Skip to main content

Wabunge wataka uwazi mali za viongozi

Na Mwandishi wetu
KAMATI za Bunge zinazosimamia fedha za umma zimeazimia kuwa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma haiweki uwazi wa kutangaza umiliki wa mali za viongozi.
Hali hiyo inasababisha viongozi kutoweka wazi mali wanazozimiliki na ni rahisi mtu kuzushiwa umiliki usio wa kweli.
Katika maazimio yao 22 yaliyofikiwa siku ya mwisho wa mafunzo, juzi, kamati hizo za Hesabu za Serikali (PAC), Serika za Mitaa (LAAC) na ile ya Bajeti zimependekeza kuwa ni vema sekretarieti ikafanya utafiti wa umiliki wa mali kwa viongozi wa umma na kuweka taarifa hizo katika tovuti yake.
Lengo la kufanya hivyo ni kuwawezesha wananchi kuziona mali zinazomilikiwa na viongozi wao na pale ambapo kiongozi hatakuwa ametoa taarifa ya umiliki huo basi taarifa hiyo itolewe kwa tume.
Katika maazimio mengine kamati zimekubaliana kuwa kutokana na kutokuwepo na taarifa sahihi kuhusu deni la taifa, kuna umuhimu wa kuwakutanisha wadau wakuu wanaohusika hususan Benki Kuu (BoT), Hazina, Kamati za Bunge na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG).
Hatua hiyo itawawezesha kujua kwa usahihi zaidi ukubwa wa deni hilo. Vilevile imeamuliwa kuwa serikali ishauriwe kuunda chombo huru kitakachosimamia deni la taifa.

“Kamati za Bunge zinazoshughulikia usimamizi wa fedha na rasilimali za taifa zishughulikie zaidi maafisa masuuli hatarishi (risk based) ili kuleta thamani ya fedha katika utendaji wao. Kamati zishirikiane na CAG katika kuamua ni afisa masuuli yupi aitwe kukutana na Kamati,” walisema.

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge na Tamisemi imetakiwa kuanzisha utaratibu wa kuratibu mikutano na mafunzo ya wakurugenzi wa halmashauri kwa pamoja kuliko kila wizara kuwaita watendaji hao katika sehemu mbalimbali kwa muda tofauti na kuwafanya kutokuwepo ofisini kwa kipindi kirefu.
“Taarifa za mwaka za Kamati za Bunge ziwe na kipengele cha kiwango cha utekelezaji wa mapendekezo ya kamati yaliyotolewa awali. Kamati ziwezeshwe kifedha ili ziweze kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo yao.
“Kanuni za Bunge zieleze utaratibu wa ufuatiliaji wa maazimio ya Bunge na namna utekelezaji wake utavyowasilishwa bungeni. Vilevile Bunge litenge siku ya kuijadili serikali ilivyoshughulikia hoja za kamati za Bunge. Spika ashauriwe kuhusu umuhimu wa kuunda kamati ya Bunge ya kufuatilia ahadi za serikali,” alisema mjumbe mmoja na kuungwa mkono na wenzake.
Serikali iandae mjadala wa kitaifa wa kutafuta ufumbuzi wa kukabiliana na vitendo vya rushwa na mmomonyoko wa maadili vinavyoongezeka kwa kasi hapa nchini.
Vilevile viongozi wa umma na watendaji waongoze kwa mfano kwa kutojihusisha na vitendo vya rushwa katika kutekeleza majukumu yao.
“Sheria ya “Anti Money Laundering” ya 2006 irekebishwe ili iweke viwango vya fedha ambavyo mtu anaweza kuingia au kutoka nazo nchini bila kuziweka wazi. Kuna umuhimu wa Waziri wa Fedha kutengeneza kanuni za kutekeleza sheria hiyo.
“Benki Kuu iandae mfumo thabiti wa usimamizi wa maduka ya fedha na kuhakikisha kutungwa kwa sheria inayozuia matumizi ya fedha za kigeni katika shughuli za kibiashara hapa nchini,” alisema mjumbe akiungwa mkono na wenzake.
Chanzo - Tanzania daima

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.