Skip to main content

MTANDAO WA KUMTOA JACK PATRICK WAUNDWA, JUX ATAJWA

Na Erick EvaristFAMILIA ya modo wa Bongo, Jacqueline Patrick aliyenaswa kwa msala wa madawa ya kulevya Macau- China inadaiwa kuunda mtandao kwa ajili ya kufanikisha zoezi la kumchomoa mrembo huyo mikononi mwa vyombo vya sheria.
Jacqueline Patrick.
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na familia hiyo (jina lipo), familia hiyo imeanza mchakato huo hivi karibuni hasa baada ya kudadisi kuhusiana na sheria za eneo alilokamatiwa (Macau) kutokuwa kali kisheria tofauti na maeneo mengine ya nchi hiyo kama Hong Kong.
“Wameandaa mikakati thabiti kwani wamegundua Macau ni tofauti na maeneo mengine ya China ambayo ukikamatwa na madawa ya kulevya na kuthibitika kuwa na hatia, hakuna msalie mtume, ni kitanzi tu. Macau sheria zao si kali sana, wanaweza wakafanikiwa kumchomoa hata kwa njia za panya,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
 
Jux.
“Kinara wa mtandao huo ni Jux yule wanayesema ni mpenzi wake Jack ambaye kwa sasa yupo China. Ndiye ambaye juzijuzi hapa aliposti picha mpya za Jack na kusababisha watu wajue mrembo huyo kaachiwa huru.”
Paparazi wetu alimtafuta dada yake Jack ambaye hakupenda kutaja jina lake  ambapo alisema inawauma kutojua hatima ya ndugu yao hivyo wameona bora wajipange kwenda kufuatilia sakata hilo kupitia kwa Jux waliyemtaja kama ni rafiki wa Jack.
“Tunasikia maneno mengi tofautitofauti, inatuuma sisi kama ndugu hivyo tutajichanga na tutawatuma ndugu wawili ili waweze kwenda kushughulikia suala la ndugu yetu. Katika mkakati huu tumepata na baadhi ya marafiki wa Jack ambao kwa sasa sitawataja,” alisema dada huyo.
Hata hivyo, imeelezwa ndugu hao wametahadharishwa kuwa makini kwani licha ya kusikia sheria za Macau si kali sana wasidharau kwani huenda wakawekewa mtego na kujikuta wameingia katika matatizo kama watajaribu kutumia mlango wa ‘uani’ kumtoa Jack.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.