Skip to main content

MADHARA YA VIATU VYA MCHUCHUMIO NA AFYA YA WANAWAKE

074 4d2e7
Nipo nazunguka zunguka madukani, ghafla wanawake wawili vijana wa Kizungu wamenisimamisha. Huu ni msimu wa Kiangazi Ulaya; wamevalia vijisuruali vifupi, vilivyoishia magotini; nadhani nyumbani vinaitwa vipedo. (HM)

Juu ya hivyo vipedo wamejiremba vijifulana vifupi visivyoficha mabega, matumbo wazi; vitovu nje. Siyo ajabu kuona asilimia kubwa ya wakazi bara hili miezi hii wakivalia ndala na kwenda nusu uchi; wanaume kwa wanawake.
Wasioonyesha miili kiasi kile ni wanawake wa Kiislamu na Wayahudi wanaofuata pia kanuni za kusitiri mwili. Kwa kanuni za Waislamu kinachoruhusiwa kuonekana mwili wa mwanamke ni viganja vya mikono na nyuso tu.
Lakini sivyo kwa wengi majuu, kutokana na majira nyanda za kaskazi ya dunia kuwa baridi, mvua ya manyunyu na ukungu robo tatu ya mwaka. Ulimwengu ni kama umekunja ndita kwa hasira.
Lakini tangu mwezi uliopita mambo ahueni. Kwa Mzungu kuwaka jua kali ni jambo adimu sana; lina Vitamin D inayotupa wanadamu furaha na kuijaza ngozi na hisia.
Ukosefu huu wa jua huwafanya wananchi wengi nchi za baridi kukosa raha hata wakaugua. Ugonjwa huwa mkubwa kiasi cha kuwalazimu kwenda kwa daktari kuandikiwa dawa ya furaha (anti-depressants). Ndiyo maana usishangae kuwaona ndugu zetu weupe wanapoitembelea Afrika wakajianika (sana) juani.
Kwa Mwafrika kukaa juani (kuliota) baada ya saa tatu asubuhi siyo kawaida, labda uwe mgonjwa wa homa.
Vilevile wanavyolala juani ni jitihada ya kuibadili rangi ya ngozi hizi za mseto wa weupe na wekundu hafifu walau uwe na kikahawia.
Kijiografia, ulimwengu wetu huu wenye wanadamu bilioni moja, unaathiriwa na hali tofauti za hewa. Wapo wanaousumbuliwa na vimbunga na matufani. Miezi hii Visiwa vya Karibian na Marekani, wasioona mwangaza kwa siku sitini uwanda wa kaskazini, Atikiti (Greenland, Finland, Norway, Canada, au walio mazingira ya ukame na mchanga, Jangwa Kalahari, Gobi hata Sahara.
Sasa kina dada wamenisimamisha.
"Samahani wee mkazi eneo hili?" "Ndiyo!"
"Tumepotea kidogo. Unaweza kutuelekeza tafadhali?"
Wanatafuta kituo cha tiba ya miguu. Mmoja anachechemea. Biashara ya tiba ya miguu ni kubwa sana majuu.
Kati ya maradhi yanayoangaliwa ni Funza wa Kuvu ("fungus")anayeishi sehemu watu wanapotembea peku peku kama penye madimbwi ya kuogelea kitaalamu anaitwa Virucca. Virucca akishaganda unyayoni ni kazi sana kumtoa.
Mganga wake anaitwa Chiropodist au Podiatrist,elimu yenyewe inaitwa "Chiropody" au "Podiatry" na hutoza Sh1 milioni au zaidi kumwondoa funza huyo, hapa London.
Tatizo jingine ni uvimbe unaotokea kwenye kidole gumba na kile kidogo, mguuni. Uvimbe huu wa mfupa unaoitwa "bunion" kwa Kiingereza huwaathiri zaidi wanawake kutokana na viatu vya kubana bana. Baadhi ya wanaume pia huupata.
Ili kusawazisha inabidi ufanywe upasuaji unaorekebisha mfupa wa kidole na hilo huchukua siyo chini ya miezi tisa kupona kabisa.
Wakati nikiwaelekeza hawa kina dada, ninamwona mmoja akimwegemea mwenzie.
"Vipi umeumia ?"
"Ah, udhia mtupu. Miguu yangu imekwisha."
"Kwa vipi?"
"Viatu vya mchuchumio."
