katika hali ngumu ya maisha. Bajeti hiyo itakayosomwa bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo itatangazwa kwa wakati mmoja na bajeti za serikali za nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), katika mtazamo wa kuimarisha mshimakano na umoja wa nchi hizo. Kwa kawaida na mazoea ya muda mrefu, baj...
Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...
Comments