Skip to main content

Matokeo ya Form Four ni kioja kingine!


Photo: Matokeo ya Form Four ni kioja kingine!
Ndugu zangu,
Jioni yote hii nilikuwa nimepumzika kujisomea tu, hata taarifa ya habari imenipita. Muda huu nilipoingia mtandaoni nakutana na habari hii ya kusikitisha; matokeo mabaya ya kidato cha nne!
Namkumbuka jamaa yangu aliyeniuliza; " Maggid, unatarajia nini pale unapoona mwalimu anahonga ili apewe nafasi ya kwenda kusahihisha mitihani?" Kioja hiki!
Nakumbuka pia miaka kadhaa iliyopita. Mzazi kule Musoma alikwenda kulalamika kwa Mwalimu Mkuu aliposikia mtoto wake amefaulu mtihani wa darasa la saba na amechaguliwa kujiunga na Sekondari. Mzazi yule akauliza kwa kushangaa; " Hivi aliyefaulu ni mtoto wangu huyu huyu ambaye mpaka hii leo hajui vema kusoma na kuandika?"- Kioja!
Na nimeona, kwenye matokeo yaliyotoka hii leo, kuwa kwenye shule iliyopewa jina la  Sekondari ya J. M. Kikwete  wanafunzi wote wamefeli! Kioja hiki!
Tunajifunza nini?
Tuna MGOGORO WA ELIMU- Education Crisis. Ni mgogoro wa kitaifa. Tuna lazima ya kutafuta suluhu ya pamoja kama taifa.  Hapa si mahala pa kutanguliza siasa za vyama. Inahusu taifa letu na mustakabali wake.
Hivi tunajua? Kuwa umejengeka mfumo sasa wenye kuashiria kuwa kuna ' Ubaguzi wa Kielimu'. Kwamba matokeo haya mabaya ya Form Four yanawahusu zaidi watoto wa makabwela na kwenye shule za makabwela.
Ni matokeo ya Serikali kutowekeza rasilimali nyingi kwenye shule za Msingi na Sekondari za umma ( Public Schools). Hii ni pamoja na kuhakikisha walimu kwenye shule hizo wanapata mafunzo yenye ubora vyuoni, na pia wanapata mishahara na marupurupu ya kuwafanya wajivunie kuwa walimu kwenye shule za umma- public schools.
Kuna tunaokumbuka, kuwa enzi zile, sisi tuliosoma kwenye Sekondari za Serikali, ndio tulioonekana kupata bahati ya kwenda kwenye shule zilizo bora kuliko zile za binafsi. Ni kwa sababu, mfumo wetu wa elimu haukuwa wa kibaguzi. Kwamba darasa la shule ya msingi niliyosoma mimi pale Kinondoni , alisoma pia mtoto wa Waziri wa Maji, Gwassa Sebabili.
Sekondari ya Tambaza niliyosoma mimi alisoma pia mtoto wa Mzee Ali Hassan Mwinyi, huyu huyu Dr. Hussein Mwinyi. Hivyo, Baraza la Mawaziri lilipokutana na kuzungumzia matatizo ya elimu, kimsingi walizungumzia matatizo ya elimu ya watoto wao katika shule ambazo watoto wao wamechanganyika na watoto wa makabwela.
Leo hii kama kwenye Baraza la Mawaziri atatokea Waziri atakayezungumzia matatizo ya shule ya Sekondari ya Kata anayesoma mwanawe pale Makumbusho, basi, kuna wenzake watakaomwangalia kwa mshangao, na kujiuliza pia; " Hivi huyu Mheshimiwa ameshindwa kumpeleka mwanawe hata pale Sekondari ya Saint nanihii!"
Naam, tunachokiona sasa ni kichuguu cha tatizo, mlima wenyewe hatujaufikia.  
NI JIONI YA KUSIKITISHA SANA. ( Picha hiyo juu niliipiga shule ya msingi Ikuvala, Kilolo, Iringa, miaka kadhaa iliyopita)
Maggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765

Ndugu zangu,
Jioni yote ya jana nilikuwa nimepumzika kujisomea tu, hata taarifa ya habari ilinipita.Nilipoingia mtandaoni nikakutana na habari hii ya kusikitisha; matokeo mabaya ya kidato cha nne!

