Skip to main content

CHEKA KAUTWAA UBINGWA WA DUNIA

HABARI/PICHA na bongostaz.blogspot.com
BONDIA Mtanzania, Francis ‘SMG’ Cheka usiku wa kuamkia leo ametawazwa kuwa bingwa mpya wa dunia wa WBF, katika uzito wa Super Middle baada ya kumshinda Mmarekani, Phil Williams kwa pointi katika pambano la Raundi 12, lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Jaji wa kwanza Eddie Marshall kutoka Afrika Kusini alitoa pointi 116 kwa 115, jaji wa pili Fidel Hayness alitoa pointi 119 kwa 118 na jaji wa tatu, John Chagu alitoa pointi 117 kwa 116 (wote wa Tanzania), wakimpa ushindi Cheka.
Kwa ushindi huo, Cheka amefuata nyayo za bondia mwingine Mtanzania, Rodgers ‘Tiger’ Mtagwa ambaye aliwapiga Wamarekani kadhaa kwao, ambako anaishi tangu 1998.
Bondia Francis Cheka wa Tanzania akimtupia konde Mmarekani, Phil Williams katika pambano la Raundi 12 kuwania ubingwa wa dunia uzito wa Super Middle usiku huu ukumbi wa Diamond Jubilee kuwania taji la WBF. Cheka ameshinda kwa pointi.
Thomas Mashali kulia ameshinda kwa pointi dhidi ya Mada Maugo

Miongoni mwa mabondia Wamarekani ambao Mtagwa, mtoto wa Keko Mwanga, Temeke, Dar es Salaam amewahi kuwapiga ni Garvin Crout kwa Knockout (KO) Raundi ya kwanza pambano la Raundi nane, kwenye ukumbi wa Blue Horizon, Philadelphia, Pennsylvania, Marekani pambano lililochezeshwa na refa James Condon Septemba 12, mwaka 2000 na mwingine Donovan Carey kwa KO pia Raundi ya Pili Juni 15, 2001 ukumbi huo huo.
Katika pambano hilo lililochezeshwa na refa kutoka Afrika Kusini, Drake Ribbinck, mabondia hao walianza kwa kusomana Raundi ya kwanza wakitupiana makonde ya tahadhari na katika Raundi ya pili, kila mmoja alitaka kuhakikisha kile alichogundua kwa mpinzani wake kabla ya kazi kuanza Raundi ya Tatu.
Cheka aling’ara katika Raundi ya Tatu na ya nne na Mmarekani akaibuka Raundi ya Tano na kuanza kuonyesha upinzani. Raundi ya Sita Mmarekani aliongeza kasi ya urushaji makonde na Raundi ya saba na ya nane walipigana sawa, ingawa Williams alianguka kwa kuteleza na kuinuka kuendelea na pambano.
Raundi ya 10 mabondia hao waliendelea kutupiana makonde kwa zamu, lakini Raundi ya 11 na 12 pamoja na Williams kusimama imara kutafuta ushindi wa Knockout (KO), lakini SMG alikuwa makini katika kukwepa na kurusha ngumi za kudonoa kichwani kwa mpinzani wake.
Na kwa sababu hiyo haikushangaza baada ya pambano, bondia mwenye maskani yake Morogoro kutangazwa bingwa mpya wa WBF.
Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara aliyekuwa mgeni rasmi alijaribu kwa tabu tabu kumvisha taji Cheka kutokana ulingo kuvamiwa na mashabiki waliopagawa na ushindi wa bondia huyo.
Katika mapambano ya utangulizi, Thomas Mashali alimshinda kwa pointi Mada Maugo, wakati Alphonce Mchumia Tumbo alimshinda kwa Technincal Knockout (TKO), baada ya wasaidizi wake kurusha taulo Raundi ya tano katika pambano la Raundi sita.
Hata hivyo, dosari  iliyojitokeza katika usiku huo ni mabondia kugoma kupanda ulingoni hadi kwanza walipwe fedha zao na ilianzia kwa Mchumia Tumbo, ikafuatia kwa Maugo na Mashali na baadaye Cheka.
Bingwa wa zamani wa dunia, bondia wa Afrika Kusini, Francois Botha alilaani hali hiyo na kusema mabondia wanapanda ulingoni kwa ajili ya fedha, hivyo kutokokuwa na uhakika wa malipo yao si sawa.
Alipoulizwa kuhusu malipo yake, Botha aliyewahi kupigwa kwa mbinde na bingwa wa zamani wa dunia, Mmarekani, Mike Tyson alisema yeye amekuja kwa mradi maalum wa kampeni kuzuia Malaria na hana anachodai kwa waandaaji wa pambano hilo.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.