Skip to main content

Mchuano wa kiti cha urais Mali katika duru ya pili


Wagombea wa kiti cha urais nchini Mali wamesema wana matumaini ya kushinda duru hiyo ya pili ya uchaguzi wa rais huku kampeni zake zikikamilika Ijumaa ya jana.
Ibrahim Boubacar Keita Waziri Mkuu wa zamani wa Mali aliypata karibu asilimia 40 ya kura zilizopigwa na Soumaila Cisse Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo alipepata asilimia 19.4 katika duru ya kwanza ya uchaguzi huo watachuana tena katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa Mali uliopangwa kufanyika kesho Jumapili, baada ya mahasimu hao kushindwa kupata kura zinazohitajika katika duru ya kwanza. 
Keita ambaye alimshinda Cisse kwa zaidi ya asilimia 20 katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa rais amesema ana matumaini ya kushinda uchaguzi wa kesho kwa kuzingatia matokeo hayo ya hapo awali. 
Ibrahim Boubacar Keita ameongeza kuwa, kipaumbele chake cha kwanza kitakuwa ni mapatano ya kitaifa baada ya nchi hiyo kukumbuwa na mgogoro na kwamba mwanzo mpya unahitajika huko Mali.
Naye Soumaila Cisse amesema kuwa ana matumaini ya kushinda duru ya pili ya uchaguzi wa rais hapo kesho akisema kuwa na hapa ninamnukuu" uchaguzi wa kesho si suala la kuongezea kura zilizopatikana katika duru ya kwanza, bali ni kuwa kutakuwa na kura mpya na kwamba huo ni uchaguzi mpya," mwisho wa kumnukuu.Inatoka kwa mdau.

Comments