Skip to main content

"Marekani, mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu"


Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, Marekani ni mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu duniani. 
Akizungumza leo mbele ya hadhara kubwa ya wananchi wa matabaka mbalimbali kutoka mkoa wa Qum kwa mnasaba wa maadhimisho ya kutimia miaka 36 tokea ilipojiri harakati kubwa ya kihistoria ya wananchi wa Qum tarehe 9 Januari 1978, Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei ameelezea matamshi ya chuki yanayotolewa na shakhsia, duru za kisiasa na vyombo vya habari vya Marekani yaliyo dhidi ya mfumo wa Kiislamu na wananchi wa Iran, yakiwemo madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini na kuongeza kuwa, kila mtu anazungumzia suala la haki za binadamu, lakini Wamarekani hawana haki hata kidogo ya kuzungumzia suala hilo, kwani serikali yao ni mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu duniani. 
Akielezea uungaji mkono unaofanywa na Marekani kwa utawala ghasibu wa Israel katika jinai zinazotendwa na utawala huo dhidi ya wananchi wa Palestina wakiwemo wakaazi wa eneo la Ukanda wa Gaza na hata kuwazuia wananchi hao wasipate huduma za chakula na madawa, Ayatullah Khamenei ameongeza kuwa, vitendo vyote hivyo vinaonyesha wazi ukiukaji wa haki za binadamu unaofanywa na utawala huo ghasibu ukishirikiana na serikali ya Washington. 

Comments