Skip to main content

Matokeo ya Form Four ni kioja kingine!


Photo: Matokeo ya Form Four ni kioja kingine!
Ndugu zangu,
Jioni yote hii nilikuwa nimepumzika kujisomea tu, hata taarifa ya habari imenipita. Muda huu nilipoingia mtandaoni nakutana na habari hii ya kusikitisha; matokeo mabaya ya kidato cha nne!
Namkumbuka jamaa yangu aliyeniuliza; " Maggid, unatarajia nini pale unapoona mwalimu anahonga ili apewe nafasi ya kwenda kusahihisha mitihani?" Kioja hiki!
Nakumbuka pia miaka kadhaa iliyopita. Mzazi kule Musoma alikwenda kulalamika kwa Mwalimu Mkuu aliposikia mtoto wake amefaulu mtihani wa darasa la saba na amechaguliwa kujiunga na Sekondari. Mzazi yule akauliza kwa kushangaa; " Hivi aliyefaulu ni mtoto wangu huyu huyu ambaye mpaka hii leo hajui vema kusoma na kuandika?"- Kioja!
Na nimeona, kwenye matokeo yaliyotoka hii leo, kuwa kwenye shule iliyopewa jina la  Sekondari ya J. M. Kikwete  wanafunzi wote wamefeli! Kioja hiki!
Tunajifunza nini?
Tuna MGOGORO WA ELIMU- Education Crisis. Ni mgogoro wa kitaifa. Tuna lazima ya kutafuta suluhu ya pamoja kama taifa.  Hapa si mahala pa kutanguliza siasa za vyama. Inahusu taifa letu na mustakabali wake.
Hivi tunajua? Kuwa umejengeka mfumo sasa wenye kuashiria kuwa kuna ' Ubaguzi wa Kielimu'. Kwamba matokeo haya mabaya ya Form Four yanawahusu zaidi watoto wa makabwela na kwenye shule za makabwela.
Ni matokeo ya Serikali kutowekeza rasilimali nyingi kwenye shule za Msingi na Sekondari za umma ( Public Schools). Hii ni pamoja na kuhakikisha walimu kwenye shule hizo wanapata mafunzo yenye ubora vyuoni, na pia wanapata mishahara na marupurupu ya kuwafanya wajivunie kuwa walimu kwenye shule za umma- public schools.
Kuna tunaokumbuka, kuwa enzi zile, sisi tuliosoma kwenye Sekondari za Serikali, ndio tulioonekana kupata bahati ya kwenda kwenye shule zilizo bora kuliko zile za binafsi. Ni kwa sababu, mfumo wetu wa elimu haukuwa wa kibaguzi. Kwamba darasa la shule ya msingi niliyosoma mimi pale Kinondoni , alisoma pia mtoto wa Waziri wa Maji, Gwassa Sebabili.
Sekondari ya Tambaza niliyosoma mimi alisoma pia mtoto wa Mzee Ali Hassan Mwinyi, huyu huyu Dr. Hussein Mwinyi. Hivyo, Baraza la Mawaziri lilipokutana na kuzungumzia matatizo ya elimu, kimsingi walizungumzia matatizo ya elimu ya watoto wao katika shule ambazo watoto wao wamechanganyika na watoto wa makabwela.
Leo hii kama kwenye Baraza la Mawaziri atatokea Waziri atakayezungumzia matatizo ya shule ya Sekondari ya Kata anayesoma mwanawe pale Makumbusho, basi, kuna wenzake watakaomwangalia kwa mshangao, na kujiuliza pia; " Hivi huyu Mheshimiwa ameshindwa kumpeleka mwanawe hata pale Sekondari ya Saint nanihii!"
Naam, tunachokiona sasa ni kichuguu cha tatizo, mlima wenyewe hatujaufikia.  
NI JIONI YA KUSIKITISHA SANA. ( Picha hiyo juu niliipiga shule ya msingi Ikuvala, Kilolo, Iringa, miaka kadhaa iliyopita)
Maggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765

Ndugu zangu,
Jioni yote ya jana nilikuwa nimepumzika kujisomea tu, hata taarifa ya habari ilinipita.Nilipoingia mtandaoni nikakutana na habari hii ya kusikitisha; matokeo mabaya ya kidato cha nne!

