Makamu wa Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, jana alikuwa mmojawapo wa wageni mashuhuri katika sherehe za
kumuapisha Rais wa mpya wa Jamhuri ya Kiislamu ya Watu wa Iran
Mheshimiwa Hassan Rouhani, sherehe iliyofanyika katika makao makuu ya
nchi hiyo yaliyopo jijini Tehran.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Rais Mstaafu wa
Jamhuri ya Kiislam ya IRAN Mhe. Al-Akbar Hashemi Rafsanjani
Kabla ya sherehe hiyo ya kuapishwa, Jumamosi Agosti 4, 2013, Mkuu wa
Kidini wa nchi hiyo Ayatollah Ali Khamenei alimthibitisha Rais Rouhani
na akatumia nafasi hiyo kufafanua kuhusu aina ya mahusianio ambayo Iran
inataka kuyaona baina yake na nchi zingine duniani.
| Dk. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Kiislam ya IRAN Mhe. Al-Akbar Hashemi Rafsanjani |
Mheshimiwa Makamu wa Rais alikuwa miongoni mwa viongozi wapatao 55
kutoka nchi mbalimbali walioshiriki sherehe hizi huku vyombo vya habari
kutokana nchini Iran vikielezea kuwa tukio la jana kwamba ni la
kihistoria kwani Iran haikuwahi kuwa na wageni mashuhuri wengi kiasi
hicho katika sherehe zake za kuapisha viongozi wa nchi hiyo.
Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Rais aliyemaliza muda wake, Rais Mahmoud Ahmadinejad.
Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na Rais aliyemaliza muda wake, Rais Mahmoud Ahmadinejad.
Akihutubia wananchi wa Iran sambamba na wafutiliaji wa siasa za Iran
mara tu baada ya kuapishwa, Rais Rouhani alisema Iran inategemea kuwa
nchi za ulimwengu wa kwanza zitatafuta suluhu nayo kwa mazungumzo na
siyo kwa kutumia vikwazo.
Kauli hii alikuwa anaitoa siku moja baada ya seneti ya Marekani
kupitisha kwa azimio moja vikwazo zaidi kwa Iran saa chache kabla ya
Rais Rouhani kuthibitishwa na Ayatollah Khamenei, Kiongozi mkubwa kabisa
na mwenye heshima ya juu katika Iran.
Comments