MKUU
wa ujumbe wa uangalizi kutoka Muungano wa Afrika nchini Zimbabwe,
Olusegun Obasanjo amesema uchaguzi mkuu wa hapo Jumatano ulikua huru na
haki. Matokeo ya awali yanaoyesha Rais Robert Mugabe na chama tawala cha
Zanu PF wakiongoza kwa kura nyingi
Chama hicho tayari kimedai ushindi.
Msemaji wa chama hicho Rugare Gumbo alisema chama hicho kilitarajiwa
kushinda kiasi ya asilimia 70 ya kura hizo. (HM)
Comments