Skip to main content

Serikali yatoa idadi ya wakimbizi walioondoka na, “Operesheni itaanza ghafla”


Imeandikwa na Magreth Kinabo — SERIKALI imesema kwamba operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu katika Kanda ya Ziwa itaanza kwa ghafla, huku ikiendelea kusisitiza kwamba watu wanoaishi nchini bila taratibu za kisheria kuondoka kwa hiari na mali zao.
Picture
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu wahamiaji haramu waliorejea kwao baada ya agizo la Rais Jakaya Kiwete alilolitoa Julai 29, mwaka huu katika ziara yake ya mkoa wa Kagera. (Picha na Lorietha Laurence)
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahamiaji haramu waliorejea kwao baada ya agizo la Rais Jakaya Kiwete alilolitoa Julai 29, mwaka huu katika ziara yake ya mkoa wa Kagera.
“Nimeshapewa maelekezo rasmi na Rais Jakaya Kikwete ya kuwaondoa wahamiaji haramu nitakapoona inafaa. Operesheni itaanza ghafla haiko mbali.

Muda mwuafaka wa kutekeleza vyombo vya dola vitasema. Tunatoa wito waondoke wenyewe na mali zao bila kunyang’nywa. Wenye mali nyingi wanatakiwa kutoa taarifa katika vituo vya polisi ili waweze kusindikizwa. Hatutawavumilia wahamiaji haramu,” alisema Waziri Nchimbi.
Aliongeza kuwa wahamiaji hao wanaotaka kuishi nchini wanatakiwa kurudi nchini kwao kwanza na kufuata taratibu za kisheria kama ambavyo nchi nyingine zinavyofanya mtu akitaka kuishi nchi yoyote anatakiwa kufuata taratibu hizo.

Comments