Skip to main content

Vyuo vikuu wampigia Makamba debe la urais..;

makamba_cd43e.jpg
Waazimia kuunda timu ambayo itamshawishi January Makamba kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Morogoro. Viongozi wa Vyuo Vikuu 21 nchini wameazimia kwa kauli moja kuunda timu ndogo itakayokwenda kumshawishi Mbunge wa Bumbuli na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe tawi la Mbeya, Theonest Theophil alisema hilo ni moja ya maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wa siku mbili na kuwashirikisha marais, makamu wa rais, mawaziri wakuu na maspika wa vyuo 21 nchini.


Theophil alisema mkutano huo uliyapigia kura majina matatu yakiwamo ya wabunge wengine wawili vijana; John Mnyika na Zitto Kabwe na kwamba Makamba alipitishwa kuwa chaguo lao baada ya kupata kura 70 kati ya 105 zilizopigwa. Alisema Zitto alipata kura 20 na Mnyika kura tisa, huku kura tisa zikiharibika.
Alisema viongozi hao wamepanga kutembea nchi nzima na kuwashawishi Watanzania kumuunga mkono Makamba endapo ataafiki kuwania nafasi hiyo ya urais, huku wakidai kwamba wamechoshwa na viongozi wenye visasi na uadui ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kulumbana na kupambana badala ya kuwatumikia wananchi.
Theophil alisema mkutano huo ulilenga kujadili mustakabali wa nchi katika masuala ya ubora wa elimu na vihatarishi vya amani ambavyo vinatokana na chuki za kidini, siasa na visasi. Pia walijadili tatizo la ajira kwa vijana, ukuaji wa uchumi na mchakato wa Katiba Mpya ambao alisema hivi sasa ni kama umetekwa na ushabiki wa kisiasa.
Theophili alisema walibaini kwamba ili kukabiliana na changamoto zilizopo lazima nchi iwe na uongozi thabiti, hivyo walimchagua Makamba kama mmoja wa viongozi wenye sifa za kushika wadhifa wa urais kwa kuzingatia sifa alizonazo.
Alizitaja baadhi kuwa ni kuonyesha uwezo na ujasiri katika nafasi za uongozi alizowahi kushika na uadilifu, kwani hajawahi kuhusishwa na vitendo vya rushwa na ufisadi katika uongozi wake.
Kwa upande wake, Said Ngolola kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alisema tatizo la mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu limekuwa likiathiri mfumo wa elimu ya juu nchini, kutokana na kushindwa kwa waliopewa dhamana ya kusimamia suala hilo hali ambayo imekuwa ikileta migogoro isiyoisha..
Mkutano wa viongozi hao uliandaliwa na kufadhiliwa na asasi isiyokuwa ya kiserikali ya FPID inayojihusisha na mapambano dhidi ya maradhi, ujinga na umaskini yenye makao yake makuu Dar es Salaam.
Katibu wa asasi hiyo, Frances Ndunguru alisema asasi hiyo haina uhusiano wowote na wanasiasa, bali lengo ni kuwezesha makundi mbalimbali ya kijamii kukutana na kujadili masuala yenye masilahi kwa nchi.
CHANZO: mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...