Skip to main content

DIMBA LA TAIFA YANGAYAICHAPA AZAM 1-0 JANA



MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, Yanga jana  wameonyesha nia yao ya kutetea taji hilo msimu ujao baada ya kuichapa Azam bao 1-0 katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo huchezwa kila mwaka kabla ya kuanza kwa ligi kuu, ikizikutanisha bingwa wa ligi ya msimu uliopita na mshindi wa pili.

Kipigo hicho kilikuwa ni mwendelezo wa ubabe wa Yanga kwa Azam baada ya msimu uliopita kushinda mechi zote mbili za ligi kuu. Katika mechi ya kwanza, Yanga ilishinda mabao 2-0 na katika mechi ya pili ilishinda bao 1-0.

Kiungo Salum Telela aliibuka shujaa wa Yanga baada ya kuifungia bao hilo la pekee na la ushindi dakika ya pili baada ya kupokea pasi kutoka kwa Didier Kavumbagu.

Yanga ilipata pigo dakika ya 11 baada ya beki wake kisiki, Kevin Yondani kuumia kufuatia kugongana na mshambuliaji John Bocco wa Azam. Beki huyo wa zamani wa Simba alitibiwa kwa dakika kadhaa, lakini alishindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikachukuliwa na Mbuyu Twite.

Yanga ilipata pigo jingine dakika ya 11 baada ya kipa wake, Ally Mustapha Barthez kuumia kufuatia kugongana na Kipre Tchetche wa Azam alipokuwa katika harakati za kuzuia mashambulizi kwenye lango lake. Nafasi yake ilichukuliwa na Deo Munishi 'Dida'

Yanga SC: Ally Mustafa ‘Barthez’/Deo Munishi ‘Dida’ , Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan/Mbuyu Twite, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Salum Telela, Jerry Tegete/Hussein Javu, Didier Kavumbangu na Haruna Niyonzima.

Azam FC; Aishi Manula, Erasto Nyoni/Joackins Atudo, Waziri Salum, David Mwantika, Aggrey Morris, Himid Mao, Kipre Tchetche, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, John Bocco ‘Adebayor’/Gaudence Mwaikimba , Kipre Balou/Ibrahim Mwaipopo na Khamis Mcha.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...