Skip to main content

Taswira:Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka amemtaka Mwekezaji wa shamba la Mpunga la Kapunga(Kapunga Rice Project)kuachia hecta 1870 za Kijiji ili kumaliza mgogoro wa ardhi uliodumu kwa muda mrefu.

 Kiwanda cha mpunga
  Mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak akisoma taarifa fupi kwa waziri
 Profesa Tibaijuka akipata maelekezo ya shamba  kutoka kwa mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak ambaye alimweleza kuwa suala la kuachia ardhi atakutana na wabia wenzake watano ili kutoa majibu muda mfupi ujao.
 Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka akiongea na wananchi wa Mbarali
 Waziri akivuka mto Chimara
Katika ziara hiyo waziri alijionea jinsi tani zaidi ya 1800 za mpunga uliovunwa na mwekezaji ukiwa umehifadhiwa nje ya maghala kutokana na kukosekana na soko ndani na nje ya nchi hivyo kufanya kiwanda kuendeshwa kwa hasara.Picha Zote na Mbeya Yetu
--- 
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka amemtaka Mwekezaji wa shamba la Mpunga la Kapunga[Kapunga Rice Project]kuachia hecta 1870 za Kijiji ili kumaliza mgogoro wa ardhi  uliodumu kwa muda mrefu.

Rai hiyo ameitoa alipofanya ziara katika shamba hilo ambalo liliuzwa hecta 7370 badala ya 5500 ambazo ndizo zilizostahili na kuacha hecta 1870 ambazo ni eneo la kijiji kabla ya kukabidhiwa shamba la NAFCO kabla ya kubinafsisha.

Ziara hiyo imefanywa na Waziri ili kujiridhisha baada ya kupokea mgogoro huo kwa muda mrefu bila majibu ya kuridhisha kutoka kwa watendaji wake hivyo kama Waziri mwenye dhamana lazima atoe majawabu yenye uhakika badala ya kuolea majibu ofisini.

Profesa Tibaijuka alikutana na Uongozi wa Serikali ya kijiji kabla ya kukutana na Mwekezaji na kuhitimisha kwa kufanya mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kapunga ambao pia ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbarali Matayo Mwangomo,Mkuu wa wilaya ya Mbarali Gulamhusein Kiffu na wataalam mbalimbali kutoka wilayani na mkoani.

Waziri Tibaijuka aliwashukuru wananchi wa Kapunga kwa uvumilivu wao kwani licha ya mgogoro kudumu muda mrefu hawajafanya vurugu zozote hivyo alimtaka Mwenyekiti wa kjiji hicho Ramadhan Nyoni kudumisha amani na upendo ili kumaliza mgogoro huo bila uvunjifu wa sheria.

Profesa Tibaijuka alipata maelekezo ya shamba hilo kutoka kwa mmoja wa wakurugenzi, Mkurugenzi mtendaji Bwana Justin Vermaak ambaye alimweleza kuwa suala la kuachia ardhi atakutana na wabia wenzake watano ili kutoa majibu muda mfupi ujao.

Hata hivyo Bwana Vermaak alibainisha kuwa shamba hilo linakabiliwa na changamoto ya wizi wa mbolea na mpunga kutoka kwa baadhi ya wananchi hivyo kuzorotesha uzalishaji wa mpunga.

Aidha Vermaak alimwambia Waziri kuwa kuharibiwa kwa miundo mbinu ya mifereji ya maji kilometa 14 kutoka mto Ruaha kumepelekea kupungua kwa maji katika shamba hilo hivyo kulazimika kulima chini ya kiwango.

Pia Bwana Vermaak amemwambia Waziri kuwa wanalazimika kukodisha mashamba kutokana na kuombwa na wananchi wa Kapunga ingawa hakuwa wazi juu ya mikataba ya ukodishaji kuokana na mashamba hayo kukodishwa kwa shilingi 2,880,000 kwa plot na kutakiwa kulipa mwekezaji tani 24 hadi 27 za mpunga baada ya mavuno.

Wananchi wameonekana kushindwa kumudu gharama za uendeshaji kauli iliyoungwa mkono na Diwani wa Kata ya Itamboleo mheshimiwa Lwitiko Mwangosi ambaye amesema kuwa licha ya kulipia shilingi 1,680,000 mwaka jana lakini hakupata kitu baada ya mwekezaji kuchukukua mpunga wote aliovuna.

Baada ya kukutana na uongozi wa kijiji na mwekezaji Waziri alihutubia wananchi na kuwaambia kuwa hivi sasa mgogoro haupo baada ya kumwomba mwekezaji kuachia hecta 1870 na kuwataka wananchi kuwa na subira kwani suala hilo halitachukua muda mrefu na kama atakaidi basi taarifa ataiwasilisha kwa Rais kwani ndiye mwenye dhamana ya kufuta hati miliki ya ardhi.

Katika mkutano huo wanachi walipata fursa ya kuuliza maswali ambapo Emmanuel Kapalamba alimwambia wazri kuwa vijana wamekosa ardhi ya kilimo hivyo kufanya maisha kuwa magumu kiuchumina pia kwamba hawpati huduma za umeme na maji licha ya miundo mbinu kupita katika kijiji chao.

Kwa upande wa wanawake walimweleza waziri kuwa kijiji hakina zahanati kutokana na iliyokuwapo kuporwa na mwekezaji hivyo kulazimika kutembea umbali wa kilomita 26 ili kupata huduma za afya katika hospitali ya Chimala.

Mkutano ulifungwa kwa waziri kuchukua baadhi ya changamoto za maji,umeme na kilimo kuzipeleka kwa mawaziri husika ili kupata ufumbuzi wa kudumu.

Katika ziara hiyo wazir alijionea jinsi tani zaidi ya 1800 za mpunga uliovunwa na mwekezaji ukiwa umehifadhiwa nje ya maghala kutokana na kukosekana na soko ndani na nje ya nchi hivyo kufanya kiwanda kuendeshwa kwa hasara ambapo baadhi ya hecta hazijalimwa na nyingine kufanya majaribio ya zao la soya kinyume na mkastaba.

Na Ezekia Kamanga 

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.