Makundi ya haki za kibinadamu yaonya kuhusu hatari ya vurugu za hali ya juu katika uchaguzi wa Kenya
Hatari ya vurugu za kisiasa nchini Kenya ni "kubwa sana" kuelekea
uchaguzi wa mwezi ujao, Human Rights Watch (HRW) ilionya katika ripoti
iliyotolewa siku ya Alhamisi (tarehe 7 Februari).
Jeshi la Kenya likifanya doria mitaani
mjini Nairobi tarehe 29 Mei 2012, siku moja baada ya dazeni ya watu
kujeruhiwa katika shambulio la bomu. [Picha ya Simon Maina/AFP]
Ripoti ya kurasa 58 kikundi hicho, "Hatari Kubwa: Vurugu za Kisiasa na
Uchaguzi wa Kenya 2013", inasema uhaba wa maendeleo ya serikali ya Kenya
juu ya mageuzi iliyoahidi na kushindwa kushughulikia ukiukwaji wa haki
za kibinadamu zinaoendelea na uliopita vimechangia kuzua mivutano Kenya
yote kabla ya uchaguzi mkuu wa tarehe 4 Machi.
Ripoti ya HRW imetokana na kuwasaili watu 225 Kenya nzima, kukiwa na
wengi zaidi katika mikoa ya Kati, Pwani, Mashariki, Kaskazini Mashariki,
Nyanza na Bonde la Ufa.
Ripoti hiyo inapendekeza kwamba viongozi wa Kenya wachukue hatua za
haraka, ikiwa ni pamoja na kuwakamata na kuwashtaki kwa haki wale
wanaohusika moja kwa moja katika kuchochea au kuandaa vurugu, ili
kuhakikisha ufanyikaji wa uchaguzi wa amani na haki.
"Vurugu haziepukiki, lakini ishara za tahadhari ziko wazi sana kiasi cha
kutostahiki kupuuzwa," alisema Mkurugenzi wa HRW Afrika Daniel Bekele.
"Serikali imeshindwa kushughulikia sababu za vurugu ambazo zimezikumba
chaguzi za vyama vingi tangu mwaka 1992, na hasa mauaji ya 2007-2008,
kwa hivyo hatua za haraka zinahitajika ili kuwalinda Wakenya."
Kiasi cha watu 1,200 waliuawa na kiasi cha 300,000 kukimbia makazi yao
wakati wa vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007-2008, kwa mujibu wa Umoja
wa Mataifa.
Comments