Skip to main content

WIZI WA WA ATM WATIKISA NCHINI


Na: Frederick Katulanda, Mwanza- Mwananchi
JESHI la Polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB imewatia mbaroni watu watatu ambao wanadaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti. Watuhumiwa hao wamenaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki na polisi kwenye saa 6.00 usiku wa Februari 10, mwaka huu na mtuhumiwa mmoja alibambwa akichukua fedha katika ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza Mwanza. Baada ya kunaswa kwa mtuhumiwa huyo,
alisaidia kuwaelekeza polisi walipo wenzake, ambao walikutwa katika hoteli moja jijini Mwanza wakiwa wamejipumzisha. Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mwanza, Christopher Fuime alisema pia walikamata vifaa mbalimbali ambavyo walikuwa wakitumia kwa ajili ya kufanyia uhalifu huo.

“Kwa muda mrefu sasa Jeshi letu lilikuwa likihangaika na wahalifu wa aina hiyo kwani tangu Oktoba 2012 tumekuwa tukipokea kesi mbalimbali za wizi wa fedha katika akaunti zao, lakini tumefurahi tumewatia mbaroni,” alieleza Fuime.
Kamanda Fuime alidai kuwa tangu kutiwa mbaroni kwa watuhumiwa hao, hawajasikia malalamiko ya wizi tena.

Alisema polisi walikuwa wakipata wastani wa malalamiko 15 katika kipindi cha siku 14.
“Hawa jamaa inaelekea ndiyo vinara wa wizi huu, ingawa haina maana kwamba kukamatwa kwao uhalifu huu utapungua. Wizi huu una mtandao mpana sana kwa vile hata wahalifu hao wamedokeza kuwa wamekuwa wakishirikiana na wataalamu wa kompyuta kutoka nchini Bulgaria,” alisema.

Vifaa walivyokamatwa navyo
Vifaa vilivyokamatwa navyo ni kadi za bandia 194 za kuchukulia fedha katika ATM za Benki ya NMB, ambapo kati yake kadi 95 zilikuwa na namba 0225152975 zinazotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina na picha ya mtu anayedaiwa kuwa ni mtumiaji mwenye jina la Molely L. P. Kadi nyingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti namba 5068000322 zikitumia jina moja la Mnuo Z. E na picha moja.

Mbali na kadi hizo pia waliweza kunasa kadi 36 za Benki za DTB, ambazo kati yake kadi 18 zilikuwa na jina moja la Kelvin G. Gratias na namba 20497883, kadi 12 zikitumia jina la John J. Paul zenye akaunti namba 2049783 huku kadi sita zikitumia jina moja la Joseph Donald akaunti namba 2049783.

Kadi nyingine tatu zenye maandishi ya Download List na nyingine ikiwa ni kadi ya Visa ya Benki ya KCB yenye namba 4183546040003827 zikitumia jina la Elikana Zacharia. Kadi nyingine zilikuwa ni tupu zisizo na maandishi wala nembo ya benki yoyote na nyingine zikiwa ni Soviet Royalty, kadi ya raia ya Urusi ikiwa na namba 000724.

Pia walikutwa na kadi ya Benki ya Amerikani yenye namba 549012345678 zilizokuwa zikitumia jina la Richard Croswell.

Walikamatwa pia wakiwa na vifaa mbalimbali vya kielektroniki ikiwamo kamera za siri tatu za kienyeji ambazo zimetengenezwa kwa kufungwa betri za simu ya mkononi na pia walikamatwa na kifaa cha kutengenezea kadi bandia (Magnetic Card reader), mikebe mitatu ya rangi za kupulizia kamera za usalama katika ATM ili wasionekane wakati wa wizi wao, ‘printer’ pamoja na kifaa cha kuchomea vifaa vya umeme.

Wizi ulivyofanyika
Wahalifu hufika katika mashine za kutolea fedha ambapo hatua ya kwanza ni kuzima kamera za usalama za eneo husika kwa kuzipulizia rangi maalumu ili kuzitia ukungu hivyo kuharibu mwonekano wake na kuruhusu wao kuingia eneo hilo bila ya kuonekana na kufanya wizi wao.
Mara baada ya kuziharibu kamera za usalama, walikuwa wakianza kwa kuweka kamera zao za siri ili kunasa namba za siri za kufungulia akaunti ambazo huzisoma katika ‘kompyuta’ na kuzinakili katika daftari lao maalumu na kisha kuchukua kadi zao bandia na kuchukua fedha.

Wizi huo wa kuchukua fedha waliufanya nyakati za usiku saa sita hadi saa tisa usiku wakati ule wa kutegea kamera zao ulifanyika muda ambao huwa na wateja wengi hasa siku za mapumziko.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.