Namkumbuka jamaa yangu aliyeniuliza; " Maggid, unatarajia nini pale unapoona mwalimu anahonga ili apewe nafasi ya kwenda kusahihisha mitihani?" Kioja hiki!

Nakumbuka pia miaka kadhaa iliyopita. Mzazi kule Musoma alikwenda kulalamika kwa Mwalimu Mkuu aliposikia mtoto wake amefaulu mtihani wa darasa la saba na amechaguliwa kujiunga na Sekondari. Mzazi yule akauliza kwa kushangaa; " Hivi aliyefaulu ni mtoto wangu huyu huyu ambaye mpaka hii leo hajui vema kusoma na kuandika?"- Kioja!


Na nimeona, kwenye matokeo yaliyotoka hii leo, kuwa kwenye shule iliyopewa jina la Sekondari ya J. M. Kikwete wanafunzi wote wamefeli! Kioja hiki!

Tunajifunza nini?
Tuna MGOGORO WA ELIMU- Education Crisis. Ni mgogoro wa kitaifa. Tuna lazima ya kutafuta suluhu ya pamoja kama taifa. Hapa si mahala pa kutanguliza siasa za vyama. Inahusu taifa letu na mustakabali wake.

Hivi tunajua? Kuwa umejengeka mfumo sasa wenye kuashiria kuwa kuna ' Ubaguzi wa Kielimu'. Kwamba matokeo haya mabaya ya Form Four yanawahusu zaidi watoto wa makabwela na kwenye shule za makabwela.

Ni matokeo ya Serikali kutowekeza rasilimali nyingi kwenye shule za Msingi na Sekondari za umma ( Public Schools). Hii ni pamoja na kuhakikisha walimu kwenye shule hizo wanapata mafunzo yenye ubora vyuoni, na pia wanapata mishahara na marupurupu ya kuwafanya wajivunie kuwa walimu kwenye shule za umma- public schools.

Kuna tunaokumbuka, kuwa enzi zile, sisi tuliosoma kwenye Sekondari za Serikali, ndio tulioonekana kupata bahati ya kwenda kwenye shule zilizo bora kuliko zile za binafsi. Ni kwa sababu, mfumo wetu wa elimu haukuwa wa kibaguzi. Kwamba darasa la shule ya msingi niliyosoma mimi pale Kinondoni , alisoma pia mtoto wa Waziri wa Maji, Gwassa Sebabili.

Sekondari ya Tambaza niliyosoma mimi alisoma pia mtoto wa Mzee Ali Hassan Mwinyi, huyu huyu Dr. Hussein Mwinyi. Hivyo, Baraza la Mawaziri lilipokutana na kuzungumzia matatizo ya elimu, kimsingi walizungumzia matatizo ya elimu ya watoto wao katika shule ambazo watoto wao wamechanganyika na watoto wa makabwela.

Leo hii kama kwenye Baraza la Mawaziri atatokea Waziri atakayezungumzia matatizo ya shule ya Sekondari ya Kata anayesoma mwanawe pale Makumbusho, basi, kuna wenzake watakaomwangalia kwa mshangao, na kujiuliza pia; " Hivi huyu Mheshimiwa ameshindwa kumpeleka mwanawe hata pale Sekondari ya Saint nanihii!"

Naam, tunachokiona sasa ni kichuguu cha tatizo, mlima wenyewe hatujaufikia.

NI SIKU YA KUSIKITISHA SANA. ( Picha hiyo juu niliipiga shule ya msingi Ikuvala, Kilolo, Iringa, miaka kadhaa iliyopita)

ImeaMaggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.