Skip to main content

Leiwing: kapombe anapoteza muda as Cannes, hapaswi kucheza daraja la nne

kapombe 5f8a6
KIRAKA wa Tanzania, Shomari Kapombe ametambulishwa juzi Ahamisi kwenye mazoezi ya klabu ya AS Cannes ya Ufaransa, lakini Kocha Mfaransa aliyetimuliwa Simba, Patrick Liewig amesema timu hiyo haina hadhi ya Kapombe.
Hata hivyo, Simba imemjibu Liewig kuwa asiwe na wasiwasi kwani tayari Kapombe anatakiwa na timu ya daraja la pili ya Ufaransa.
Liewig aliiambia Mwanaspoti kwa simu kutoka jijini Paris, Ufaransa jana Ijumaa kwamba klabu hiyo ya daraja la nne ni ya hadhi ya chini sana kulinganisha na ubora wa Kapombe ambaye alipaswa kuchezea madaraja ya juu hivyo Simba imempeleka sehemu anakokwenda kupoteza muda wake.
Liewig alisema; "Naijua Cannes ni timu ndogo sana, inashiriki daraja la nne ni ya chini sana kulinganisha na ubora wa Kapombe niliyemfundisha hapo Simba. Yeye hadhi yake ni daraja la kwanza au la pili, na zipo klabu nyingi tu ambazo angeweza kupata nafasi."
"Simba na huyo wakala wanampotezea Kapombe muda wake, wachezaji wakubwa wa Tanzania wanapaswa kukaa chini na kujipanga. Klabu zikae na watu wa maana zifanye mambo kwa kufuata weledi, mimi najuana na watu wengi sana kuanzia makocha na viongozi ambao naweza kuwaunganishia wachezaji wa Tanzania na wakacheza soka daraja la kwanza.
"Mchezaji mwenyewe ajipange anifuate aonyeshe nia ya kweli mimi nitashirikiana na viongozi nitamsaidia, lakini huko alikokwenda Kapombe sijapaafiki," alisisitiza kocha huyo ambaye bado hajapata dili mpya.
Katika klabu hiyo, Kapombe atajumuika na 'Waswahili' wanne kutoka Burundi, Uganda, Senegal na Togo.
Kapombe atakuwa katika klabu hiyo na iwapo atauzwa ndio Simba itapata mgawo wake.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Usajili wa Simba, Zacharia Hanspoppe aliliambia Mwanaspoti jana Ijumaa kuwa hawana wasiwasi na suala hilo kwani tayari Kapombe ameivutia timu ya daraja la pili.
"Sisi tunajiamini na mambo tunayoyafanya, hapo nazungumza na wewe nilikuwa napata mawasiliano kutoka Ufaransa kuwa kuna timu ya daraja la pili inamhitaji Kapombe. Hao AS Cannes wakimuuza Kapombe sisi tunapata asilimia 40," alisema Hanspoppe. Chanzo: mwanaspoti

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them ...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Mwana muziki Marufu kwa jina la Chuck Brown Afariki Dunia Akiwa na umri wa miaka 75

View Photo Gallery — Chuck Brown dies at 75: The “godfather of go-go” has died By Chris Richards, Updated: Wednesday, May 16, 4:42 PM Chuck Brown, the gravelly voiced bandleader who capitalized on funk’s percussive pulse to create go-go, the genre of music that has soundtracked life in black Washington for more than three decades, died May 16 at the Johns Hopkins University hospital in Baltimore. He was 75. The death, from complications from sepsis, was confirmed by his manager, Tom Goldfogle. Mr. Brown had been hospitalized for pneumonia. Known as the “Godfather of Go-Go,” the performer, singer, guitarist and songwriter developed his commanding brand of funk in the mid-1970s to compete with the dominance of disco. Like a DJ blending records, Mr. Brown used nonstop percussion to stitch songs together and keep the crowd on the dance floor, resulting in marathon performances that went deep into the night. Mr. Brown said the style got its name because “the music j...