Wanacheka, mchanganyiko wa dhihaka na kero. Hivi karibuni, utafiti uliofanywa hapa Uingereza umegundua kuwa asilimia 90 ya wanawake wameshapatwa na maumivu ya miguu, magoti au mgongo kutokana na viatu vyenye urefu wa sentimeta 10 hadi 15, vinavyoitwa "high heels" kwa Kimombo.
Wanawake waliohojiwa katika utafiti walikiri wanajua kama wavuta sigara walivyo, kuwa siyo vizuri kuvaa viatu vya mchuchumio, lakini huendelea tu kuvivaa. Utafiti huu uliotangazwa ndani ya majarida ya mavazi na urembo ulisema, mjini New York, mathalan, viatu virefu aina ya Stilleto vinavyovutia macho na kupendeza, vinajeruhi wanawake kutokana na siyo urefu wake tu.
Mmoja wa watengenezaji wa viatu hivyo alikiri hulipwa fedha nyingi kutoa madarasa kwa wanawake husika namna ya kuvitembelea. Anasema mbali na urefu wa viatu hivyo, tatizo ni kutojua kuvitumia.
Uchunguzi mwingine uliofanywa Australia umetanabahi namna ajali nyingi za kuanguka, majeruhi na maumivu zinavyowaathiri wanawake wanaofanya kazi za umaarufu mfano utangazaji TV na ubunifu mavazi.
Uchunguzi ulibaini muda kuwa maumivu hupoanza baada saa moja na dakika saba.
"Mwanamke husikia maumivu kiasi ambacho huamua kuviondoa na kurudi nyumbani peku peku." Tatizo linatokana na wanawake hasa vijana, kudhani wanavutia zaidi kihaiba kuliko wakiwa na viatu vifupi.
Miaka ile nilipoishi Brazili kulikuwa na misemo iliyowagawanya wanawake mafungu mawili. Mosi ni wale waliovalia mavazi ya kubana bana, wadogo wadogo, mviringo mviringo, umbo la herufi nane. Mwanamke aliyedondokea daraja hili aliitwa "gitaa".... ( kwa Kireno "violão").
Wa pili uliwahusu kina dada warefu kiasi, wenye nywele ndefu waliotembea haraka na viatu vya mchuchumio. Waliitwa "ndege abiria"- eropleni Kiswahili- (Kireno "avião") ikiwa na maana mwanamke aliyependeza kutokana na viatu hivi virefu.
Maelezo ya kitaswira kama haya huathiri zaidi wanawake, maana wanapopita mitaani hutazamwa na kuwekwa katika mafungu na matabaka; huandamwa na mipangilio ya kuvaa, kutembea na kadhalika. Mengi yanayomwekea masharti ya urembo na wajihi, pia ni adha kwake.
Mfano ni mtindo ulioenea hii leo kwa wanawake weusi kuvaa nywele za bandia au kuzichoma zilainike. Mtindo huu umehodhiwa na wanawake weusi maarufu kama mkewe Rais Obama (Michelle), mwimbaji Beyonce na mtangazaji tajiri wa runinga, Oprah Winfrey.
Matokeo wanawake wanapofikisha miaka 40, siku hizi hata mapema zaidi nywele hudondoka, wanageuka vipara kutokana na dawa zilizomo ndani ya ghasia zinazotumika. Nyingine ni matumizi yasiyo sahihi ya sidiria.
Wanawake wangapi wanafahamu saizi inayotakiwa kwa matiti yao? Je, utumiaji sidiria unawezaje kuathiri haiba na afya ya kiungo hicho?
Kwa nini wanawake vijana sana siku hizi tayari wanafikiwa na tatizo la "malapa" (kuanguka matiti)?
Hii ni baadhi ya mifano; lakini tatizo la viatu vya mchuchumio siyo mchezo.
Licha ya kuhatarisha miguu, mgongo na magoti, linaweza kumfanya mwanamke ashindwe kabisa kutembea anapofikia uzeeni.
Suluhisho ni kuchagua viatu vinavyopendeza, lakini havikongi au kuchakaza mwili kiasi hicho.
Uchaguzi huo ni wa mwanamke mwenyewe kujua linalomfaa na lisilomfaa. Si vyema haiba na afya vikakinzana. Chanzo: www.freddymacha.com

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.