Namkumbuka jamaa yangu aliyeniuliza; " Maggid, unatarajia nini pale unapoona mwalimu anahonga ili apewe nafasi ya kwenda kusahihisha mitihani?" Kioja hiki!

Nakumbuka pia miaka kadhaa iliyopita. Mzazi kule Musoma alikwenda kulalamika kwa Mwalimu Mkuu aliposikia mtoto wake amefaulu mtihani wa darasa la saba na amechaguliwa kujiunga na Sekondari. Mzazi yule akauliza kwa kushangaa; " Hivi aliyefaulu ni mtoto wangu huyu huyu ambaye mpaka hii leo hajui vema kusoma na kuandika?"- Kioja!


Na nimeona, kwenye matokeo yaliyotoka hii leo, kuwa kwenye shule iliyopewa jina la Sekondari ya J. M. Kikwete wanafunzi wote wamefeli! Kioja hiki!

Tunajifunza nini?
Tuna MGOGORO WA ELIMU- Education Crisis. Ni mgogoro wa kitaifa. Tuna lazima ya kutafuta suluhu ya pamoja kama taifa. Hapa si mahala pa kutanguliza siasa za vyama. Inahusu taifa letu na mustakabali wake.

Hivi tunajua? Kuwa umejengeka mfumo sasa wenye kuashiria kuwa kuna ' Ubaguzi wa Kielimu'. Kwamba matokeo haya mabaya ya Form Four yanawahusu zaidi watoto wa makabwela na kwenye shule za makabwela.

Ni matokeo ya Serikali kutowekeza rasilimali nyingi kwenye shule za Msingi na Sekondari za umma ( Public Schools). Hii ni pamoja na kuhakikisha walimu kwenye shule hizo wanapata mafunzo yenye ubora vyuoni, na pia wanapata mishahara na marupurupu ya kuwafanya wajivunie kuwa walimu kwenye shule za umma- public schools.

Kuna tunaokumbuka, kuwa enzi zile, sisi tuliosoma kwenye Sekondari za Serikali, ndio tulioonekana kupata bahati ya kwenda kwenye shule zilizo bora kuliko zile za binafsi. Ni kwa sababu, mfumo wetu wa elimu haukuwa wa kibaguzi. Kwamba darasa la shule ya msingi niliyosoma mimi pale Kinondoni , alisoma pia mtoto wa Waziri wa Maji, Gwassa Sebabili.

Sekondari ya Tambaza niliyosoma mimi alisoma pia mtoto wa Mzee Ali Hassan Mwinyi, huyu huyu Dr. Hussein Mwinyi. Hivyo, Baraza la Mawaziri lilipokutana na kuzungumzia matatizo ya elimu, kimsingi walizungumzia matatizo ya elimu ya watoto wao katika shule ambazo watoto wao wamechanganyika na watoto wa makabwela.

Leo hii kama kwenye Baraza la Mawaziri atatokea Waziri atakayezungumzia matatizo ya shule ya Sekondari ya Kata anayesoma mwanawe pale Makumbusho, basi, kuna wenzake watakaomwangalia kwa mshangao, na kujiuliza pia; " Hivi huyu Mheshimiwa ameshindwa kumpeleka mwanawe hata pale Sekondari ya Saint nanihii!"

Naam, tunachokiona sasa ni kichuguu cha tatizo, mlima wenyewe hatujaufikia.

NI SIKU YA KUSIKITISHA SANA. ( Picha hiyo juu niliipiga shule ya msingi Ikuvala, Kilolo, Iringa, miaka kadhaa iliyopita)

ImeaMaggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...