Skip to main content

PISTORIUS:AFUNGUKA KUMUUA MPENZI WANGU



JOHANNESBURG, Afrika Kusini

MCHEZAJI nyota wa michezo ya walemavu, Oscar Pistorius amesisitiza kuwa, hakuwa amedhamiria kumuua mpenzi wake, Reeva Steenkamp.

Pistorius alisema hayo juzi kupitia taarifa iliyosomwa mahakamani kuhusu tuhuma za kumuua Reeva katika tukio lililotokea nyumbani kwake Februari 14 mwaka huu.

Mshtakiwa huyo alidai kuwa, alimuua Reeva kimakosa kwa kuhisi ni mwizi aliyeingia nyumbani kwake kupora baada ya kushtuka kutoka usingizini usiku wa manane.

Awali, Mwendesha Mashtaka Gerrie Nel aliieleza mahakama kuwa, Pistorius aliamka kitandani na kuvaa miguu yake ya bandia na kutembea umbali wa mita saba kabla ya kumfyatulia risasi Reeva kupitia kwenye mlango wa bafu uliokuwa umefungwa.

Nel aliieleza mahakama kuwa, mauaji hayo yalikuwa yamepangwa na mtuhumiwa baada ya kutokea ugomvi kati yake na marehemu.

Lakini Pistorius aliieleza mahakama kuwa, alishtuka kutoka usingizini baada ya kusikia sauti kutoka bafuni, akiamini alikuwa mwizi.

Mshtakiwa huyo alidai kuwa, alipiga kelele kabla ya kufyatua risasi kupitia kwenye mlango wa bafu.

Alidai kuwa, baadaye aligundua kwamba Reeva hakuwepo kitandani na ikamjia hisia kwamba, huenda ndiye aliyekuwemo bafuni wakati huo.

Mshtakiwa huyo aliieleza mahakama kuwa, alilazimika kutumia kifaa cha kuchezea kriketi kuvunja mlango wa bafuni na kumkuta Reeva akiwa amelala sakafuni.

Pistorius alidai kuwa, alimkuta Reeva akiwa bado yupo hai na kuamua kupiga simu kuita gari la wagonjwa kabla ya mchumba wake huyo kupoteza maisha akiwa mikononi mwake.

"Nilishindwa kuelewa nitafunguliwaje mashtaka ya tuhuma za mauaji kwa sababu sikupanga kumuua mpenzi wangu,"alidai mwanamichezo huyo.

Kwa mujibu wa Pistorius, amekuwa na kawaida ya kulala na bastola kitandani kwake tangu alipopata vitisho vya kuuawa na kwamba alipoinuka kitandani kwenda bafuni, hakuwa amevaa miguu yake ya bandia.

Wakati taarifa hiyo ikisomwa mahakamani, Pistorius alikuwa akilia na kutetemeka.Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Desmond Nair.

Wakili Barry Roux, anayemtetea Pistorius aliieleza mahakama kuwa, Reeva hakuwa ameuawa kwa makusudi na kwamba zipo kesi nyingi za aina hiyo, ambazo baadhi ya watu waliwaua ndugu wa familia zao kupitia madirishani kwa kuwahisi wezi.

Pistorius alishinda medali mbili za dhahabu na moja ya fedha katika michezo ya Olimpiki ya Walemavu iliyofanyika 2012 mjini London, Uingereza.

Wakati huo huo, mazishi ya Reeva yalifanyika juzi nyumbani kwake katika mji wa Port Elizabeth.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...